Wimbo 185
Ufufuo—Uandalizi Wenye Upendo wa Mungu
1. Ufufuo wa watu ni
Rehema ya Mungu,
Ni kwa kifo cha Yesu kwa
Upendo wa Mungu.
Kwanza ni wa “kundi dogo”;
Taji la uzima.
Kwa kufa waaminifu,
Wao watawala.
2. Na “wingu la mashahidi,”
Kupewa uzima.
‘Ufufuo ’lio bora’
Wameahidiwa.
“Kondoo wengine” nao
Wafao kwa sasa
’Tafufuliwa mapema
Watukuze Mungu.
3. Walio makaburini
’Tasikia Yesu
Kufurahi Paradiso,
Kama muhalifu.
Mwisho wa miaka elfu,
Jaribu la mwisho;
Wenye kuepa Shetani
Watabarikiwa.
4. “Mabaki” ya “kundi dogo,”
“Kondoo wengine,”
Ambia waliofiwa
Wataona wafu.
Zidisheni kazi Bwana
Alizoamuru.
Kifo hakiwazuii
Kuvuna thawabu.