Wimbo 74
Yehova, Mwandalizi wa Wokovu
1. Leo unabii watimizwa sasa.
Shetani katupwa; ole kwa dunia.
Mungu akatawaza Yesu Bwana. Twaimba:
“Yah ataokoa.”
(Korasi)
2. Ushikamanifu unajaribiwa;
Roho ya ’limwengu yatushambulia.
Fikira na mwenendo uwe safi, Tutunze,
Tuje tuokoke.
(Korasi)
3. Upesi Kristo ataponda Shetani,
Na hakutakuwa kilio na kifo.
Na mbingu na dunia, Yah afanya Ni mupya,
Yah ametuponya.
(KORASI)
Yehova huokoa wa’minifu
Adui ’taona Yah ni Mwamba wa nguvu.
Bila woga, watu wa Mungu, twamusifu
Yah Yehova, Wokovu wetu, twamusifu.