Wimbo 72
Zile Furaha na Matunda ya Utumishi wa Ufalme
1. Utumishi wa Yehova, Mungu,
Una furaha nyingi sana,
Pasipo choyo tunahubiri
Ili kufariji wengine.
Yesu alituhakikishia:
Tunavuna furaha nyingi.
Tungetoa kitu bora gani
Kuliko ukweli wenye uzima.
2. Tunapohubiri milangoni
Tunadhihakiwa na watu,
Tunabaki imara kabisa
Na kushika ukamilifu.
Hata tukipatwa na mateso
Tukisema jina Yehova
Yesu alisema ni furaha,
Hali moja na manabii kale.
3. Utumishi ni wenye furaha
Kwa kufuata Bwana wetu;
Hubiri kisasi cha Yehova
Utukuze Yehova Mungu!
Tunawapa watu tumaini
La Paradiso bora sana.
Tunafurahia jambo hilo,
Uzima wa milele na milele.