Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA JANUARI 1
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pia, kazia toleo la Januari kama linavyotaarfiwa kwenye Matangazo. Andaa majina ya vichapo vya zamani vilivyo kwenye akiba yenu. Ikiwa vitabu vya zamani vilivyotajwa havipatikani, kazia matumizi ya kitabu Usalama Ulimwenguni Pote.
Dak. 20: Tangaza Kichwa cha Mazungumzo Kipya: Amani—Je! Waweza Kuipata? Kwa ufupi zungumza juu ya matangulizi yanayoweza kutumiwa na kupitia maandiko yaliyopendekezwa na kutoa madokezo juu ya jinsi hayo yaweza kuunganishwa na habari kuu. Painia au mhubiri mwenye uwezo atoe wonyesho wa kielelezo kifuatacho:
“Mimi natafuta watu ambao wangependa kuishi katika ulimwengu ulio huru na vita na jeuri. Katika karne hii peke yake kumekuwako mamia ya vita na visa vingine vyenye jeuri. Wewe unafikiri ni nini kinachohitajiwa ikiwa vita na jeuri vitaepukwa? Ni nani anayeweza kutokeza ulimwengu wenye amani kikweli? (Ruhusu jibu.) Tafadhali angalia ahadi ya Mungu ya kusimamisha hali zenye amani duniani pote hapa katika Zaburi 37:10, 11. (Soma.) Je! si wazi kwamba waovu wakiisha ondolewa vitendo vya jeuri na vita vitakuwa ni mambo ya wakati uliopita? Kwa hiyo tunaweza kuwaje kati ya wale watakaofurahia wingi wa amani? Tunatiwa moyo kwenye Zaburi 37:34 tushike njia ya Mungu. (Soma.) Kwa hiyo njia pekee ya kuhakikisha tunapata shangwe ya amani ya duniani pote iliyoahidiwa na Mungu ni kushika njia yake. Njia hiyo imeonyeshwa katika Biblia Takatifu na kichapo hiki kinatoa msaada wa kupata kuelewa na kitia-moyo cha kushika njia ya Mungu. Kwa kielelezo, . . . ” Halafu onyesha jambo fulani mahususi na kutoa toleo. Watie moyo wote watumie kichwa kipya mwisho-juma huu.
Dak. 15: “Kuongoza Mafunzo ya Biblia ya Nyumbani.” Mapitio ya Maswali na Majibu ya makala yenye kichwa hiki katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Mei 1989, ukurasa 1.
Wimbo 24 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JANUARI 8
Dak. 5: Matangazo ya kwenu na matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Tangaza mipango ya utumishi wa shambani kwa ajili ya mwisho-juma.
Dak. 25: Medical Document na Identity Card. Mwandishi ahakikishe kadi zinagawanywa na azungumze kwa ukamili barua ya Januari 1, 1990 juu ya Medical Document kwa ajili ya wahubiri waliobatizwa na Identity Card kwa ajili ya watoto wadogo wasiobatizwa wa mzazi au wazazi Mashahidi. Sababu na wasikilizaji juu ya ni kwa nini maagizo yanapasa kufuatwa kusudi kadi hizo zifane sana kwa ajili ya ulinzi wetu.
Dak. 15: “Kaa Chonjo Kutoa Fasihi za Biblia.” Mazungumzo ya Maswali na majibu ya makala. Unapozungumza fungu 5, tia ndani wonyesho wa mhubiri akichukua fursa ya kuanzisha funzo la Biblia mahali ambapo tayari mwenye nyumba ana kichapo (vichapo) kinachotolewa. Pia, fanya mahoji mafupi na mhubiri ambaye amefaulu kuangusha fasihi na kuanzisha mafunzo.
Wimbo 63 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JANUARI 15
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Tia ndani shukrani za Sosaiti za michango yote kama ilivyoonyeshwa kwenye taarifa za Desemba. Sifu kundi kwa ajili ya kutegemeza kimwili kazi ya Ufalme mahali penu na ulimwenguni pote.
Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kutumia Trakti kwa Matokeo.” Maswali na majibu. Unapozungumza mafungu 5 na 6, tia ndani maonyesho mawili yakionyesha jinsi (1) Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani na (2) Sababu Kwa Nini Unaweza Kuitumaini Biblia zaweza kutumiwa kuwa sehemu ya utangulizi. Si lazima kutoa mahubiri yote bali kuonyesha tu jinsi ya kufanya badiliko la kuingia kwenye Kichwa cha Mazungumzo. Kazia thamani ya kuchukua hatua ya kwanza kutumia trakti kwenye kila fursa. Tangaza mipango ya kundi ya utumishi wa shambani, na uwaalike wote washiriki.
Dak. 15: “Nawezaje Kuepuka Kufanya Kama Wenzangu Wanavyotaka?” Kwa busara mzee anayestahili azungumza mambo makuu kutoka Amkeni! Oktoba 1983 kurasa 12-14 pamoja na vijana wawili walio mfano mzuri. Sema kwa ufupi kwamba tamaa ya kutaka kuwa maarufu na kukubaliwa na marika ni yenye nguvu. Hata watu wazima waweza kuathiriwa na mkazo huo. Je! imekuwa rahisi kwa vijana kukabiliana na hilo? Wamefauluje kukinza hilo? Tumia maswali yanayotegemea makala hiyo kuvuta vijana hao waeleze wanavyohisi na kuonyesha jinsi inavyowezekana kusitawisha imara ya kukabiliana na mkazo wa marika. Toa maneno ya uthamini kwa ajili ya mfano mzuri ambao vijana katika kundi wanaweka. Yehova anapendezwa sana na mwenendo wao mzuri naye anastahiwa nao.—Mit. 27:11.
Wimbo 188 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JANUARI 22
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Pitia ratiba ya kundi ya utumishi wa shambani kwa juma hili. Watie moyo wote wanaoweza wafanye mipango ya utumishi kwa ajili ya mwisho-juma huu.
Dak. 20: “Kuendeleza Matokeo Yetu Tukiwa Wahudumu.” Maswali na majibu. Unapozungumza fungu 4, tia ndani maonyesho mawili mafupi juu ya matangulizi yaliyodokezwa katika mafungu 5 na 6 kwenye ukurasa 16 wa Mnara wa Mlinzi wa Julai 15, 1988. Yapasa yatolewe kwa njia ya moyo mweupe na iliyo chanya.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu au “Wewe Unaweza Kuhamisha Milima” ikitegemea Mnara wa Mlinzi wa Desemba 15, 1988, kurasa 25-7.
Wimbo 168 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA JANUARI 29
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. “Kutambulisha Majumba ya Ufalme.” Toa maelezo yanayohusu hali zenu.
Dak. 15: Mambo makuu ya Kitabu-Mwaka 1990. Hotuba iliyotayarishwa vizuri juu ya habari ya utangulizi katika Kitabu-Mwaka 1990. Taja matendo yenye kutokeza yaliyoonewa shangwe na watu wa Yehova ikiwa ni kwa sababu ya baraka ya Yehova juu ya utumishi wao wa bidii. Kwa kadiri wakati unavyoruhusu, simulia mengine ya mambo yaliyoonwa ya kutia moyo yaliyotolewa. Ripoti kutoka kwa ndugu zetu ulimwenguni pote zapasa kutusukuma sisi sote tushiriki kikamili katika utumishi wa Yehova. Watie moyo wote wanufaike kwa kusoma Kitabu-Mwaka.
Dak. 20: “Matangulizi Yenye Matokeo.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Toa wonyesho wa utangulizi ulioonyeshwa katika fungu 5. Pia onyesha mmoja wa matangulizi katika kitabu Reasoning (kur. 9-15) ambao ungefaa kwa ajili ya eneo lenu. Watie moyo akina ndugu wachukue kitabu Reasoning katika utumishi wa shambani na kukitumia katika kujibu maswali na kushinda vipingamizi. Watie moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Wimbo 108 na sala ya kumalizia.