Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/92 kur. 1-2
  • Kutoa Habari Njema—Kwa Ushahidi wa Barabarani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Habari Njema—Kwa Ushahidi wa Barabarani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Ushahidi Barabarani kwa Njia Inayofaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Kuwapata Wenye Kupendezwa Kupitia Kutoa Ushahidi wa Barabarani Wenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Hubiri Habari Njema Kila Mahali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kuonyesha Uthamini kwa Mawonyesho Mawili Yaliyo Makubwa Zaidi Sana ya Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 7/92 kur. 1-2

Kutoa Habari Njema—Kwa Ushahidi wa Barabarani

1 Mithali 1:20 husema: “Hekima hupaza sauti yake katika njia kuu, hutoa sauti yake katika viwanja.” Maneno hayo ni kweli hasa leo ambapo watumishi wa Yehova wanahubiri habari njema za Ufalme kwa bidii mahali popote wanapoweza kuwapata watu. Kama vile Yesu na manabii wa kabla ya Ukristo, upendo wetu wa moyo mweupe kwa watu hutusukuma kutoa kweli kwa kila mtu, kila mahali.—Yer. 11:6; Mk. 6:56; Lk. 13:22, 26.

2 Ingawa nyumbani kwa mtu ndiko mahali bora zaidi kusema nao kuhusu kweli, si watu wengi wanaopatikana nyumbani tunapohubiri nyumba kwa nyumba. Wenye nyumba wanapokuwa nyumbani, mara nyingi ni mtu yule yule tuliyesema naye wakati uliopita anayefungua mlango, na washiriki wengine wa familia hawapati ujumbe. Kwa hiyo, kutoa ushahidi barabarani kwapaswa kuwe sehemu ya maana katika huduma yetu. Huenda ukapata kwamba eneo la barabarani ni ‘lenye kusisimua, jipya, na lenye kupatikana watu,’ kama alivyoeleza painia mmoja.

3 Mabadiliko ya hali na mambo ya hivi karibuni yanafanya iwezekane kutoa ushahidi barabarani kwa mara nyingine tena katika mahali pengi. Tafadhali fuateni mielekezo, maagizo, na miongozo kutoka kwa wazee kuhusu eneo na mara ambazo maeneo fulani yanahubiriwa. Makundi katika baadhi ya miji mikubwa yamepokea madokezo na miongozo fulani katika barua ya Juni 2, 1992. Tafadhali shirikianeni kwa kufuata maagizo hayo ili kutimiza mambo mengi mazuri. Kumbukeni kwamba kutoa ushahidi barabarani kwaweza kufanywa katika eneo la mtu binafsi, katika ujirani, au sokoni.

4 Mwelekeo Chanya Wenye Uchangamfu: Kwa nini usijaribu kutoa ushahidi barabarani sehemu ileile kwa ukawaida? Dada mmoja anayefanya hivyo anasema amefahamiana na wauzaji wengi na watu wengineo wanaokuwa kwenye barabara “yake.” Uhusiano mzuri umekua, ukifungua njia kwa mazungumzo mengi ya Biblia yenye matokeo. Painia msaidizi mmoja anayefurahia sana kutoa ushahidi barabarani alisema kwamba yeye hujaribu kuwahubiri watu wanaotazama vitu kwenye madirisha ya maduka, watu wanaoketi kwenye magari yao, watu wanaongoja mabasi, na hata wale waliokataa kusikiliza nyakati zilizopita. Ujasiri na uamuzi mzuri unahitajiwa ili kuwa hodari na wenye kusadikisha, na bado tusiwe wenye kusisitiza mno.

5 Ufunguo wa kutoa ushahidi barabarani kwa matokeo ni kuwafikia watu tukiwa wachangamfu, wenye kusisimuka, na wenye moyo mweupe. Tabasamu. Ikiwa unaweza, vuta uangalifu wa mtu huyo, lakini ikiwa huwezi, anzisha mazungumzo kwa urafiki. Chunguza hali, na kuzitumia kwa faida. Dada mmoja huchunguza wanawake waliobeba vikapu vya bidhaa na kusema, “Ninaona umekuwa ukinunua vyakula. Kwa kweli siku hizi vyakula ni ghali. Namna gani nikikupa chakula chenye kukutia moyo cha akilini na moyoni? Nilifurahia makala hii . . . .” Kwa mtu mwenye watoto, yeye husema, “Ninaona una watoto wawili wazuri. Je! ulijua kwamba Biblia husema kwamba watoto ni baraka kutoka kwa Mungu? Ebu nikuonyeshe . . . .” Ili kuanzisha mazungumzo na mtu aliye katika fikira nzito, yeye husema, “Ninaona kwamba unafikiria jambo fulani. Ulimwengu umejaa sana matatizo leo, sivyo? Je! unafikiri kutakuja kuwa na wakati ambapo . . . ?”

6 Ikiwa mtu anatembea haraka barabarani, huenda ukampa tu trakti na kusema, “Hii ni habari njema ya kusoma unapopata wakati.” Ikiwa watu hawaonekani wakiwa na haraka, basi toa magazeti. Ni vema kuwapa watu fasihi hiyo inapowezekana.

7 Wahubiri wengi waliokuwa na wasiwasi pale mwanzoni kuhusu kutoa ushahidi barabarani sasa huona aina hiyo ya mahubiri kuwa yenye kupendeza zaidi. Bila shaka, ni lazima tuwe waangalifu tunapohubiri maeneo yenye hatari au katika nyakati ambapo si salama. Hata katika miji midogo, mara nyingi kuna sehemu zenye shughuli nyingi, vituo vya usafiri wa umma, au sehemu za kuegeshea magari ambapo mazungumzo ya habari njema yanaweza kuanzishwa na watu. Tumia fursa hiyo, na kwa hekima sauti yako na itoe habari njema barabarani na peupe, kwa baraka ya wale wasikiao na kwa heshima ya Yehova.—Mit. 1:20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki