Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/96 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Septemba 2
  • Juma Linaloanza Septemba 9
  • Juma Linaloanza Septemba 16
  • Juma Linaloanza Septemba 23
  • Juma Linaloanza Septemba 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 9/96 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba

Juma Linaloanza Septemba 2

Wimbo 98

Dak 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Kumbusha kutaniko kwamba twarudia funzo letu la kitabu Upeo wa Ufunuo! juma lifuatalo. Tia moyo washiriki wote wa familia wawe na nakala yao ya kibinafsi kwa ajili ya funzo. Habari za Kitheokrasi.

Dak 15: “Tembea kwa Imani.” Maswali na majibu.

Dak 18: “Kutoa Habari Njema Tukiwa na Mtazamo Chanya.” Toa maelezo ya utangulizi yakitegemea fungu la 1. Eleza kwamba toleo badala ya kitabu Creation, ni kitabu Maisha ya Jamaa kipaswacho kutumiwa kwanza. Makutaniko ambayo yana kitabu Kuishi Milele yaweza kutoa kitabu hicho. Kisha shughulikia mafungu 2-5 tu ya makala hiyo. Toa wonyesho wa utoaji mbalimbali uliotayarishwa vizuri unaoonyesha jinsi ya kutoa vitabu Creation, na Maisha ya Jamaa, kufanya ziara ya kurudia, na kuanzisha funzo katika kitabu Ujuzi.

Wimbo 48 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 9

Wimbo 18

Dak 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Zungumzia “Hubiri Ufalme.”

Dak 18: Pitia Ripoti ya Mwaka wa Utumishi wa Kutaniko ya 1996. Hotuba yenye kujenga, yenye idili itolewe na mwangalizi wa utumishi. (Ona kitabu Huduma Yetu, kurasa 100-102.) Onyesha pale kutaniko lilipofanya vema, na utoe pongezi. Onyesha jinsi utendaji wa mapainia wa kawaida na wasaidizi umefanya mengi kusaidia kuendeleza kazi kwenu. Taja tarakimu za uhudhuriaji wa mikutano, ukikazia umaana wa uhudhuriaji wa kawaida. Eleza miradi yenye kutumika ambayo kutaniko laweza kufikia mwaka ujao.

Dak 15: “Kutoa Habari Njema Tukiwa na Mtazamo Chanya.” Pitia mafungu 6-8 peke yake, na utoe wonyesho wa utoaji mbalimbali wa duka kwa duka katika ziara ya kwanza na ziara ya kurudia. (Ona madokezo ya ziada katika Huduma ya Ufalme Yetu, Septemba 1989, ukurasa wa 4.) Tia moyo wote wafanye ziara zao za kurudia upesi.

Wimbo 123 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 16

Wimbo 10

Dak 15: Matangazo ya kwenu. Tumia angalau dakika kumi katika hotuba ukishughulikia mafungu ya kwanza saba ya broshua Mapokeo chini ya kichwa “Je! Wewe Ungali Mtumwa wa Mapokeo Yasiyo ya Kikristo?”

Dak 15: “Uwe Kielelezo Katika Usemi na Katika Mwenendo.” Maswali na majibu.

Dak 15: Mwenendo wa Kikristo Shuleni. Baba aongea na mwana au binti yake ili aonyeshe matatizo mazito yaliyo katika mazingira ya shule; akazia uhitaji wa kuangalia mashirika na kuepuka utendaji wenye kutilika shaka. Yeye apitia sanduku lililo kwenye ukurasa 24 katika broshua Elimu na kueleza uhitaji wa kuweka kielelezo chema akiwa Shahidi. Baba ataja baadhi ya vishawishi vitokeavyo vya kutumia dawa za kulevya, miadi ya kijinsia, kuhudhuria vikusanyiko vya kirafiki, au kushiriki katika michezo; wanazungumza jinsi ya kuepuka matatizo. Baba amtia moyo kijana asikawie kumwendea anapokuwa na magumu—yeye ataka kuyajua na kusaidia.

Wimbo 32 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 23

Wimbo 21

Dak 12: Matangazo ya kwenu. Zungumzia Sanduku la Swali.

Dak 13: Mazungumzo pamoja na wasikilizaji ya mafungu 8 hadi 13 katika kurasa 2-3 za broshua Mapokeo ukishughulikia kichwa kidogo “Daraka la Mume,” “Daraka la Mke,” na “Haki za Ndoa.”

Dak 20: “Hubiri Habari Njema Kila Mahali.” Maswali na majibu. Shughulikia mafungu 1-15 peke yake. Soma mafungu 3 na 5. Tia ndani mambo yaliyoonwa na wale ambao wamepata mafanikio katika kutoa ushahidi barabarani au kwenye gari la kusafiria umma.

Wimbo 215 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Septemba 30

Wimbo 171

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Panga uwe na maonyesho mawili mafupi ya utoaji wa magazeti ukikazia matoleo ya karibuni. Julisha kutaniko juu ya mipango ya utumishi wa shambani kwa mwisho-juma.

Dak 20: “Hubiri Habari Njema Kila Mahali.” Maswali na majibu. Shughulikia mafungu 16-35. Onyesha jinsi madokezo hayo yanavyoweza kutumiwa kwenu. Toa wonyesho kwa mafungu 24-26. Soma mafungu 34-35.

Dak 15: Pitia Toleo la Fasihi la Oktoba. Tutatoa maandikisho ya magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Zungumzia mambo tofauti-tofauti, kama vile: (1) Kusudi la kutangazwa kwa hayo magazeti, kama ielezwavyo kwenye kurasa za mwanzo. (2) Yanatangazwa katika lugha nyingi, yakijulisha ujuzi wa Biblia ulimwenguni pote. (3) Mnara wa Mlinzi limekusudiwa kwa ajili ya funzo la kibinafsi, la familia na la kikundi. (4) Watu wanaoshiriki dini mbalimbali huyasoma. (5) Tutapeleka matoleo ya karibuni kwa yeyote anayetaka kuyasoma kwa moyo mweupe. (6) Yamekusudiwa hasa kwa ajili ya watu wenye shughuli nyingi. (7) Mnara wa Mlinzi limekuwa likitangazwa tangu 1879; Amkeni! tangu 1919. Malizia kwa kusimulia maelezo yaliyotolewa na msomaji mwenye kuthamini.—Ona Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1986, ukurasa wa 32.

Wimbo 3 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki