Wimbo 6
Zitangaze Habari Njema za Milele
1. Malaika aizunguka dunia,
Akiwa nazo habari za milele.
Asema: ‘Ogopeni, sifa mupeni
Yehova; Mungu pekee abuduni.
Imefika hukumu inayotisha,
Karibu waovu kuhisi uwezo.’
Wahubiri Ufalme wasiogope
Kote tu habari njema waziseme.
2. Ni nini wa pili anatuarifu,
Mashahidi tuyashiriki halafu?
Anguko la Babeli asimulia,
Mikononi mwa Mungu kuangamia.
Tutangaze, Yehova anaagiza,
Kwa kulaumiwa atajilipiza.
Ni kubwa sana shamba tufundishako;
Lakini malaika anaongoza.
3. ‘Mwanadamu,’ malaika wake wote,
Leo hii afanya hukumu yake.
Chukieni baya! Fanyeni mazuri.
Ogopeni Mungu mushike amuri.
Wajibu tunao, Bwana anasema,
Funza kweli, ‘hubiri habari njema.’
Kwa hiyo, sisi wahudumu, twasihi,
‘Njoo abudu Yehova, ufurahi.’