Kuonyesha Kupendezwa Kibinafsi na Wengine
1 Kupendezwa kwa Yehova na wengine ni wazi sana. Je! yeye hakuandaa kwa ukarimu sana mahitaji ya vitu vya kimwili ya viumbe wake? (Mwa. 1:29, 30; 2:16, 17; Mt. 5:45; linganisha Luka 6:35.) Jambo la maana hata zaidi, je, yeye hakuonyesha kupendezwa kibinafsi nasi kwa kutuandalia ukombozi kutoka katika dhambi na kifo?—Yn. 3:16.
2 Yesu alipokuwa duniani, yeye aliiga kielelezo kikamilifu cha Baba yake katika kuonyesha kupendezwa kibinafsi na wengine. (Mt. 11:28-30; 1 Pet. 2:21) Wakati mtu aliyejawa na ukoma aliposema kwa Yesu, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa,” Yesu alijibu, “Nataka; takasika,” naye akamponya mtu huyo. (Mt. 8:2, 3) Akikaribia mji wa Naini, Yesu alikutana na mwandamano wa maziko ukibeba kijana, mwana pekee wa mama mjane, na kwa kusukumwa na sikitiko, Yesu alimrudisha kwenye uhai. (Luka 7:11-15) Bila kuulizwa, Yesu alionyesha kupendezwa kibinafsi na wengine. Hata watoto wadogo walionwa kuwa wastahili kupewa wakati na ufikirio wake, naye hakuwa na shughuli nyingi mno asiweze kufariji na kutia moyo wengine.—Mt. 20:31-34; Mk. 10:13-16.
FAMILIA NA MARAFIKI
3 Yatupasa sisi kujitahidi kuwa kama Yehova na Yesu Kristo katika kutafuta njia za kuonyesha kupendezwa kibinafsi na wengine. Kwa hiyo, acheni sisi tufikirie baadhi ya fursa za kufanya hivyo.
4 Mojawapo mahitaji makubwa zaidi ni ndugu kuonyesha kupendezwa kibinafsi na kihalisi na washiriki wa familia zao wenyewe na kutopuuza hali ya kiroho ya familia. Hilo latia ndani funzo pamoja na familia kwa ukawaida. Katika funzo la familia yako, je, wewe huzungumza habari katika njia ya kwamba inapendeza na ni yenye thamani yenye mafaa? Je! wewe hufuatia pia kwa kufanya kazi kwa ukawaida katika utumishi wa shambani pamoja na kila mshiriki wa watu wa nyumba yako? Je! wewe unajenga katika watoto wako tamaa ya kusaidia watu wengine, hivyo kuonyesha upendo wa Kikristo kwa jirani? Ikiwa umeoa na hamna watoto nyumbani, je, hata hivyo wewe huwa na funzo la familia?
5 Sisi tunataka kutoa usaidizi wa kiroho kwa kila mmoja tuwezaye. Lakini katika maisha zetu zenye shughuli nyingi, je, sisi husahau kuonyesha kupendezwa kibinafsi na washiriki wa kundi ambao wana mahitaji ya pekee? (Mit. 3:27; Gal. 6:10) Katika kundi la Kikristo, mna yatima, wenye umri mkubwa, wajane, walemavu, walioshuka moyo, wasiojiweza, na wengine ambao wana mahitaji ya pekee. Katika kumwiga Yehova na Mwana wake, Yesu Kristo, sisi hatupaswi kupuuza kuonyesha kupendezwa kibinafsi na ndugu na dada zetu wote.—1 Kor. 10:24; Flp. 2:4; Ebr. 13:16.
WENYE MFANO WA KONDOO SHAMBANI
6 Twaweza kuonyeshaje kupendezwa kibinafsi na watu ambao wana funzo la Biblia nyumbani? Wengi wao wameona uhitaji wa kuvunja ushirika na watu wa ulimwengu waliojuana nao. Hata ingawa sisi tuna shughuli nyingi, je, sisi huonyesha kupendezwa kibinafsi na hao wanafunzi na kufanya wale waliofanya mabadiliko wajisikie wanakaribishwa kuwa marafiki wetu wapya? Je! sisi ni chanzo cha kitia-moyo kwao hata ingawa si sisi tunaojifunza nao?—Linganisha Marko 10:28-30.
7 Je! wewe waweza kuwa na ushiriki zaidi katika kuonyesha kupendezwa kibinafsi kwa unyofu na watu ambao wana nia ya kusikiliza habari njema? Je! wewe utajaribu kuwasaidia watimize mahitaji yao ya kiroho? Wewe binafsi, waweza kufanya nini ili kuwa na ushiriki zaidi katika huduma ya shambani? Usijizuie ikiwa sasa uko katika hali ya kushiriki kikamili zaidi.—Luka 9:60-62.
8 Ni lazima sisi tumwige Yehova na Yesu katika kuonyesha kupendezwa kibinafsi na wengine. Sisi twahitaji kuwa wenye kuhurumia na kufikilia kusaidia, kama alivyofanya Yesu kwa habari ya mtu yule aliyejawa na ukoma. Ndiyo, sikuzote ni lazima sisi tuwe macho kuona njia ambazo katika hizo twaweza kuonyesha kupendezwa kibinafsi na wengine.