Wimbo 128
Fanya Zaidi—Kama Walivyofanya Wanadhiri
1. ’Nadhiri—Tuwe kama hao.
Tutende kama wao.
Walitengwa wawe wa Mungu
Kwa njia ya pekee.
Chunguza! Fikiria hilo.
Wakati wamalizika.
Tuzidishe utumishi,
Tupa’ze sauti.
2. ’Nadhiri—Hawakutamani.
Walijinyima sana.
Walikaribia Yehova.
Nasi tufanye hivyo.
Walikuwa na vizuizi;
Kwa kuwa walinadhiri.
Na wengi wa ndugu zetu,
Wanaishi hivyo.
3. ’Nadhiri—Tofauti sana,
Wakawa na ishara.
Walifanya mengi zaidi;
Wakawa watiifu.
Kwa kufanya kazi na Mungu
Kwa imani tunatii
Yehova atubariki,
Na kutuhimiza.
4. ’Nadhiri—’Kaweka mufano.
Kuwa watakatifu.
Kama wao tusichafuke;
Na walibarikiwa.
Hesabu gharama halafu
Utumaini Yehova.
Uwe mustari wa mbele,
Ufurahi sana.