Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/90 uku. 12
  • Kutangaza Habari Njema Kwa Kuzungumza na Watu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema Kwa Kuzungumza na Watu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TUMIA TULIVYO NAVYO
  • TANGULIA KUJITAYARISHA
  • Jinsi ya Kuboresha Stadi za Mazungumzo
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kutoa Habari Njema—Kwa Utambuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Matangulizi Yenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Je! Wewe Unatumia Utangulizi Unaofaa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 10/90 uku. 12

Kutangaza Habari Njema Kwa Kuzungumza na Watu

1 Kulingana na kamusi moja, mazungumzo ni “badilishano la hisia, maoneleo, maoni, au mawazo kwa mdomo.” Lakini waweza kuanzishaje mazungumzo yanayotegemea Biblia wakati watu unaokuta huenda wakawa wanapinga mazungumzo ya kidini au wanashughulika na mambo yao wenyewe? Yesu aliuliza maswali ili kuhusisha wasikilizaji.—Yn. 4:9-15, 41, 42.

2 Yatupasa tusali kwa Yehova kwa bidii atusaidie tupate watu wenye mioyo yenye ufuatiaji haki na atufungulie njia tuzungumze nao. Kutoa ushahidi kunakuwa rahisi zaidi ikiwa tunamwona kila mwenye nyumba kuwa yawezakana akawa mtumishi wa Yehova. Hali hiyo ya akili itatusaidia tuwasilishe ukweli kwa njia ya uchangamshi, yenye weupe wa moyo ambayo itavuta wenye kupendezwa.

TUMIA TULIVYO NAVYO

3 Kitabu Kutoa Sababu kinatoa matangulizi mengi bora katika kurasa 9-15. Mengi ya hayo yanafanya utumizi wenye mafanikio wa maswali. Mwenye nyumba anapoitikia swali, sikiliza kwa staha na kisha ujibu kwa njia ambayo itamwonyesha mwenye nyumba umefikiria yale ambayo amesema.—Kol. 4:6.

4 Bila shaka, uulizapo swali, hujui mwenye nyumba atajibuje. Uwe tayari kurekebisha mazungumzo yako kulingana na asemayo. Jaribu kuendeleza mazungumzo kwa kuingiza habari zaidi kutoka kwa Biblia inayoshughulika na mapendezi yake kwa kuuliza maswali zaidi yenye ufikirio.

TANGULIA KUJITAYARISHA

5 Huenda ukawa unafahamiana na njia ya kawaida ya kufikiri ya watu katika eneo lako. Ikiwa ndivyo, basi chagua matangulizi katika kitabu Kutoa Sababu yatakayokuwa yenye mafanikio zaidi katika eneo hususa lako. Kupatanisha mojapo matangulizi hayo na Kichwa cha Mazungumzo cha sasa huenda likawa ndilo jambo unalohitaji tu. Anza mazungumzo na mambo unayoamini kuwa ndiyo yanayohangaikiwa na mwenye nyumba, tokeza tatizo kifupi, kisha uongoze kwenye utatuzi wa Biblia. Anapotoa oneleo, toa elezo chanya, si kuchambua yale anayosema. Kupendezwa kwako na mawazo na hisia zake kwapaswa kumtie moyo aendelee kuzungumza nawe. Jaribu kupata mambo mnayokubaliana na kutoa maelezo juu yayo. Endeleza mazungumzo yakiwa chanya kwa kukazia baraka za Ufalme kama ndio utatuzi wa Biblia kwa matatizo ya binadamu.

6 Yaone maoni yenye kutofautiana kuwa njia za kuendeleza mazungumzo. Ikiwa mwenye nyumba ana nia ya kusababu, waweza kuuliza, “Je! wewe umepata kulifikiria kwa maoni haya?” Kisha onyesha yanayosemwa na Neno la Mungu juu ya habari hiyo. Ukipata kwamba mtu huyo hakubali sababu, usisisitize kwamba akubali uliyosema. Bali, malizia kwa maneno yenye urafiki ukiacha njia wazi kwa fursa ya wakati ujao ya kumtolea habari njema.—Mit. 12:8, 18.

7 Baadhi ya watu wanaelekea kuzungumza zaidi unapowakuta kwa njia isiyo rasmi. Usisite kuanza mazungumzo na watu unaokutana nao barabarani au wanaofanya kazi au wanaostarehe uani mwao. Huenda wakakaribisha kupendezwa kwako kihalisi na utendaji wao, na huenda ukaweza kuongoza mazungumzo yaingie katika maongezi juu ya ahadi ya Biblia kwamba dunia itakuwa paradiso karibuni. Unapoanza mazungumzo, jaribu kuyafanya yawe ono la kumpendeza mwenye nyumba. Kwa kadiri inavyokutegemea, mwache mtu huyo akiwa na mtazamo wenye kufaa zaidi kuelekea Mungu, Neno lake, na watumishi wake. Kwa njia hiyo, hata kama hukufanikiwa mwanzoni kufikia moyo wake, huenda akawa mwenye kusikiliza zaidi wakati mwingine Shahidi atembeleapo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki