Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/96 uku. 1
  • Uwe Kielelezo Katika Usemi na Katika Mwenendo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Kielelezo Katika Usemi na Katika Mwenendo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • “Jiendesheni kwa Namna Inayozistahili Habari Njema”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kuwa na Adabu Nzuri Ni Sifa ya Watu wa Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Kuonyesha Adabu Tukiwa Wahudumu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kusitawisha Adabu za Kikristo Katika Ulimwengu Usio na Adabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 9/96 uku. 1

Uwe Kielelezo Katika Usemi na Katika Mwenendo

1 Mtume Paulo alimsihi sana Timotheo kuwa kielelezo katika usemi na katika mwenendo. (1 Tim. 4:12) Sisi pia twapaswa kuonyesha mfano mzuri wa usemi na mwenendo, hasa tunaposhiriki katika huduma, kwa kuwa kufanya hivyo kwaweza kuamua kama twaufikia ama hatuufikii moyo wa wale tunaokutana nao.

2 Twahitaji kuonyesha pande zote za adabu nzuri, kutia ndani jamala, ufikirio, fadhili, uungwana, na busara. Kwa kuonyesha sifa hizi, twaonyesha kwamba tunajua jinsi matendo yetu yanavyoathiri hisia za wengine. Adabu nzuri katika huduma zaweza kulinganishwa na vikolezo, vinavyotumiwa kuongeza ladha ya chakula. Bila hivyo, chakula kinachofaa chaweza kuwa bila utamu na kisicholeta hamu. Kushindwa kuonyesha adabu nzuri katika shughuli zetu pamoja na wengine kwaweza kuwa na athari hiyohiyo.—Kol. 4:6.

3 Uwe Kielelezo Katika Usemi: Tabasamu ya kirafiki na salamu changamfu ni mambo muhimu ya utoaji wetu wa habari njema. Tunapoutia ladha utangulizi wetu kwa uchangamfu na weupe wa moyo, twamfanya mwenye nyumba ajue kwamba twapendezwa naye kikweli. Anaposema, sikiliza kwa uangalifu na mwonyeshe staha istahiliyo kwa maoni yake. Unaposema, fanya hivyo kwa busara na neema.—Linganisha Matendo 6:8.

4 Pindi kwa pindi sisi hukutana na mtu ambaye huenda akawa asiye na urafiki, au hata mwenye kutaka vita. Twapaswa kuitikiaje? Petro alituhimiza tuseme kwa njia ambayo yaonyesha “tabia-pole na staha yenye kina kirefu.” (1 Pet. 3:15, NW; Rum. 12:17, 18) Yesu alisema kwamba mwenye nyumba akikataa kifidhuli ujumbe wa Ufalme, twapaswa tu ‘kukung’uta mavumbi ya miguuni mwetu.’ (Mt. 10:14) Kuonyesha kwetu adabu nzuri chini ya hali kama hizo huenda hatimaye kukalainisha moyo wa mpinzani.

5 Uwe Kielelezo Katika Mwenendo: Kuhubiri habari njema kwenye barabara zenye watu wengi na mahali pa umma hutaka tuwe wenye ufikirio, tusiwe kamwe wenye kelele au wenye kusisitiza sana, na tusizuie mpita-njia. Tunapokuwa katika nyumba za watu wenye kupendezwa, twapaswa kudumisha adabu ifaayo na kujiendesha wenyewe tukiwa wageni wenye neema, tukionyesha uthamini kwa ukaribishaji-wageni wao. Watoto wowote wanaoandamana nasi lazima waonyeshe staha kwa mwenye nyumba na mali yake na wapaswa kuwa na adabu nzuri na wenye usikivu tunapozungumza. Watoto wakiwa watukutu, hiyo itaacha wonyesho usiofaa.—Mit. 29:15.

6 Sura yetu binafsi yapaswa kuonyesha wengine wazi kwamba sisi ni wahudumu wa Neno la Mungu. Kwa mavazi yetu na kujipamba kwetu, hatupaswi kuwa wazembe na wasio nadhifu wala wenye kutaka kujionyesha na wenye kupita kiasi. Sura yetu yapaswa sikuzote kustahili habari njema. (Linganisha Wafilipi 1:27, NW.) Kwa kukazia fikira kwa uangalifu sura yetu na vifaa vyetu, hatutawapa wengine sababu ya kukwazwa au kutafuta lawama katika huduma yetu. (2 Kor. 6:3, 4) Usemi wetu na mwenendo wetu mzuri huongezea ujumbe wa Ufalme ubora wenye kuvutia, ukimletea Yehova heshima.—1 Pet. 2:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki