Wimbo 82
Wanawake Ni Jeshi Kubwa
1. Yehova asema mwenyewe.
Wahubiri wanawake;
Dada hao ni jeshi kubwa;
Wanatangazia watu.
Waamuka mapema sana
Watunze jamaa zao.
Kwa kutangulia kupanga,
Wanashiriki huduma.
2. Dada hawa, tunaombea,
Baraka tele za Mungu.
Wanatimiza mengi sana,
Sisi ndugu twawasifu.
Wengi wajane, wa zamani,
Wakabili matatizo.
Hawakosi mikutanoni;
Nao wadumu mbioni.
3. Tujali hawa ambao ni
Mama, mabinti na wake.
Wanayashiriki mavuno,
Kuziokoa maisha.
Jeshi hili linasifika.
Bidii yao faida.
Na tuwajali kwa huruma.
Mungu ‘hakusema’ bure.