Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/90 kur. 1-4
  • Kuendeleza Matokeo Yetu Tukiwa Wahudumu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuendeleza Matokeo Yetu Tukiwa Wahudumu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KABILIANA NA HALI VILIVYO
  • KUFANYA HILO LIWE LENGO LETU
  • Uwe Stadi Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Toa Uangalifu Daima kwa Fundisho Lako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Njia za Kuboresha Kuhubiri Kwetu Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 1/90 kur. 1-4

Kuendeleza Matokeo Yetu Tukiwa Wahudumu

1 Kwa kuwa masilahi ya Ufalme yapasa kuchukua mahali pa kwanza maishani mwetu, tunapaswa kuchochewa tuwe mafundi katika huduma ikiwa kazi-maisha yetu iliyochaguliwa. (Marko 13:10) Hata tuwe tumekuwa tukihubiri kwa muda mrefu jinsi gani, tunataka kuendeleza matokeo yetu tukiwa wahudumu. Tunaweza kufanyaje hivyo?

2 Watu wengi ambao wamefaulu katika nyanja za kazi zinazotaka utaalamu wanaendelea daima kutafuta maarifa na ustadi wa kisasa. Riziki yao huenda ikategemea hilo. Pia tukiwa wahudumu wenye kudhamiria, tunahitaji kuwa wenye bidii yenye uendelevu ili kuendeleza uwezo wetu wa kufanya wanafunzi, kuwafundisha wengine juu ya Ufalme wa Mungu. Tunapaswa kutafuta mifikio mipya na tofauti ambayo inavutia watu wa aina zote.—Mt. 28:19, 20.

KABILIANA NA HALI VILIVYO

3 Kwa kuwa sasa Yehova anaharakisha kukusanywa kwa wenye mfano wa kondoo, wengi wetu tunawatembelea majirani wetu kwa ukawaida zaidi. Utendaji wa kutoa ushahidi uliongezwa na wahubiri na mapainia wengi mno unachokora shamba la ulimwengu. Kwa sababu ya utendaji wetu ulioongezwa, mahubiri yaliyokuwa na matokeo wakati fulani huenda sasa yasivutie watu tunaokutana nao. Huenda ubora wa huduma yetu ukahitaji kufanyiwa maendeleo.

4 Ni jambo la lazima kudumisha mtazamo chanya katika kusema na watu kusudi tuwe stadi sana katika kazi yetu. Kutumia vizuri madokezo yenye manufaa yaliyotolewa kwenye toleo la Julai, 15, 1988 la Mnara wa Mlinzi kwaweza kutusaidia katika hilo. Kielelezo ni ukurasa 16, fungu 6, linaloongea juu ya jinsi ya kutoa utangulizi wa kujijulisha katika njia ya kupendeza na iliyo chanya katika eneo unalozuru kila juma na ambako unajulikana sana. Habari inayohusu jinsi ya kufikia mtu aliyekuambia juma lililopita, “Mimi najihusisha sana na kanisa langu mwenyewe, nalo linashughulikia mahitaji yangu yote ya kiroho,” inapatikana kwenye ukurasa 16, fungu 5.

5 Je! umepata kufanyia kazi eneo lako ukifanya toleo la moja kwa moja la funzo la Biblia la nyumbani? Je! wewe unafanyia kazi eneo la kibiashara la kundi lenu? Je! inawezekana na kufaa kufanya ushahidi wa barabarani katika saa zinazofaa na zenye matokeo? Kwa vyovyote, pitia madokezo mazuri yaliyotolewa kwenye Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1988. Kutumia madokezo hayo kwaweza kutusaidia tuendeleze matokeo yetu tukiwa wahudumu.

6 Kuwa wenye matokeo pia kunatia ndani ukamili. (Efe. 6:13) Uwe chonjo kuona mahali ambapo jamaa zaidi ya moja zinaishi ndani ya nyumba. Watu wengine wanaishi kwenye vyumba vya chini ya ardhi, juu ya vijumba vya kuegesha magari, au kwenye sehemu nyinginezo ambazo si rahisi kuzifikia kupitia mlango wa mbele. Tafuta washiriki mbalimbali wa jamaa—mtu mzee-mzee zaidi ambaye kwa kawaida hangekuja kwenye mlango au mtu ambaye huenda akawa kazini wakati kwa kawaida ziara zinafanywa kwenye nyumba hiyo. Huenda ikawa kwamba kwa kuzuru saa nyingine, waweza kukutana na washiriki wengine wa jamaa. Kutoa ushahidi wa jioni pindi nyingi kunaandaa fursa hizo.

KUFANYA HILO LIWE LENGO LETU

7 Kuendeleza matokeo yetu katika huduma ni lengo linalostahili ambalo wengi wetu tunaweza kufikia. Inataka sala ya hisia za moyoni na kujitayarisha kimbele. Kuwa kwetu wenye matokeo katika utumishi wa shambani kunapoongezeka, huenda tukaweza kusaidia mtu mwingine afanye maendeleo ayo hayo.—Gal. 6:6.

8 Kumbuka, kazi yetu ya kufundisha haitakomeshwa na “dhiki kubwa.” (Mt. 24:21) Tunatazamia miaka mingi ya kuwasaidia watakaofufuliwa wajifunze njia za Yehova. Kwa hakika shangwe yetu wakati wa mileani itakuwa tele tuonapo waliofundishwa wakijitiisha kwa uaminifu-mshikamanifu kwa enzi ya Kristo. Kwa kuendeleza matokeo yetu katika kazi ya kuhubiri na kufundisha, tunaweza kutimiza mengi zaidi katika huduma yetu—ilete heshima na sifa kwa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki