Wimbo 24
“Si Sehemu ya Ulimwengu”
1. Yehova ametutenga,
Ni kwake tunajitoa.
Sisi si wa ulimwengu;
Kama Yesu tunakuwa.
2. Ulimwengu tuepuke,
Tufanye kazi ya Mungu.
Tuachane na ya mwili.
Ili tubaki milele.
3. Rafiki zake Yehova,
Wachukie ulimwengu.
Mateso yatakuwapo,
Na Mungu atatulinda.
4. Tunapiga moyo konde.
Yesu alituombea:
‘Walinde kwa jina lako.’
Tuangaliwe na yeye.