Wimbo 205
Kristo Mfano Wetu
1. Yehova ni mwenye Upendo, na mwema,
Mwanaye alimutuma!
Akiwa Mukate, Wanadamu wale
Ili waishi milele.
2. Yesu alifunza Tusali kwa Mungu:
’Litakaswe Jina lako.
Ufalme na uje. Mapenzi yafanywe.
Tupewe riziki yetu.
3. Alifunza kweli Akawafariji
Wasikia neno lake.
Akafa mutini Wote wawe huru
Afanye Neno la Mungu.
4. Tukiithamini Dhabihu ya Yesu,
’Takuwa “Kondoo” zake.
Siku zijawe na Kumusifu Mungu,
Tutavuna tunda naye.