Hukumu za Mungu Lazima Zitangazwe
“Lazima wewe uinuke na kunena kwa hao kila jambo ambalo mimi mwenyewe nakuamuru wewe. Usipatwe na ogofyo lo lote kwa sababu ya hao.”—YEREMIA 1:17, NW.
1. Ni jinsi gani Mashahidi wa Yehova ‘waliacha nuru yao ing’ae’ katika Ujeremani ya Nazi?
“MNYANYASO wa Mashahidi wa Yehova katika ule Ufalme wa Maangamizi Makubwa [Ujeremani ya Nazi] umetukia miongoni mwa nyakati nyingine za jaribu katika historia yao.” (Holocaust Studies Annual, Volume II—The Churches’ Response to the Holocaust) Karatasi-habari Daily News ya Afrika Kusini ya Julai 15, 1939, ilitaarifu hivi pia juu ya Mashahidi Wajeremani: “Kikiwa kama nuru ambayo haisinzii kamwe katika umulikaji, kikundi hiki kidogo cha wanaume na wanawake Wakristo kinasimama kwa uthibitifu katika imani yao, kikiwa mwiba wenye kuchoma ubavuni pa Mmaliki wa Munich [Adolf Hitler] na kikiwa ushuhuda ulio hai kwamba yeye si mtu asiyeweza kufa.” Maneno hayo yanatukumbusha kwamba Yesu alisema wafuasi wake wangekuwa “nuru ya ulimwengu” na ingekuwa lazima waache nuru yao iangaze mbele ya ulimwengu, bila kujali gharama ingekuwa nini.—Mathayo 5:11, 12, 14-16, NW.
2, 3. Ni kielelezo gani cha kuhubiri bila woga kilichotukia katika Sri Lanka?
2 Ripoti nyingine, kutoka Sri Lanka inayokumbwa na uvamizi-haramu, inaeleza juu ya Shahidi kijana wa lugha ya Tamili, David Gunaratnam, ambaye pasipo hofu aliwahubiria wenye mamlaka jeshini, kwa kufanya sawasawa na Yeremia. Kijana huyo mwanamume alikuwa amezingirwa pamoja na vijana wengine ili kuulizwa maswali. Ripoti hiyo inataarifu hivi: “Maafisa na wanaume hao walishangazwa sana na mwelimiko wa mwanamume huyo, na zaidi ya hilo, na weupe wake wa moyo ulioonekana wazi, hasa wakati yeye aliposema, ‘Na kama mimi ningekutana na wo wote wale wanaoitwa wavamizi-haramu, mimi ningewahubiria wao pia jambo hili hili.’”
3 Usiku huo huo yeye alitwaliwa nyumbani na wavamizi-haramu, ambao walimshtaki juu ya kufanya njama pamoja na jeshi. Yeye alisisitiza juu ya kutokuwamo kwake na akasema kwamba alikuwa akihubiri ujumbe wa Ufalme wa Mungu tu. “Mimi ninafanya kazi ya Mungu na nitaendelea kuifanya. Ninahubiri bila ubaguzi kwa mtu ye yote anayetaka kusikiliza.” Shahidi huyo mjasiri alipigwa risasi akauawa na hao wavamizi-haramu, akiacha nyuma mjane kijana na kitoto mvulana.—Linganisha Matendo 7:51-60.
4. Ni mnyanyaso gani wenye kibali cha viongozi wa kidini juu ya Mashahidi wa Yehova uliotukia katika nchi moja ya Latini Amerika?
4 Kutoka nchi moja ya Latini Amerika, ambako mnyanyaso wa Mashahidi wa Yehova umepewa kibali na kuachiliwa tu na viongozi fulani wa kidini Wakatoliki na Wapresbiteri, inakuja ripoti hii: “Kulikuwa na Mashahidi wa Yehova watano katika yale makao ya kijeshi . .. Wao walikuwa wakipigwa-pigwa na kuwekwa peke yao bila chakula. Afisa wa kisiasa katika kikosi chetu, mwenye daraka la kurekebisha tabia za watu kwa kujaza fikira ngeni katika akili zao, aliwaadhibu [Mashahidi] kwa sababu wao walihubiria askari wale wengine. Yeye alisema kwamba kati ya wakaidi wote wa kidini, Mashahidi wa Yehova ndio hatari zaidi.”
Kichochezi na Kitendo cha Kujibiza
5. Sawa na vile ilivyotukia katika kisa cha Yeremia, mara nyingi ni kitu gani kinachochochea mnyanyaso wa Mashahidi?
5 Ndiyo, sawa na vile Yeremia alivyonyanyaswa na watawala wa kidini na kisiasa wa siku yake, ndivyo Mashahidi wa Yehova wanavyoelekeana na upinzani ulimwenguni pote kutoka sehemu hizo hizo. Ni kitu gani kinachochochea vitendo hivyo? Hata ingawa Mashahidi ndio kikundi cha watu wenye kuamanika na kufuata sheria zaidi ya wote katika jumuiya yo yote, adui zao wanafikiria Neno la Mungu kuwa hatari, kwa maana wana uchungu kuhusu ujumbe walo wa Ufalme wa Mungu na wanaukataa. Mahubiri na kanuni wanazofuata bila kuacha msimamo wao zinafichua ubinafsi na udanganyifu wa sehemu za kisiasa, kibiashara, na kidini za mfumo wa Shetani.—Yohana 15:18, 19; 1 Yohana 5:19.
6. Hata hivyo Mashahidi wa Yehova wametenda jinsi gani kujibiza mnyanyaso?
6 Hata hivyo, ijapokuwa wamepatwa na vifungo gerezani, mapigo, na hata kifo, Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wamejibiza kwa kutenda kama Yeremia wa kale. Ingawa wanaonyesha upendo na nadhari, wao wanaendelea kuhubiria mataifa hukumu za Mungu zisizopendwa na wengi. (2 Timotheo 2:23-26) Wanajua ni lazima watii Mungu kuwa Mtawala kuliko wanadamu. (Matendo 4:19, 20; 5:29) Wao wanatia katika fahamu zao shauri la Paulo kwa Wakristo Waebrania, yaani, kuvumilia katika kufanya mapenzi ya Mungu. Ndipo watakapoona utimizo wa ile ahadi, uhai wa milele. Kwa hiyo, kama Paulo na Yeremia, inatupasa sisi tuweze kusema: “Sisi si aina ya warudio nyuma kwenye uharibifu, bali aina ya walio na imani kuhifadhi hai nafsi.”—Waebrania 10:35-39, NW.
Yeremia wa Ki-Siku-Hizi Afichua Jumuiya ya Wakristo
7. Mashahidi katika karne ya 20 wamefuata jinsi gani kielelezo cha manabii waaminifu wa Yehova waliotumwa kwa Israeli na Yuda?
7 Sawa na vile Yehova alivyoendelea kutuma manabii wake kwa Israeli na Yuda, yeye ametuma mashahidi wake wakautangaze kweli kweli ujumbe wa hukumu yake inayokuja. (Yeremia 7:25, 26; 25:4, 8, 9) Hasa tangu ule mwaka wa 1919 wenye kuwatia sulubu ya kiroho, mabaki wapakwa mafuta wa ndugu za Kristo walipeleka hukumu za Mungu bila woga kwa Jumuiya ya Wakristo, maujumbe makali ya maafa. (Linganisha Yeremia l1 9-13.) Katika mwaka huo gazeti The Golden Age lilitokezwa. Katika muda wa miaka iliyofuata, na likiwa na vichwa vilivyobadilishwa Consolation (1937) na Amkeni! (1946, kwa Kiingereza), gazeti hilo limetumikia kufichua uwongo wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo na Ukristo wayo bandia.
8, 9. (a) Kwa sababu gani makanisa yalilaumiwa waziwazi katika 1922? (b) Ni afa gani ambalo lilitabiriwa kwayo?
8 Mathalani, Golden Age la Oktoba 11, 1922, lililaumu waziwazi dini bandia kwa maneno haya: “Jitihada zote za matengenezo ya makanisa yenye madhehebu, viongozi wayo wa kidini, waongozi na wafungamani wayo, za kuokoa na kusimamisha upya ule utaratibu wa mambo katika dunia . . . lazima zikose kufanikiwa, kwa sababu wao si sehemu yo yote ya ufalme wa Masihi. Bali tofauti na hivyo, wakati wa Vita ya Ulimwengu [ya Kwanza] viongozi wa kidini wa madhehebu hizo mbalimbali za makanisa walikosa ushikamanifu kwa Bwana Yesu Kristo katika jambo hili, kwamba wao waliungana kimakosa pamoja na biashara kubwa na wanasiasa wakubwa kuendeleza ile Vita ya Ulimwengu.”
9 Hilo lawama la wazi liliendelea kusema: “Zaidi ya hilo wao walikataa katakata Bwana na ufalme wake na wakaonyesha ukosefu wao wa ushikamanifu kwa kujiunga na tengenezo la Shetani kwa kujitakia wenyewe, na kutangazia ulimwengu kwa ujasiri kwamba Ushirika wa Mataifa ndio wonyesho wa kisiasa wa ufalme wa Mungu duniani.” Hatimaye ukaja ule ujumbe wa “afa,” au hukumu: “Wakati mkubwa wa ‘dhiki ya namna ambayo haikuwako tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka wakati huu, la, wala haitakuwako tena kamwe,’ kulingana na maneno ya Kristo Yesu, sasa unaning’inia juu na uko karibu kuanguka juu ya mataifa ya dunia.”
10. Ni lawama gani la waziwazi lililofanywa katika 1926?
10 Fungu la kazi ya Yeremia lilipanuliwa kupitia utumizi wa vichapo vingine, kama gazeti Mnara wa Mlinzi, vijitabu, na vitabu. Mathalani, katika 1926 kitabu Deliverance kilitia ndani ufichuzi mkali wa mafundisho yenye kuongoza watu vibaya ya Jumuiya ya Wakristo. Katika ukurasa wa 203 huo unasema hivi: “Mafundisho bandia yaliingizwa kwa wingi [ndani ya Jumuiya ya Wakristo ya uasi-imani] na yakawekwa badala ya ukweli. Miongoni mwa hayo yalikuwamo na yangali yamo yale mafundisho ya utatu, kutokufa kwa nafsi zote, kuteswa-teswa milele kwa waovu, haki ya kimungu ambayo viongozi wa kidini wanayo, na haki ya kimungu ambayo wafalme wanayo kutawala. Baada ya muda kupita, Mariamu mama ya mtoto Yesu alifanywa kuwa mungu; na watu wakaja kumwabudu yeye kuwa mama ya Mungu.”
Jumuiya ya Wakristo Yenye Kuleta Migawanyiko Yaonywa
11, 12. (a) Ukosefu wa kutokuwamo wa viongozi wa kidini ulifichuliwa jinsi gani? (b) Ni onyo gani ambalo lilitolewa na jamii ya Yeremia?
11 Kichapo hicho hicho kilifichua ushiriki wa viongozi wa kidini katika vita, kikisema: “Viongozi wa kidini wa mifumo hii mbalimbali ya wahubiri-dini wanabariki majeshi ambayo yanatumwa nje na sehemu za kibiashara na kisiasa, nao wanawanyooshea baraka yao bila kujali majeshi hayo yanapigana yakiwa upande gani. Viongozi wote wa kidini wanasingizia kuwa wanampelekea sala Mungu yule yule mmoja ili abariki majeshi ya pande zote mbili yenye kufanya vita.” (Linganisha Yeremia 7:31.) Halafu ikagusiwa kwamba hukumu ilikuwa karibu sana: “Sehemu zote hizi ambazo zinaenda kufanyiza ile sehemu inayoonekana ya tengenezo la Shetani zinawekwa pamoja na kukusanyishwa kwa ajili ya lile pigano kubwa la Har–Magedoni.”—Ufunuo 16:14-16.
12 Sawa na ilivyokuwa katika siku ya Yeremia, wakati viongozi waliposema walikuwa salama na katika amani pamoja na Mungu, “ndivyo viongozi hao wahubiri-dini wanajiungamia wenyewe kwamba wako salama, kwamba kile tu ambacho wao wanahitaji ni kuitwa kwa jina la Kristo, huku wao wakiendelea kucheza na moto wa Ibilisi. Wao wanajipofusha wasione hali halisi iliyopo kwa kutia mchanga ndani ya macho yao wenyewe na pia ndani ya macho ya wanadamu wenzao.” (Deliverance, ukurasa 270) Kujidanganya kwao wenyewe kulifichuliwa na hao Wanafunzi wa Biblia wenye bidii, kama vile Mashahidi wa Yehova walivyojulikana wakati huo.—Mathayo 7:21-23.
13. Ni tukio gani ambalo lilitukia katika 1931, na kwa sababu gani lilifaa?
13 Kadiri wakati ulivyozidi kupita, Wanafunzi wa Biblia walihusianishwa na Yeremia kwa ukaribu zaidi, wakati, katika 1931, ilipotangazwa kwenye mkusanyiko mmoja katika Columbus, Ohio, U.S.A., kwamba jina la Kibiblia la kikundi hiki chenye ushujaa cha Wakristo linapasa kuwa “Mashahidi wa Yehova.” (Isaya 43:10-12) Jina hilo lilikuwa limetokezwa katika karne ya nane K.W.K. wakati Yehova alipolitumia kwa Israeli. Kwa hiyo, yapata miaka mia moja baadaye, wakati Yeremia alipotumikia akiwa nabii, yeye pia alikuwa shahidi kwa ajili ya Yehova. (Yeremia 16:21) Vivyo hivyo Yesu, alipokuja duniani akiwa Myahudi, alikuwa shahidi kwa ajili ya Baba yake, Yehova. (Yohana 17:25, 26; Ufunuo 1:5; 3:14) Basi, ilifaa kwamba kwenye wakati unaofaa wa Mungu, watu wake wastahili hatimaye kuwa na jina hili lililowekwa rasmi kwa njia ya kimungu—“Mashahidi wa Yehova.”—Yohana 17:6, 11, 12.
Jumuiya ya Wakristo Yavuliwa Kibandiko cha Usoni
14. Jumuiya ya Wakristo imefichuliwa jinsi gani muda wa miaka 70 iliyopita?
14 Katika muda wa miongo saba iliyopita, Mashahidi wa Yehova wameeneza mfuriko halisi wa malawama ya wazi na hukumu kuzunguka ulimwengu, huku wakitangaza pia lile tumaini tukufu la Ufalme wa Yehova unaokuja. Katika mamia ya mamilioni ya vichapo vya Biblia vinavyotoboa mambo wazi, vyenye kugonga sana, wao wamefichua Jumuiya ya Wakristo kuwa ndiyo kani yenye nguvu nyingi zaidi katika yule kahaba wa kidini, “Babuloni Mkuu,” ambaye analaumiwa wazi katika Ufunuo sura 17 na 18. (Ona “Babylon the Great Has Fallen!” God’s Kingdom Rules!, kurasa 576-615, kilichotangazwa katika 1963 na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.)
15. Ni jinsi gani Jumuiya ya Wakristo ilifichuliwa katika 1955?
15 Katika 1955 Mashahidi wa Yehova wa. ligawanya mamilioni ya nakala za kijitabu Christendom or Christianity—Which One is“the Light of the World”? Maelfu yacho yalipelekwa moja kwa moja kwa viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo. Nacho kijitabu hicho kiliwaambia nini? Kwa mtindo halisi wa Yeremia, kilitaarifu hivi: “Ijapokuwa Jumuiya ya Wakristo imepata faida zote zile ambazo zimeisukuma mbele kiuchumi, kiakili na kijeshi, hiyo haikujithibitisha kuwa ‘nuru ya ulimwengu.’ Kwa sababu gani sivyo? . . . Hiyo haihubiri wala kuzoea Ukristo [wa Biblia].’ Ndipo ilipotokeza swali hili: “Je! kufichua dini za bandia ni kunyanyasa wafuasi wazo? Je! ni kushikilia kauli moja tu kwa njia isiyo ya Kikristo?”
16. Je! Mashahidi walikuwa wanashikilia mno kauli moja tu kwa kufichua Jumuiya ya Wakristo? Eleza.
16 Jibu lilikuwa: “Hapana; ama sivyo Yesu Kristo alikuwa mnyanyasaji wa Wayahudi mwenye kushikilia kauli moja tu, . . . na manabii wote wa Yehova wa nyakati za kale [kutia na Yeremia] ambao walitangulia Yesu walikuwa wanyanyasaji na wenye kushikilia kauli moja tu, kwa maana wote walifichua dini bandia ya Wayahudi waasi-imani na ya mataifa yasiyoerevuka katika ibada.” Kwa uhakika, ikiwa Wakristo wa kweli watakuwa “nuru ya ulimwengu,” ni lazima “giza” la kiroho lifichuliwe. (2 Wakorintho 6:14-17) Hiyo haimaanishi kwamba watu mmoja mmoja wanashambuliwa, bali unaoshambuliwa ni ule mfumo unaotumikisha watu hao. Hivyo, Yehova alimpa Yeremia amri hii: “Wewe unapaswa kufunga viuno vyako, na lazima wewe uinuke na kunena kwa hao kila jambo ambalo mimi mwenyewe nakuamuru wewe. Usipatwe na ofogyo lo lote kwa sababu ya hao . . . Na hakika wao watapigana dhidi ya wewe, lakini wao hawatashinda dhidi ya wewe, kwa maana ‘mimi nipo pamoja na wewe,’ ndilo tamko la Yehova, ‘ili kukukomboa wewe.’”—Yeremia 1:17, 19, NW.
Kazi ya Yeremia Inakuja Kwenye Ukamilisho
17, 18. (a) Ni jinsi gani Mashahidi wa Yehova wameendeleza kazi yao ya Kiyeremia katika miaka ya majuzi? (b) Ni shauri gani ambalo limetolewa kwa wenye mioyo ya ufuataji haki
17 Je! Mashahidi wa Yehova wamepunguza sauti katika kutangaza hukumu ya Mungu? Ni kweli, sisi tunaishi katika muda ambao haifikiriwi kuwa inafaa kuchambua dini nyingine. Hata hivyo, vichapo vya Mashahidi wa Yehova vinaeleza wazi ujumbe ule ule wa hukumu kwa Jumuiya ya Wakristo kama sikuzote. Mathalani, katika miaka minne iliyopita, Mashahidi wa Yehova wamechapa nakala milioni 32 za kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, katika lugha 76. Kichapo hiki kinatokeza majibu kwa maswali mengi ya wakati huu, kama vile “Inakuwaje Wakati wa Kufa?” “Sababu Gani Mungu Ameruhusu Uovu Uwepo?” na “Kuitambua Dini ya Kweli.” Lakini kinatoa pia onyo la waziwazi kuhusu ile milki ya ulimwengu ya dini bandia.
18 Katika sura ya 25, yenye kichwa “Upande wa Ulimwengu wa Shetani, au Upande wa Mfumo Mpya wa Mungu?” kinataarifu hivi: “Katika Biblia dini [bandia] inafananishwa na ‘kahaba mkuu,’ au malaya, mwenye jina ‘BABELI MKUU.’ . . . Na ni kweli kwamba katika historia yote dini imejichanganya na siasa, mara nyingi ikiziambia serikali jambo la kufanya.” Basi, ni mwendo gani wa tendo ambao kitabu hicho kinapendekeza? Hicho kinauliza hivi: “Je! unataka kuwa sehemu ya ulimwengu wa Shetani? Au unataka kuwa upande wa mfumo (taratibu) mpya wa Mungu? Ikiwa uko upande wa mfumo mpya wa Mungu utajitenga na ulimwengu, kutia na dini yake ya [bandia]. Utatii amri hii: ‘Tokeni kwake [Babeli Mkuu], enyi watu wangu.’ (Ufunuo 18:4)”
19. Wewe unaweza kuonyesha jinsi gani kwamba ile sauti ya Yeremia wa ki-siku-hizi haijatiwa ububu wakati wa tarehe hii iliyosonga sana?
