Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/94 uku. 1
  • Hawajaacha Kutoa Ushahidi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hawajaacha Kutoa Ushahidi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Usisahau Kamwe Wewe Ni Shahidi!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kuonyesha Uthamini kwa Mawonyesho Mawili Yaliyo Makubwa Zaidi Sana ya Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Ongea Juu ya Utukufu wa Umaliki wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kutoa Ushahidi kwa Simu —Njia ya Kufikia Wengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 9/94 uku. 1

Hawajaacha Kutoa Ushahidi

1 Jina letu, Mashahidi wa Yehova, hututambulisha na kueleza yale tufanyayo. Sisi hutoa ushahidi kwa sifa bora za Mungu wetu, Yehova. (Isa. 43:10, 12) Kila mmoja lazima ashiriki katika kutoa ushahidi huu ikiwa atakuwa mshiriki wa kutaniko. Kutoa ushahidi kwafanywa hasa kupitia huduma yetu ya peupe, inayotia ndani kwenda nyumba kwa nyumba, mahubiri ya barabarani, kufanya ziara za kurudia, na kuongoza mafunzo ya Biblia. Sisi sote twasihiwa kwa kufaa tujitahidi kushiriki kikamili.—1 Kor. 15:58.

2 Hata hivyo, washiriki fulani wa kutaniko, wamepungukiwa katika yale wanayoweza kufanya. Ugonjwa au udhaifu mbaya unaweza kuwazuia. Watu wa ukoo wenye kupinga wanaweza kutokeza vizuizi. Kijana huenda akawekewa vikwazo na mzazi asiyeamini. Watu mmoja-mmoja wanaoishi katika maeneo yaliyo pekee yasiyo na usafiri huenda wakahisi hicho ni kizuizi. Haya ya kiasili yaweza kufanya wenye woga warudi nyuma. Baadhi ya wahubiri ambao wanajipata katika hali hizi au zinazofanana nazo huenda wakahisi kwamba hawastahili kuwa Wakristo kwa sababu yale wanayoweza kufanya ni kidogo sana kuliko yale wengine wanafanya na kidogo kuliko yale wanayotaka kufanya. Hakuna sababu ya kuona jitihada zao zikiwa ndogo sana. (Gal. 6:4) Wanaweza kupata faraja kwa kujua kwamba Yehova anapendezwa wanapotoa yaliyo bora zaidi katika hali yoyote ile wanayojipata.—Lk. 21:1-4.

3 Kutafuta Njia ya Kushiriki: Maelfu ya mambo yaliyoonwa yamesimuliwa kuonyesha jinsi watu mmoja-mmoja wakiwa kwenye hali ngumu hawajaruhusu vizuizi viwazuie kutoa ushahidi. Wakitumia nishati yao, wamebuni njia mbalimbali za kutoa ushahidi wa vivi-hivi. Wale waliowekewa mipaka ya kukaa nyumbani wametumia simu mahali zinapopatikana kufungua mlango ulio mpana wa kutoa ushahidi. Kila mgeni huonwa kuwa awezaye kuwa msikilizaji mwenye matokeo. Hata ingawa mke aliye na familia yenye kupinga huenda asiweze kutoa ushahidi nyumbani, yeye hutumia kwa manufaa fursa za kuongea na majirani au wengine anaokutana nao katika kawaida yake ya kila siku.

4 Kijana anaweza kukatazwa na mzazi asiyeamini kushiriki katika kutoa ushahidi wetu wa peupe. Badala ya kukubali jambo hilo kuwa kizuizi kikubwa sana, anaweza kuwaona wanadarasa-wenzi na walimu kuwa “eneo” lake la kibinafsi na aweze kutoa ushahidi mzuri na labda hata kuongoza mafunzo ya Biblia. Wengi wanaoishi katika maeneo yaliyo pekee wameweza kushiriki kwa kuandika barua. Wale wanaochochewa na bidii ya Kikristo sikuzote watapata njia ya kuepuka kuwa “wasiotenda ama wasiozaa matunda kuhusu ujuzi wa Bwana wetu Yesu Kristo.”—2 Pet. 1:8, NW.

5 Inapohusu ushiriki wetu katika kazi ya kutoa ushahidi, Yehova ameweka kiwango kinachofanana kwa wote, yaani, kwamba twapaswa kuwa wenye “nafsi yote.” (Kol. 3:23, NW) Ingawa kiasi cha wakati tunaotumia na yale tunayotimiza yatatofautiana, nia yetu ni ileile—upendo wa kweli utokao kwa “moyo mkamilifu.” (1 Nya. 28:9; 1 Kor. 16:14) Ikiwa tunatoa yetu yaliyo bora zaidi, hatutakuwa na sababu kamwe ya kuhisi kwamba tunapungukiwa na imani au hatufai tukiwa washiriki wa kutaniko kwa sababu kiasi tuwezacho kufanya ni kidogo. Kama vile Paulo, twaweza kusema kikweli kwamba ‘sikujizuia kuwaambia nyinyi lolote kati ya mambo yaliyokuwa yenye kuleta faida wala kuwafundisha nyinyi hadharani.’—Mdo. 20:20, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki