Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/95 kur. 3-6
  • Urahisishaji wa Mkusanyiko wa Wilaya wa 1995

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Urahisishaji wa Mkusanyiko wa Wilaya wa 1995
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • “Imani Katika Neno la Mungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1997
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • “Wasifaji Wenye Shangwe” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1995
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Mikusanyiko ya Wilaya ya 1999 ya “Neno la Mungu la Kiunabii”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wa 1988
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 5/95 kur. 3-6

Urahisishaji wa Mkusanyiko wa Wilaya wa 1995

1 Inasisimua kama nini kuwepo kwenye karamu za kiroho, iwe ni kwenye mikutano ya kutaniko, makusanyiko ya mzunguko, siku za kusanyiko la pekee, au mikusanyiko ya wilaya! Kushirikiana na watu wenye kuhofu Mungu kwaburudisha, na mambo ya kiroho yanayotolewa kwenye pindi hizi hutukumbusha mambo ya maana zaidi.

2 Maelfu yenye kuongezeka yamevutwa katika vikusanyiko hivyo vya kiroho katika miaka ya majuzi. Kati ya miaka ya 1985 na 1994, idadi ya makutaniko ulimwenguni pote imeongezeka kwa zaidi ya asilimia 50, kutoka 49,716 hadi 75,573. Kadiri Yehova aongezavyo mwendo wa kazi ya kukusanya, ndivyo idadi ya mikusanyiko ya wilaya na makusanyiko ya mzunguko inavyoongezeka vivyo hivyo. (Isa. 60:22) Ongezeko katika idadi ya mikusanyiko, ni wonyesho wa ukuzi huu mkubwa ajabu katika idadi ya makutaniko. Kazi itokanayo na kupanga na kushughulikia mikusanyiko hii imekuwa ikiongezeka kwa kiwango kikubwa zaidi. Kwa kuwa sisi hukusanyika ili kunufaika na programu ya kiroho iliyotayarishwa kwa karamu hizi, laonekana kuwa jambo la hekima tu kuhusisha machache iwezekanavyo katika kuhangaikia mipango ya kimwili.

3 Matokeo ya baraka za Yehova yatokeza takwa ambalo lazima likabiliwe, na tuna furaha kuona kwamba amewapa watu wake roho ihitajiwayo ya hekima na uelewevu. Lazima tukubali kwamba kupitia jamii ya mtumwa mwaminifu mwenye akili, Yesu Kristo ameelekeza mambo kwa kufaa kwa ajili ya kutimizwa kwa kusudi la Yehova katika njia ya ajabu. (Mt. 24:45-47; Kol. 1:9, 10) Kuhusu mikusanyiko, makusanyiko ya mzunguko na siku za kusanyiko la pekee tafadhali angalieni yafuatayo: “Kuanzia mikusanyiko ya wilaya ya 1995 na makusanyiko ya mzunguko ya Septemba 1995 na siku za kusanyiko la pekee, hakuna chakula kitakachoandaliwa. Kila mtu apaswa kuleta chakula na kinywaji chake mwenyewe.” Makusanyiko ya mzunguko na siku za kusanyiko la pekee yataendelea na mipango yao ya chakula iliyorahisishwa ya wakati huu hadi Agosti 1995. Huenda ukapendezwa kujua jinsi badiliko hili litakuwa lenye manufaa. Labda pitio lifuatalo la marekebisho lililofanywa miaka ya majuzi litathibitika kuwa kikumbusha kizuri cha manufaa tulizopokea tayari kwa kurahisisha kazi kwenye mikusanyiko.

4 Kabla ya utekelezaji wa mipango iliyosawazishwa na iliyorahisishwa ya mkusanyiko wa wilaya, kama vile utumishi wa chakula, utumishi wa kujitolea, na mahali pa kulala, kazi nyingi zaidi ilihitajiwa kwa upande wa mamia ya ndugu na dada katika kazi ya kabla ya mkusanyiko. Kwa kufikiria misongo na madai yanayofanyiwa ndugu zetu na maisha ya kila siku na kuendelea kwa ukuzi wa tengenezo, marekebisho ya kurahisisha kazi yalihitajiwa. Kwa kuongezea, kama tokeo la kurahisisha mipango yetu ya chakula mamia ya ndugu na dada waliokuwa wakifanya kazi kwa bidii wakati wa makusanyiko ili kutuandalia chakula waliweza kusikiliza programu. Katika 1987 mipango zaidi ya urahisishaji ilitekelezwa kuhusu chakula katika mikusanyiko na wakati wa mwaka wa utumishi uliofuata kwenye makusanyiko ya mzunguko na siku za kusanyiko la pekee. Haya yalikuwa marekebisho mazuri kama nini, yakifanya kazi iwe nyepesi na kuruhusu uangalifu zaidi kutolewa kwa mambo ya kiroho ya mkusanyiko, huku wafanyakazi wakiweza kusikiliza na kufurahia mengi zaidi ya programu. (Kum. 31:12) Wale waaminifu miongoni mwetu wenye miaka mingi ya utumishi mshikamanifu wanakumbuka maendeleo haya vizuri na wameonyesha uthamini kwa mwelekezo uliopokewa. Lakini ni kazi gani zaidi ingeweza kuondolewa hata kutokana na mipango hii iliyorahisishwa?

5 Wakati wa miaka ambayo orodha ya vyakula iliyorahisishwa ilipotayarishwa na kutumiwa, ilionekana kwamba kwa kadiri fulani “mambo machache” yalikuwa kwa kweli “yahitajiwa.” (Linganisha Luka 10:38-42, NW.) Hata hivyo, kujumlisha mambo hayo machache na idadi ya wahudhuriaji hutokeza ugavi mwingi na kazi nyingi zaidi, pamoja na vifaa vilivyoongezwa vyenye bei ghali. Kisha, pia, idadi kubwa ya wajitoleaji walihitajiwa ili kupanga na kutegemeza mipango hiyo. Ununuzi na uhifadhi kwa chakula ulikuwa lazima uandaliwe. Katika nchi nyingine matrela ya Sosaiti yenye mashine ya barafu yamebidi kupakiwa upakizi wa chakula, ukisafirishwa kilometa nyingi, na kupakuliwa. Yote hayo yamehusisha madaraka yahangaishayo mno Sosaiti. Matrela hayo pia yamehitaji udumishaji, uhifadhi, na utaratibu unaohusisha kazi, wakati, na gharama. Kukiwa na urahisishaji wa sasa, hakutakuwa na uhitaji wa kuwa na majiko, mitungi ya gesi, sahani, n.k., au mahangaiko juu ya jinsi ya kusafirisha vifaa hivyo kwenye na kutoka mahali pa mkusanyiko. Isitoshe, ndugu wengi watapunguziwa ile kazi kubwa ya kudumisha vifaa hivi.

6 Utumishi wa hiari wa wale waliotumikia wakiwa wajitoleaji katika maeneo yanayohusiana na haya umekuwa wa thamani isiyoweza kukadiriwa na wathaminiwa sana sana. Hata hivyo, kukiwa na urahisishaji huu wa ziada, wale maelfu wanaotumikia nje wakifanya utegemezo na kuendesha malori makubwa na vilevile kununua, kufanya matumizi ya fedha, kutayarisha na kuandaa chakula wataweza kutumia wakati wao katika ufuatiaji mwingineo wa Ufalme ulio wa lazima, kutia ndani kufurahia ushirika katika mikusanyiko kikamili zaidi. Wajitoleaji waliokuwa wakitumika katika Utumishi wa Chakula wataweza sasa kusaidia katika idara nyingine, kama vile Ukaribishaji na Usafi. Kufanya hivi kutarahisisha mzigo kwa kila mtu na hakutahitaji kwamba wengi zaidi wafanye kazi usiku zaidi, kama ilivyokuwa na idadi fulani katika Utumishi wa Chakula.

7 Sosaiti yathamini sana sana tegemezo zuri ambalo nyinyi ndugu na dada mmetoa kwa “ukamilifu wa moyo” kwa miaka iliyopita kwa mipango ya mkusanyiko, kutia ndani utumishi wa chakula. (1 Nya. 29:9) Kufanya hivi kumesaidia katika njia nyingi. Kumefanya iwezekane kukodisha majengo mazuri na kutunza gharama za mkusanyiko. Pia kumewezesha wale wanaohudhuria wabaki mahali pa mkusanyiko wakati wa kipindi kifupi cha pumziko la mchana ili wapate chakula kwa kufaa, waburudishwe, na kisha wawepo kwa ajili ya programu ya kiroho. Hata hivyo, urahisishaji huu wa ziada wamaanisha kwamba gharama zote za kukodisha vifaa vya mkusanyiko na kujengwa kwa jukwaa, n.k., sasa lazima zishughulikiwe na michango yenu. Tuna hakika kwamba ukarimu wenu na tegemezo la maandalizi haya utakuwa mwingi zaidi ili kushughulikia gharama za uendeshaji wa mkusanyiko. Twathamini wonyesho huu wa uthamini wenu katika njia yenye kutumika.—Kut. 36:6, 7; Mit. 11:25; Luka 16:9.

8 Hata hivyo, kukiwa na marekebisho haya ya ziada, itafaa kwa watu mmoja-mmoja na vikundi vya familia kujiandalia wenyewe kile kinachohitajiwa tu kwa namna ya maakuli ya kimwili wakati wa pumziko la mchana. Twastahi zaidi manufaa nzuri za programu ya kiroho. Kuacha chakula cha kimwili kichukue umaana wa kupita kiasi hakungekuwa jambo la hekima. Ni muhimu kwamba kila mtu ‘apate kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi’ kwa upande huu. (Flp. 1:9, 10a, NW) Mikusanyiko mikubwa ya watu wa Yehova ya majuzi katika Poland, Urusi, na Ukrania, pamoja na sehemu nyingine za Ulaya Magharibi, imefanywa kwa mafanikio bila mipango ya utumishi wa chakula. Kwa kuongezea, mizunguko fulani, imefanya makusanyiko yao na programu za siku za kusanyiko la pekee bila utumishi wa chakula kwa sababu ya hali za kwao. Katika kila kisa wajumbe walileta chakula chao wenyewe cha mchana. Tutaona kwamba tukileta kiburudisho chepesi, kitachangia hali ya akili iliyo chonjo, ikituwezesha kupata manufaa kamili kutoka programu ya alasiri. Kwa kupatana na hili, kila mtu apaswa kuleta kwenye mkusanyiko chakula sahili na chenye kujenga. Kwa kielelezo, Yesu alipokuwa akilisha umati, aliandaa vitu viwili tu, mkate na samaki. (Mt. 14:16-20; ona pia Luka 10:42a.) Kwa hiyo, twapenda kuwatolea madokezo fulani ya kile kinachoweza kufaa na chenye kutumika kwa ajili ya pumziko fupi la mchana na aina ya vifaa tunavyotumia.

9 Kwa kuwa hakutakuwa na mipango ya chakula tena kwenye mkusanyiko, wakiwa na mpango mzuri wale wanaohudhuria wataweza kufurahia kiamsha-kinywa pamoja na familia zao ama nyumbani kwao ama mahali pa kwenu pa kulia. Kwa kupata usingizi wa kutosha usiku unaotangulia, inapaswa iwezekane kuamka mapema ili kupata yaliyo ya lazima kwa ajili ya ulishaji wa asubuhi na kufika kwenye mkusanyiko kwa wakati wa kutosha ili kufurahia ushirika pamoja na wajumbe wengine. Manufaa nyingine ya mipango hiyo mipya ni kwamba milango ya majengo hayo haitahitaji kuwekwa watu na kufunguliwa mapema kama wakati wajitoleaji wa utumishi wa chakula walipokuwa wakiruhusiwa na familia zao. Milango ya majengo hayo itafunguliwa saa 2:00 asubuhi kwa wajumbe wote, isipokuwa wachache walio na migao ya kazi hususa ambayo yawalazimu kuingia mapema. Kama ilivyokuwa wakati uliopita, hakutakuwa na haja ya kukimbia mahali pa mkusanyiko kutafuta viti, kwa kuwa kumekuwa na viti vya kutosha vilivyopangwa kwa umati unaokadiriwa.

10 Pumziko la mchana litakuwa fupi kuliko la mikusanyiko iliyopita. Hata hivyo, bado litaandaa fursa ya kutwaa lishe nyepesi kama burudisho kwa kujitayarisha kwa ajili ya programu ya alasiri, pamoja na wakati wa kushirikiana na wengine. Ndugu na dada zetu wanaoishi katika jiji la mkusanyiko au karibu-karibu na ambao kila siku hurudi nyumbani jioni wataweza kutayarisha chakula kidogo kwa kila mshiriki wa familia ili kubeba kwa ajili ya pumziko la mchana la kila siku. Hiki chaweza kuwa kipande cha mkate na kipande cha tunda, maandazi, na kinywaji. Watu wengi huwa na vyakula vya mchana kama hivyo mahali pao pa kazi.

11 Hili bila shaka litatokeza tatizo kwa wale wanaohudhuria mkusanyiko kutoka nje ya jiji la mkusanyiko, na mipango ya mapema ya vifaa vya chakula cha mchana itakuwa ya lazima. Labda vyombo vya lazima vingeweza kuletwa kutoka nyumbani. Wengine huenda wakaona kwamba chakula chepesi cha matunda, mboga, au sambusa kitatosha kutosheleza mahitaji yao, nacho chaweza kuletwa kutoka nyumbani pia. Mahitaji mengine ya chakula cha kila siku mchana yaweza kupatikana dukani au sokoni katika jiji la mkusanyiko. Bila shaka, twatambua kuwa hifadhi ya barafu na utayarishaji wa orodha ndefu ya vyakula hautawezekana kwa wale wanaokaa katika hoteli, nyumba za faragha au mahali pa mkusanyiko.

12 Kikiwa kikumbusha, tafadhali USIPIKE KATIKA MAHALI PAKO PA KULALA isipokuwa kama kuna mahali pa jikoni kwa kusudi hilo. Ni hatari na si halali kufanya hivyo na kwaweza kuharibu vitu vya nyumba kwa madoa na mafuta. Mabaraza ya mkusanyiko yataandaa habari kuhusu ni nini kinapatikana kwa wale waliopatiwa mahali pa kulala mahali pa mkusanyiko. Kwa hiyo, huenda likawa jambo la hekima kununua vitu visivyoharibika, kama vile njugu, matunda, na bisi, au huenda ukachagua kuleta vitu vilivyookwa, kama vile mkate, vitumbua, au keki ndogo. Ikiwa kitu cha kula wakati wa mchana chahitajiwa, kama vile kipande cha mkate, labda unaweza kununua aina hiyo ya kitu kilichotayarishwa tayari na hivyo kuondoa utayarishaji wa chakula katika mahali pako pa kulala.

13 Kwa kuwa mahali pa mkusanyiko kwa kweli panakuwa Jumba la Ufalme kubwa wakati wa mkusanyiko, pia ni jambo la hekima kuepuka kusitawisha mazingira ya mandari wakati wa pumziko la mchana. Na kama vile hatuli wakati wa mikutano kwenye Jumba la Ufalme, pia hatutakuwa tukila au kunywa wakati wa vipindi vya mkusanyiko. Tafadhali usilete vyombo vikubwa kupita kiasi, kwa kuwa vyaweza kutokeza hatari na kuchukua nafasi kubwa kati ya viti; vyapasa kuwekwa chini ya viti. Labda vyondo au mifuko ya karatasi iwezayo kutupwa itafaa kuwa vyombo vya vyakula vyepesi ambavyo vitahitajika kwa ajili ya pumziko letu la mchana. Chochote kitakachotumiwa chapaswa kuwa kidogo ili kutosha kuwekwa chini ya kiti chako.

14 Tahadhari yapasa kuwepo kuhusu aina ya vyombo vya kuwekwa vinywaji tunavyochagua kuleta mahali pa mkusanyiko. Vinywaji moto vinaweza kuletwa ndani ya flaski. Chupa za glasi za aina yoyote zaweza kuthibitika kuwa hatari kwa hiyo, tafadhali uwe mwangalifu katika kushughulika na chupa zozote za vinywaji unazochagua kutumia.

15 Kwa kweli twaweza kuona hekima ya mipango kama hiyo iliyorekebishwa. Wote wataweza kutoa uangalifu kamili katika kupokea manufaa za kiroho—kusudi halisi la kukusanyika kwetu. Manufaa hizi zaandaliwa katika ushirikiano tunaofurahia pamoja na programu yenyewe. Kwa hiyo badala ya kuacha mahali pa mkusanyiko wakati wa pumziko la mchana ili kutafuta chakula, itanufaisha kuja na kitu. Kufanya hivi kutafanya iwezekane kufurahia ushirika wa ndugu na dada zetu na kutuzuia kukosa programu yoyote ya alasiri.

16 Tukiwa tumeburudishwa kiroho kufuatia programu ya alasiri, wengine huenda wakafurahia ushirika wa Kikristo wenye kuendelea na mazungumzo juu ya mambo mazuri tuliyojifunza tunapokula mlo wenye nguvu tukiwa na familia na marafiki katika mahali petu pa kulia. Wengine huenda wachukue kitu kwenye duka la matunda na mboga au sokoni. Wale wanaochagua kurudi nyumbani mwao huenda wakachagua kuwa na mlo wa jioni huko, kama vile wafanyavyo siku nyingine watumiazo wakiwa kazini au kwenye utumishi wa shambani.

17 Kwa kweli twafurahia karamu ya kiroho kwenye makusanyiko na mikusanyiko hii ambapo sisi hupokea vichapo vipya, mafundisho mema, na shauri lenye kutumika. Baraka hizi ndizo kila mtu hukumbuka, pamoja na shangwe ya kuwa watu wa Mungu waliokusanyika. Mithali 10:22 husema: “Baraka ya BWANA hutajirisha, wala hachanganyi huzuni nayo.” Hii ni kwa sababu tukiwa watu wa Yehova, hatuhudhurii mikusanyiko tukitaka vitu vya kimwili na tukifikiria starehe. Twakusanyika tukiwa na tamaa chanya ili kupata manufaa kubwa zaidi katika njia ya kiroho, na Yehova hututajirisha kwa roho tuonyeshayo.—1 Tim. 6:6-8; Ebr. 11:6.

18 Pindi hizi za kitia-moyo pia zatukumbusha maendeleo ya mavuno ya kiroho. (Yn. 4:35, 36) Maneno ya utangulizi ya Isaya sura 54 hutolea wito tengenezo la Yehova lililo kama mke kujitayarisha kwa ajili ya maongezeko yenye shangwe. Ongezeko zaidi, upanuzi, na nguvu iliyofanywa upya viko kwenye ukaribio kwa kuwa Isaya alitabiri: “Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako. Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto.” Kutimizwa kwa unabii huu wenye kusisimua kumetokeza mpanuko wa ajabu wa ibada ya kweli tunaoona sasa.—Isa. 54:1-4.

19 Kwa kweli yaonekana kuwa mwendo wenye uamuzi mzuri kutekeleza urahisishaji huu wa ziada wa mipango ya mkusanyiko ili kwamba kukiwa na vikengeushaji vichache wote wataweza kufurahia programu ya kiroho ambayo imetayarishwa. Twatumaini kwamba huu pia utakuwa na baraka za Yehova, kwa kuwa utaruhusu kushughulika kwenye matokeo kwa ukuzi zaidi. Kwa kukazia yanayohitajiwa tutaweza kufurahia siku zetu zilizopangwa za ushirika wenye furaha na mambo mazuri ya kiroho. Ni sala yetu ya unyoofu kwamba Yehova atabariki jitihada zetu zote tuendeleapo kukusanyika na kulishwa kwenye meza ya Yehova.—Linganisha Kumbukumbu la Torati 16:14, 15.

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

Manufaa za Kutokuwa na Mipango ya Utumishi wa Chakula

◼ Kazi chache kabla, wakati wa, na baada ya programu, ikiruhusu ushirika zaidi

◼ Hakuna vifaa vya utumishi wa chakula vya kutunzwa

◼ Watu wengi zaidi waweza kutoa uangalifu kamili kwa programu ya kiroho

◼ Wajitoleaji wengi zaidi wapatikanao ili kusaidia idara nyingine

◼ Wakati mwingi zaidi wapatikana kwa ajili ya ufuatiaji mwingine wa kitheokrasi

Vifaa Vinavyodokezwa vya Kuleta Kwa Ajili Ya Pumziko la Mchana

◼ Vitu vyepesi, sahili, na vyenye lishe bora vya chakula cha mchana

◼ Njugu, maandazi, matunda, mahindi-choma, sambusa

◼ Vinywaji moto katika flaski

◼ Soda, maji ya matunda, au maji ya chupa

USILETE Mahali pa Mkusanyiko

◼Alkoholi (Vileo)

◼Vyombo vya kuwekea chakula vikubwa mno

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki