Wimbo 30
“Wenye Bidii kwa Kazi Njema”
1. Tutie bidii kuhubiri
Juu ya Ufalme wa Mungu.
Jina la Yehova ni Tukufu.
Daima sisi tumwabudu.
2. Upendo wetu uwe wa moyo,
Sisi tutumikie ndugu.
Har–Magedoni yakaribia,
Tuimarike hudumani.
3. Bidii kwa ajili ya Mungu.
Imani, tumaini, pendo.
Utumishi unaturidhisha,
Kama moto ndani ya moyo.
4. Imara katika majaribu.
Upendo usiwe baridi.
Bidii ya kutetea jina
La Yehova na tuzidishe.