Wimbo 130
Utumishi Wenye Furaha
1. Kwa furaha tutumikie Mungu,
Kwa vipawa hata ujuzi wetu.
Hata kazi ndogo yahakikisha
Moyo kamili, pendo, twaonyesha.
2. Utumishi wa Yehova ni mwingi,
Na wavunaji wanatakwa wengi.
Toka mbinguni tumeamuriwa;
Kwa kazi, sana tunabarikiwa.
3. Wawongo wajapokana ukweli,
Twajua ‘Mungu hasemi uwongo.’
Na tuhubiri Neno kwa bidii,
Kwa maana tuna hakika nalo.
4. Na kazi tamu tuishirikipo,
Kushuhudu wote tujaribupo,
Mungu atukubali chini hapa,
Tumutumikie, tumupe sifa.