Kupata Faida Zote za Kitheokrasi Desemba Huu
1 Imesemwa kuwa wakati ujao ni wa wale wanaojitayarisha kwa ajili yao. Ni lazima tupange kimbele ikiwa tunataka kutumia wakati wetu kwa njia ambayo itatuletea hisi ya kuridhika. Kwa mwezi wa Desemba, tunaingia katika kipindi ambapo tuna wakati mwingi zaidi unaopatikana kwa utendaji wa kibinafsi. Ni mipango gani tunayoweza kufanya sasa ili kuhakikisha utumizi bora kabisa wa wakati wetu kwa njia ya kitheokrasi?
2 Idadi kubwa ya watu waliopendezwa hivi karibuni ilihudhuria Ukumbusho katika Machi 30. Maendeleo yao ya kiroho yanategemea kwa kadiri kubwa juu ya msaada wanaopokea kutoka kwetu. Ingekuwa baraka kwao kuhudhuria mkusanyiko wa wilaya. Tunaweza kuwajulisha juu ya faida zao nyingi za kiroho na kuwasaidia na mipango yao ya kusafiri, labda tukiwaalika wasafiri pamoja nasi au na wengine katika kundi.
3 Kuhudhuria mkusanyiko hutoa fursa zaidi za kufanya ushuhuda wa kivivi hivi. Mipango ya kimbele yapasa kutia ndani kupakia ugavi wa vichapo vya karibuni. Tunaweza kuwatolea ushuhuda watu wanaofanya kazi katika stesheni za petroli, hoteli, na mikahawa, kutia na wale wanaosafiri kwa usafiri wa umma. Hii ni njia nzuri ya kuonea shangwe maono mengi yenye kusisimua.
4 Vijana siku zote hushirikisha Desemba na wakati wa mapumziko. Ingawa tafrija nzuri yaweza kuwa na mafaa, je! sehemu fulani ya wakati huu usiotumika yaweza kutumiwa kwa ushiriki zaidi katika kazi ya kutoa ushuhuda, kama vile upania msaidizi? Wazazi wanaweza kuanza sasa kuwasaidia watoto wao kufanya mipango. Labda watoto kutoka familia tofauti tofauti waweza kujiandikisha na kufanya kazi pamoja wakiwa kikundi. Wengine wasioweza kujiandikisha waweza kujitahidi kufanya mengi zaidi, hasa katika huduma ya katikati ya juma.
5 Wengi watapewa likizo kazini mwao na watasafiri kwenda sehemu nyingine. Kufanya mipango ili kuhudhuria mikutano ya kundi la mahali pao na kushiriki nalo katika huduma kwaweza kutokeza badilishano zuri la kitia moyo. Huenda ikawa unaenda sehemu ambayo kuna eneo lisilofanyiwa kazi mara nyingi, hilo likikuwezesha kutoa ushuhuda kwa watu wasioweza kusikia ujumbe wa Ufalme mara nyingi.
6 Vijana wengi wamemaliza shule juzijuzi au watamaliza shule hivi karibuni. Hili latokeza hangaiko zito kuhusu miradi yao maishani. Vijana wanaopangia wakati wao ujao kuhusiana na miradi ya kitheokrasi kwa hakika watabarikiwa. (1 Yn. 2:15-17) Uamuzi wa kuchukua utumishi wa painia wa kawaida waweza kutuongoza kwenye aina ya maisha yenye kuridhisha inayotia mapendeleo mengi ya pekee.
7 Kwa hiyo wengi wetu tutakuwa na wakati wa ziada. Acheni tutende kwa hekima, ‘tukiununua kabisa wakati unaofaa kwa ajili yetu wenyewe.’ (Efe. 5:15, 16, NW) Mipango inayotuweka tukiwa tumekazwa kwenye utumishi wa Yehova itatuletea sisi pamoja na wengine faida za milele.—1 Tim. 4:15, 16.