Wimbo 52
Jina la Baba Yetu
1. E Yehova, Baba yetu,
Jina na litakaswe.
Na kusudi lako liwe,
Lisidharauliwe.
Karibuni litetewe,
Kwa ushindaji wako.
Sifa yako izidishwe;
Watu wote waone.
(Korasi)
2. Twatafuta njia za
Kutakasa jina lako;
Kwa ujasiri twasema
Sifa, kusudi lako.
Kwa imani uhodari,
Tukuheshimu wewe.
E Baba Mutakatifu,
Tuwe waaminifu.
(Korasi)
3. E Bwana Yehova Mungu,
Ni wewe Peke Yako.
Kutukuzwa kwa Yehova
Ni kwa maana sana.
Tunakweza jina lako;
Twataka kujulisha
U Mungu wa kusudio
Milele tubariki.
(KORASI)
Ewe Bwana, u Mufanyi;
Vyote uliviumba,
U Mungu wa makusudi,
Unayatekeleza.
E Yehova, Mungu Mweza,
Uliyetoa Mwana,
Mapenzi yako yafanywe,
Na yeye kwa Ufalme.