Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/96 uku. 4
  • Wasaidie Waelewe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasaidie Waelewe
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kupiga Mbiu ya ‘Maneno ya Unabii’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Saidia Wengine “Kuyashika Yaliyoandikwa”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Ufunuo—Ufunguo wa Furaha ya Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 2/96 uku. 4

Wasaidie Waelewe

1 Mtume Petro alikubali kwamba mambo mengine yaliyoandikwa katika Biblia ni “vigumu kuelewa.” (2 Pet. 3:16) Wengi wamehisi hivyo kuhusu kitabu cha Ufunuo. Hata hivyo, maana yacho imefanywa ieleweke wazi kabisa katika kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Twaweza kusaidiaje wenye kupendezwa wakitumie vizuri?

2 Ikiwa mlizungumza kuhusu Ufunuo 1:3 kwenye ziara yako ya kwanza, wazo hili laweza kuchochea kupendezwa kupya:

◼ “Wakati uliopita tulizungumza jinsi uelewevu wa kitabu cha Ufunuo uwezavyo kuleta furaha. Hata hivyo, furaha hiyo haiji yenyewe. Angalau mambo mawili yanatakwa upande wetu: Lazima tujifunze Biblia, na lazima tufanye yale tunayojifunza.” Soma na utoe maelezo juu ya Yakobo 1:25. Fungua kwenye ukurasa wa 8 fungu la 9, na ukazie jinsi uelewevu wa kitabu cha Ufunuo uwezavyo kutusaidia tujifunze jinsi tunavyoweza kupata furaha katika ulimwengu mpya wa paradiso.

3 Ikiwa mlizungumza kuhusu Yohana 17:3 kwenye ziara yako ya kwanza, unaweza kukazia uhitaji wa kutwaa ujuzi zaidi wa Biblia kwa kusema:

◼ “Wakati uliopita nilipokuwa hapa, tulisoma Yohana 17:3 kwamba kutwaa ujuzi kuhusu Mungu kwaweza kuongoza kwenye uhai udumuo milele. Lakini ungependa kuishi milele katika dunia tunayoishi leo? [Ruhusu itikio.] Walio wengi hawangependa. Kwa sababu hii, twaweza kushangilia tunaposikia yale ambayo Mungu ameahidi.” Fungua kwenye fungu la 6 ukurasa wa 303, soma Ufunuo 21:4, kisha ufafanue vile ulimwengu utakavyokuwa wakati “mambo ya kwanza yamekwisha kupita.” Panga kurudi tena kwa mazungumzo zaidi.

4 Ikiwa ulitumia picha iliyo kwenye ukurasa wa 302 kuonyesha kwamba Ufalme wa Mungu utakomesha taabu, unaweza kufungua kitabu kwenye ukurasa huo tena na kusema:

◼ “Tulizungumzia baraka zinazoonyeshwa hapa ambazo watu watafurahia chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu. Unafikiri lazima tufanye nini ikiwa twataka kuishi chini ya Ufalme huo? [Ruhusu itikio.] Watu fulani katika nyakati za Biblia waliweka kielelezo bora zaidi ambacho kitatunufaisha kuiga.” Soma Matendo 17:11, ukikazia uhitaji wa ‘kuyachunguza Maandiko kila siku.’ Eleza kwamba Mashahidi wa Yehova wanasaidia watu wanyoofu katika jumuiya kujifunza Neno la Mungu na kulielewa vizuri.

5 Ukipata wenye kupendezwa, hatimaye utapenda kuelekeza uangalifu kwenye kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele na kukitumia kuanzisha funzo. Kwa hakika utapata shangwe nyingi katika kusaidia ‘wasio na uzoefu kuelewa.’—Zab. 119:130, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki