Wimbo 188
Zawadi ya Sala
1. Mungu anasikia
Washika neno lake.
Kupitia Yesu tu
Tumufikie Mungu.
2. Sala asikiazo
Ni zile za unyofu.
Zikitoka moyoni
Huwa zenye heshima.
3. Tusalipo kwa Mungu,
Sala zetu zisiwe
Wimbo wa kurudiwa,
Na ziwe changamufu.
4. Tusiache kusali
Twendapo uzimani.
Sala inafariji;
Zawadi toka Mungu.