Kwa Nini Tunapaswa Kuhofu Mungu?
“HOFUNI Mungu na kumpa yeye utukufu, kwa sababu saa ya hukumu kwa yeye imewasili.” (Ufunuo 14:7, NW) Maneno hayo ya kuchochea yalisikiwa kwanza na Yohana mtume mzee katika njozi. Yakitamkwa na malaika mmoja mwenye kuruka katikati ya mbingu yalielekezwa hasa kwa watu wenye kuishi katika huu wakati wa mwisho, ambacho ndicho kipindi cha kufungua “siku ya Bwana.”—Ufunuo 1:10.
Hata hivyo huenda maneno hayo yakaonekana kuwa yasiyofaa sana kwa watu fulani! Watu wengi hata hutilia shaka kuwako kwa Mungu, achia mbali kule kumhofu. Kwa hesabu fulani ya wale wanaodai kuwa Wakristo, wazo la kuhofu Mungu linaonekana kuwa la kikale. Wao wanaweza kukubali upendo wa Mungu. Lakini kumhofu kunaonekana zaidi kuwa jambo la zile Enzi za Kati. Je! hiyo ndiyo rai yako wewe kuhusu jambo hilo?
Hofu ya Yesu kwa Mungu
Ikiwa ndivyo, fikiria maana ya kuwa Mkristo. Kulingana na Biblia, kuwa Mkristo kunahusisha ndani kufuata kwa ukaribu katika hatua za nyayo za Yesu Kristo. (1 Petro 2:21) Sasa, ingawa hakuna shaka kwamba Yesu alipenda Mungu, Biblia inaonyesha wazi sana kwamba yeye alihofu Mungu pia.Isaya, akinena kwa unabii juu ya Yesu, alisema kwamba angekuwa na “roho ya maarifa na ya hofu kwa Yehova.” (Isaya 11:2, NW) Ingawa hivyo, jambo la kupendeza ni kwamba hofu hiyo haikuwa himila nzito juu ya Yesu. Haitupasi kuifikiria kuwa kama vile mtoto anavyohofu baba mkatili au vile idadi ya watu inavyoogofywa na mtawala mwonevu. Kwa uhakika, Isaya alitoa unabii huu pia juu ya Yesu: Yeye ataona shangwe katika kuhofu Yehova.” (Isaya J.l:3, NW) Wewe unaweza kuonaje shangwe juu ya kuogopa mtu fulani?
Uhakika ni kwamba, katika Biblia neno “hofu” lina maana mbalimbali. Kuna ile hofu au mtetemo wa kimwili tunaohisi wakati mtu fulani anapotaka kutudhuru. Hivyo, majeshi ya Kiisraeli ‘waliogopa sana’ Goliathi. (1 Samweli 17:23, 24) Halafu kuna ile hofu ya mambo ya kugutusha yasiyotarajiwa au yasiyojulikana, kama ile aliyohisi Zekaria alipokabiliwa kwa ghafula na malaika wa Yehova hekaluni. (Luka 1:11, 12) Hata hivyo, hofu ambayo Yesu alihisi kwa Baba yake haikuwa kama yoyote ya hizo.
Badala ya hivyo, maneno ya awali ya Kiebrania na Kigiriki yanayotumiwa katika Biblia kuhusu “hofu” huwa mara nyingi yanarejezea kicho kingi sana na staha kubwa mno kwa Mungu. Hiyo ndiyo hofu ya kumcha Mungu aliyokuwa nayo Yesu na ambayo malaika yule alikuwa akimtia moyo kila mtu leo aisitawishe. Hiyo staha kubwa mno, au hofu, hutia mizizi katika moyo wetu wakati tunapotafakari juu ya uweza na nguvu za Yehova na kuzilinganisha na uduni wetu ulio kamili. Hiyo huwa inakua wakati sisi tunapofikiria sana kazi zake zenye uweza, na inakuzwa pia kwa kukumbuka katika sala uhakika wa kwamba yeye ndiye Hakimu Mkuu Kupita Wote, mwenye nguvu za kutolea uhai na vilevile kuadhibu kwa kifo cha milele.
Hofu ya jinsi hiyo ni muhimu kwa sababu inatuzuia tusifanye makosa na kutenda kana kwamba tunamchukua Mungu kivivi-hivi tu. Inatusaidia tuepuke mwelekeo wa jinsi hii: |‘Mungu atanisamehe. Yeye anajua kwamba mimi ni dhaifu, wakati tunapokabiliwa na kishawishi na kuonelea ni afadhali kujiachilia kitushinde kuliko kupigana nacho. Kama vile Mithali 8:13, inavyotuambia: “Hofu kwa Yehova inamaanisha kuchukia ubaya.” Na Mithali 16:6, NW, inaongeza hivi: “Katika kuhofu Yehova mmoja hugeukia mbali kutoka kwenye ubaya.” Adamu na Hawa walishindwa kujizoeza hofu hiyo inayofaa, yenye afya kwa Yehova wakati ambapo hawakumtii. Tokeo likawa nini? Walihisi hofu ya aina nyingine iliyo ya mwelekeo hasi na wakajificha kutoka kwenye kuwapo kwake. Adamu alisema: “Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa.”—Mwanzo 3:10.
Tofauti na Adamu na Hawa, Ayubu alikuwa mtu aliyebaki mwaminifu kwa Yehova ajapotahiniwa vikali sana. Kwa nini? Yehova mwenyewe alisema kwamba Ayubu alikuwa ‘mtu aliyemhofu na kwa hiyo angegeukia mbali kutoka kwenye ubaya.’ (Ayubu 1:8; 2:3, NW) Leo ni lazima sisi tuhakikishe kwamba Yehova anaweza kusema hivyo hivyo juu yetu! Hofu kwa Mungu inafaa, na ni lazima iwe sehemu ya kufikiri kwetu.
Hofu kwa Mungu na Hofu kwa Mwanadamu
Hofu kwa Mungu ni hisia ya kiasili inayotupatia usalama wa aina ile ile ambayo baba mwenye kuvuvia staha ya kina kirefu huwapa watoto wake. Hofu ya jinsi hiyo husaidia pia kuondolea mbali ile hofu isiyopendeza ya mwelekeo hasi kwa mwanadamu, ambayo ni mtego. (Mithali 29:25) Mmoja ambaye hakujifunza somo hilo alikuwa Uria, mwana wa Shemaya, aliyehubiri katika Yerusalemu pamoja na Yeremia kabla ya 607 K.W.K. Tofauti na Yeremia, Uria aliruhusu hofu kwa mfalme imtie mtegoni. Yeye aliacha kuhubiri akakimbia kutoka mgawo wake. Hatimaye, mfalme alimshika na kuagiza auawe. (Yeremia 26:20-23) Uria angaliweza kuepukaje msiba huo wenye kuhuzunisha? Kwa kukuza hofu yenye imara nyingi kwa Yehova kuliko hofu yake kwa mwanadamu.
Baada ya kufufuliwa kwake na kupaa mbinguni, Yesu aliwashauri hivi wafuasi wake: “Usiwe mwenye kuogopa vitu ambavyo wewe u karibu kupatwa navyo.” (Ufunuo 2:10, NW) Historia inaonyesha uhitaji wa shauri hilo, kwa kuwa Wakristo—kuanzia nyanja za Kiroma za kupambana na hayawani hadi kambi za mateso za Kinazi —wamekabiliana na hali za kuogofya. Wao wamewezaje kushinda hofu ambayo adui zao walijaribu kuvuvia? Kwa kutumia maneno ya Yesu: “Msihofu wale ambao wanaua mwili na baada ya hapo hawawezi kufanya jambo lolote zaidi. Bali mimi nitaonyesha nyinyi yule wa kuhofiwa: Hofuni huyo ambaye baada ya kuua ana mamlaka ya kutupa ndani ya Gehena.”—Luka 12:4, 5, NW.
Kwenye Zaburi 19:9, W, tunafundishwa hivi: “Hofu kwa Yehova ni yenye utakato, ikisimama milele. Maamuzi ya hukumu za Yehova ni ya kweli; yamethibitika kabisa kuwa ya uadilifu.” Kwa hiyo hakuna jambo lolote la mwelekeo hasi kuhusu hofu kwa Mungu. Hiyo ina utakato na himaya na hufanya mtumishi wa Mungu awe mwenye imara kuliko adui zake. Kama Yesu, Mkristo hupata uradhi katika hofu hiyo kwa njia ile ile ambayo yeye huona shangwe juu ya baraka nyingine zote kutoka kwa Yehova.—Isaya 11:3.
Kwa sababu hiyo, inafaa kabisa kabisa kwamba malaika huyo anachagiza aina ya binadamu wote leo wahofu Mungu. Bila hofu inayofaa ya kumcha Mungu, inaelekea kwamba sisi tutajiachilia tushindwe na misisimuko yenye makosa au tujiachilie kuhofu mwanadamu. Tukisitawisha namna inayofaa ya hofu, tutasaidiwa tutende kwa hekima. “Hofu kwa Yehova ndio mwanzo wa hekima.” (Mithali 9:10; Zaburi 111:10, NW) Ni kweli, inatupasa tupende Mungu kwa moyo wetu wote, nafsi, akili, na imara yote. (Marko 12:30) Na inatupasa pia tuwe katika staha nyingi mno kwake, tukimheshimu, au, kwa maneno ya malaika yule, ‘tuhofu Mungu na kumpa yeye utukufu, kwa sababu saa ya hukumu kwa yeye imewasili.’—Ufunuo 14:7, NW.
[Picha katika ukurasa wa 30]
Kama Uria angalikuwa na hofu ya kina kirefu kwa Yehova, hofu kwa mwanadamu isingalikuwa mtego kwake