19 Ujumbe huu huu mkali wa mtenganisho na hukumu unavuma kwa kusikika wazi katika kitabu Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani,” kilichochapishwa katika 1986 (nakala milioni sita katika lugha 25). Hicho kinafichua viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo juu ya ‘kuwachochea vijana kwa mahubiri yao waende kwenye nyanja za mapigano’ za Vita ya Ulimwengu ya Kwanza. Hicho kinaendelea kusema: “Jumuiya ya Wakristo inaendelea kuwa adui wa Mungu Aliye Juu Zaidi mpaka wakati uu huu. Bila shaka yeye hana [himaya ya] kimungu, na kwa sababu hii yenye maana kuwako kwake kunaendelea kuwa katika hali isiyo na usalama.” (Ona kurasa 30-2.) Sauti ya Yeremia wa kisasa haijatiwa ububu! Ingawa jitihada zinafanywa na viongozi wa kidini na wanasiasa kufifisha kuhubiriwa kwa hukumu za Mungu, mashahidi wake waaminifu wanasonga mbele, wakiwa wamepiga moyo konde kukamilisha ile kazi ya kutoa onyo.—Yeremia 18:18.
20. Kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova wataendelea kutangaza hukumu za Yehova kwa mataifa?
20 Na ni kwa sababu gani lazima kazi hii ikamilishwe? Kwa sababu Yehova, Bwana Mwenye Enzi Kuu aliye hai wa ulimwengu wote mzima, ana mhesabiano pamoja na mataifa na dini zao. Sawasawa na vile Yehova alivyouliza Yuda na Yerusalemu wenye udanganyifu, ndivyo swali hilo linavyohusika kwa Jumuiya ya Wakristo leo: “Je! mimi sipaswi kufanya mhesabiano kwa sababu ya mambo haya haya?” ndilo tamko la Yehova. ‘Au nafsi yangu haipaswi kujilipizia kisasi yenyewe juu ya taifa lililo kama hili?? “Basi, Mashahidi wa Yehova wataendelea kuzuru jamii za mataifa wakiwa na ujumbe unaouma watu walio wengi, huku ukionwa kuwa ujumbe usiopendwa na wengi lakini ukiwa ni habari njema za kufurahisha walio wachache —zile habari njema za Ufalme wa Mungu, —Yeremia 5:9, 29; 9:9; Matendo 8:4, 12, NW.
21. Kujapokuwa na afa lililotabiriwa, ni tumaini gani kubwa lililoko mbele ya wale wanaotii kazi ya Yeremia? (Zaburi 37:9, 11, 18, 19, 28, 29)
21 Ingawa mara nyingi Yeremia ameitwa mpiga mayowe ya maafa, ni kweli pia kwamba ujumbe wake ulianzishia Wayahudi miali ya tumaini. (Yeremia 23:5, 6; 31:16, 17) Kwa njia inayofanana na hiyo, ingawa Mashahidi wa Yehova wanatangaza “dhiki kubwa” inayokaribia sana, pamoja na hukumu ya Mungu ya Har–Magedoni, wao wanatangaza pia baraka za “mbingu mpya na dunia mpya” ambazo zitatokeza kurudishwa kwa haki na Paradiso kwenye sayari hii, pamoja na uhai wa milele. (Mathayo 24:21, 22; Ufunuo 16:16; 21:1-4) Basi, sasa ndio wakati wa kutii ujumbe wa Yehova wa hukumu na kutegemeza kukamilishwa kwa ile kazi kubwa ya Yeremia.—Linganisha Yeremia 38:7-13.
Je! Wewe Unakumbuka?
◻ Kama Yeremia, ni jinsi gani Mashahidi wa Yehova wananyanyaswa?
◻ Kwa sababu gani Mashahidi wanazidi tu kuhubiri?
◻ Ni jinsi gani kazi ya Yeremia imepanuliwa?
◻ Ni vielelezo gani vya hivi majuzi ambavyo vinaonyesha kwamba kule kulaumu waziwazi hakujabadilika?
◻ Ujapokuwako ule ujumbe wa afa, ni tumaini gani linalotokezwa pia?
[Picha katika ukurasa wa 23]
Baada ya muda Mariamu... alifanywa kuwa sanamu ya kuabudiwa na watu wakaja kumstahi sana kuwa “Mama ya Mungu”
[Picha katika ukurasa wa 24]
Katika 1931 Wanafunzi wa Biblia walikubali jina “Mashahidi wa Yehova” katika mkusanyiko wao mmoja katika Columbus, Ohio
[Picha katika ukurasa wa 25]
Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wanafuata kielelezo cha Yeremia