Jenga Kupendezwa kwa Kufanya Ziara za Kurudia Zenye Matokeo
1 Kila hotuba yenye kutayarishwa vizuri inatia ndani utangulizi wenye kuamsha kupendezwa, habari yenye kuarifu, na umalizio wenye kusukuma. Utangulizi unavuta uangalifu wa wasikilizaji, lakini bila habari na umalizio, hotuba haingekuwa kamili. Kanuni iyo hiyo yatumika kwa huduma yetu. Ni jambo zuri kuamsha kupendezwa kwa mwenye nyumba kwenye ziara ya kwanza, lakini ni lazima tuendelee kujenga kupendezwa huko kulikoonyeshwa mara ya kwanza kwa kufanya ziara za kurudia zenye matokeo.
2 Kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka? Hilo ni swali lenye kuchochea fikira kama nini! Je! hukubali kwamba habari hiyo imo akilini mwa watu wengi leo? Ndiyo sababu, katika makala iliyopo juu, ilidokezwa kwamba utokeze swali hilo mwishoni mwa ziara yako ya kwanza kwa kusudi la kulijibu unapofanya ziara ya kurudia.
3 Waweza kusema hivi:
◼ “Hujambo. Mara ya mwisho tulipoongea, habari juu ya Mungu kuruhusu kuteseka kulitokea, na niliahidi kurudi nikiwa na habari kwa ajili yako. Watu wengi huhisi kwamba ikiwa kwa kweli Mungu anatujali, yeye angekomesha kuteseka. Labda umehisi hivyo. [Mruhusu mwenye nyumba ajibu.] Biblia hutuhakikishia kwamba kweli Mungu anajali. [Soma 1 Yohana 4:8.] Mungu ana sababu nzuri za kuruhusu kuteseka kuendelee hadi sasa. Mojayapo sababu hizo inaelezwa kwenye 2 Petro 3:9. [Soma.] Sababu nyinginezo zinaelezwa katika broshua hii.” Kisha fungua kurasa 12-14 za broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? na uzungumze juu ya jambo lenye kupendeza.
4 Huenda wenye nyumba wengine wakapendezwa na elezo lenye ukamili zaidi, na huenda ziara za kurudia kadhaa zikahitajika kabla ya wao kutosheka kabisa na jibu. Vitabu kadhaa vya Sosaiti vilivyojalidiwa vyenye kurasa 192 vitakavyotolewa katika Januari vinatia ndani sura inayoweza kutumiwa ikiwa msingi wa mazungumzo zaidi juu ya habari hiyo.
5 Unapofikia mwisho wa mazungumzo, tokeza swali jingine na umwambie mwenye nyumba utafurahia kushiriki pamoja na yeye habari yenye kupendeza unaporudi. Watu wengi wangependa kujua lile linalompata mtu anapokufa. Kwa nini usipange kuzungumzia kichwa hicho kwenye wakati ufaao?
6 Ni msaada kwako kukumbuka kanuni tatu za msingi. Uwe mwenye kubadilikana. Huenda mwenye nyumba asizoee kuweka kando wakati hususa kwa ajili ya mazungumzo ya Biblia. Eleza mambo kifupi. Usikae muda mrefu sana au kupitia mambo mengi sana mwanzoni. Katika visa vingi, ukipitia mambo machache tu katika muda mfupi, ziara zako zitakuwa na itikio lenye kupendeleka zaidi. Uwe mchangamfu na mwenye urafiki. Mwonyeshe mwenye nyumba kwamba unapendezwa kibinafsi na yeye binafsi.
7 Lengo letu la mara hiyohiyo ni kumhusisha mwenye nyumba katika mazungumzo ya Kimaandiko. Kisha twataka kuanzisha funzo la Biblia lenye matokeo katika kichapo kinachofaa, kama vile kitabu Kuishi Milele. Shangwe yaweza kuwa yako ukijenga kwa saburi kule kupendezwa kulikoonyeshwa mara ya kwanza kwa kufanya ziara za kurudia zenye matokeo.