Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/1 kur. 10-15
  • Kuogopa Mungu Je! Kunaweza Kukunufaisha Wewe?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuogopa Mungu Je! Kunaweza Kukunufaisha Wewe?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Zifikirie Manufaa
  • Ni Lazima Sisi Tujifunze Kuogopa Yehova
  • Sitawisha Moyo wa Kumhofu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kujifunza Kupata Furaha Katika Kumhofu Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kwa Nini Tunapaswa Kuhofu Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kwa Nini Kuhofu Mungu, Si Wanadamu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/1 kur. 10-15

Kuogopa Mungu Je! Kunaweza Kukunufaisha Wewe?

“Ogopa Mungu wa kweli na kushika amri zake. Kwa maana huo ndio wajibu mzima wa mwanadamu.”—MHUBIRI 12:13, NW.

1, 2. (a) Ibada yetu kwa Mungu inapasa iwe juu ya msingi gani? (b) Hata hivyo, ni jambo gani jinginelo ambalo Mungu anataka? (Kumbukumbu 10:12)

JE! MANENO “kuogopa Mungu” yanasikika ya kiajabu kwako wewe? Wengi huenda wakahisi kwamba ikiwa wao wanapenda Mungu kweli kweli, haiwapasi wamwogope yeye pia. Je! ni lazima kweli kweli sisi tufanye yote haya mawili? Ikiwa ndivyo, woga kwa Mungu unatunufaisha sisi jinsi gani?

2 Maandiko yanaonyesha kwamba ibada na utumishi wetu kwa Mungu lazima vitegemee msingi wa upendo. Yesu alifanya jambo hilo liwe wazi wakati yeye alipotuambia tupende Yehova kwa moyo wetu wote, nafsi yote, akili zote, na nguvu zote. (Marko 12:30, NW) Lakini umaana wa kuogopa Mungu unakaziwa pia katika Neno lake. Kwa kuelezwa wazi sana, sisi tunaambiwa kwenye Mhubiri 12:13, NW: “Ogopa Mungu wa kweli na kushika amri zake. Kwa maana huu ndio wajibu mzima wa mwanadamu.” Je! Yehova anakosa upatani kwa kutuagiza sisi tumwogope yeye na kumpenda wakati ule ule mmoja?

3. Kwa habari ya woga, ni jambo gani ambalo lazima lizingatiwe katika akili?

3 Si hivyo hasa—ikiwa sisi tunazingatia akilini kwamba kuna aina tofauti-tofauti za woga. Wakati watu wanapofikiri juu ya woga, kwa kawaida wao wanakuwa katika akili na hisia ya kigonjwa-gonjwa ambayo inaharibu tumaini na kutufanya tuvunjike moyo. Kwa wazi, Yehova hangetutaka sisi tuhisi hivyo juu yake! Baba yetu wa kimbingu anatutaka sisi tumjie yeye sawasawa na vile mtoto angejia baba yake, akiwa na uhakika wa kupata upendo wa baba yake na wakati ule ule awe anaogopa kumchukiza yeye. Woga kama huo utatusaidia sisi tubaki tukiwa watiifu kwa Baba yetu wa kimbingu wakati tunaposhawishwa kufanya makosa. Huo ni ‘woga wa kimungu’ ambao unafaa, ulio wa lazima Wakristo wawe nao. —Waebrania 5:7; 11:7, NW.

4. Ni woga wa namna gani ambao upendo ungeondoa kabisa?

4 Yehova si kama hakimu asiye na hisia ambaye anaadhibu tu watumishi wake kila wakati ambapo wao wanateleza. Bali, yeye anawapenda wao na anataka wafanikiwe. Kwa hiyo ikiwa sisi tunafanya kosa la kutotazamia au kutenda dhambi, woga kwa Yehova haupasi kutuzuia kusema naye kumweleza jambo hilo. (1 Yohana 1:9; 2:1) Woga wetu wenye staha kwa Yehova si woga wa kuogopa kurudishiwa maneno makali au kukataliwa. Ni kama vile tunavyosoma kwenye 1 Yohana 4:18, NW: “Hamna woga katika upendo, bali upendo mkamilifu unatupa woga nje, kwa sababu woga umejizoeza kizuizi.” Hata hivyo, ‘Upendo mkamilifu” haungeondoa kabisa ile staha yenye kina kirefu na woga unaofaa ambao sisi tunapaswa kuwa nao kwa Yehova akiwa ndiye Muumba wetu na Mpaji-uzima.—Zaburi 25:14.

Zifikirie Manufaa

5. (a) Ni jinsi gani tu hekima inaweza kupatwa? (b) Ni jambo gani lililosukuma mmoja aliyekuwa mzoelevu wa dawa za kulevya abadili mwendo wake usio wa hekima katika maisha?

5 Acheni sisi tufikirie baaahi ya manufaa ambazo zinatiririka kutokana na “kuogopa Yehova.” Kwa mfano, huo unatuongoza tupate hekima ya kweli. Wanadamu wamejaribu njia nyingi. wamejitahidi kabisa kabisa kupata hekima hiyo, lakini wao wameshindwa kwa sabahu wanapuuza kanuni moja ya msingi: “Kuogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima.” (Zaburi 111:10: Mithali 9:10, NW) Fikiria jinsi woga huo ulisaidia mmoja aliyekuwa mzoevu wa dawa za kulevya atende kwa hekima. Yeye anaeleza hivi: “Wakati mimi nilipokuwa nikitwaa maarifa ya kujua Mungu, nilisitawisha pia woga wa kuumiza maoni yake au kumchukiza. Mimi nilijua yeye anachungulia, na nilikuwa na tamaa kubwa ya kukubaliwa machoni pake. Woga huo ulinisukuma mimi kuharibu dawa za kulevya nilizokuwa nazo kwa kuzipiga maji chooni.” Mwanamume huyo alishinda mazoea mabaya yake, akaweka wakfu maisha yake kwa Yehova, na sasa ni mhudumu katika Johannesburg, Afrika Kusini.

6. Ni jinsi gani “kuogopa Yehova” kutatupa sisi himaya dhidi ya mambo mabaya, nao utatuongoza kwenye nini?

6 Je! wewe ungependa kuepuka yaliyo mabaya? “Kuogopa Yehova humaanisha kuchukia mabaya.” (Mithali 8:13, NW) Ndiyo, woga huo unaofaa unaweza Kukuepusha na tabia nyingi mbaya mbaya ambazo Mungu anakataza, kama vile kuvuta sigareti, kutumia vibaya dawa za kulevya, ulevi, na ukosefu wa adili katika ngono. Zaidi ya kupendeza Yehova, wewe unajipatia mwenyewe himaya pia dhidi va kutopatwa na mambo mabaya sana ambayo yanapata watu, kutia na magonjwa ya kuogopesha sana ambayo wao wanajitia katika hali ya kuweza kupatwa nayo. (Warumi 1:26, 27; 12:1, 2; 1 Wakorintho 6:9, 10; 1 Wathesalonike 4:3-8) Si kwamba woga kwa Mungu utakusaidia wewe kujikinga tu dhidi va yaliyo mabaya na mapotovu bali pia utakuongoza ufanye mambo yanayotakata na yenye kufaa, kwa maana sisi tunaambiwa kwamba “Kuogopa Yehova ni kwenye kutakata.”—Zabun 19:9, NW.

7, 8. (a) Msichana mmoja mdogo alionaje kwamba “kuogopa Yehova” kunaongoza kwenye furaha? (b) Taja manufaa zaidi ambazo zinakuja kwa wale ambao wanaogopa Yehova.

7 Furaha ni mradi mwingine unaotafutwa na watu walio wengi. Ni jinsi gani wewe unavyoweza kuipata? Neno la Mungu linasema: “Mwenye furaha ni mtu aliye katika woga kwa Yehova.” (Zaburi 112:1; 128:1, NW) Jambo aliloona msichana mmoja tineja linathibitisha hilo. Yeye alikuwa amejihusisha katika namna zote za ngono zisizo halali, vilevile katika kuwasiliana na ulimwengu wa roho na kuiba. Ndipo yeye alipoanza kujifunza Biblia na kuona uhitaji wa kusikiliza Yehova na kumwogopa. Yeye anasema: “Kujua Yehova ndicho kitu kilicho bora zaidi ambacho kimenipata mimi. Yehova alinisaidia mimi sana katika kupata ukweli na furaha. Mimi nahisi ninawiwa deni kubwa na yeye kwa sababu yeye alifungua macho yangu na kunipa nafasi ya kufikiri kweli kweli na kumpata yeye. Sasa mimi nataka kusaidia watu wengine wapate furaha hiyo.”

8 Yehova anaahidi pia kwamba yeye atathawabisha ‘wale wanaoogopa jina lake.’ (Ufunuo 11:18, NW) Zaidi ya hilo, “woga kwa Yehova una elekeo la kuelekea uzima, na mmoja atautumia usiku akiwa ameridhika; mmoja hatatembelewa na kilicho kibaya. (Methali 19:23 NW) Kwa kweli, “kuogopa Yehova” ndio utakaotuletea sisi mambo yote ambayo tungehitaji wakati wo wote. Wakati woga huo unapounganishwa na unyenyekevu, tokeo ni “mautajiri na utukufu na uzima.​—Mithali 22:4. 10:27, NW.

9. Kwa sababu gani “kuogopa Yehova” kunaongoza kwenye mwendo ule mmoja tu katika maisha ambao unaonyesha hekima? (Ayubu 28:28; Mika 6:9)

9 Je! hilo halitupi kitia-moyo kamili ili kuogopa yule Mungu wa kweli? Kweli kweli, “woga kwa Yehova” unavutia sana sana. Huo unaongoza kwenye mambo yote ambayo yatatuletea sisi uradhi wa kweli—jambo ambalo ni haba sana leo. Jinsi yalivyo ya kutia moyo maneno haya yaliyovuviwa na Mungu: “Ingawa huenda mtenda dhambi akawa anafanya jambo baya mara mia moja na kuendelea kwa muda mrefu kama afurahiavyo yeye, bado mimi najua pia kwamba itageuka kuwa vizuri kwa wale wanaoogopa yule Mungu wa kweli, kwa sababu wao walikuwa katika woga kwa yeye. Lakini haitageuka kuwa vizuri hata kidogo kwa yule mwovu, wala yeye hatarefusha siku zake ambazo ni kama kivuli, kwa sababu yeye hayumo katika kuogopa Mungu.” (Mhubiri 8:12, 13, NW) Ni mwanamume gani ambaye hatamani mambo ‘yageuka kuwa mazuri’ kwake? Jambo hilo lenye kufurahisha litafurahiwa na wale tu ambao wanaogopa Mungu.—Zaburi 145:19, NW.

10. Ni sababu za muhimu ambazo zinapasa kutusukuma sisi kuogopa Mungu?

10 Je! hilo halipasi kutufanya tupige moyo konde tuonyeshe staha nyingi sana, ndiyo, kicho, kwa Baba yetu wa kimbingu Yehova? Kwa kweli, inatupasa sisi tuwe na hofu inayofaa ya kutotaka kumchukiza yeye. Sisi tunathamani kwa kina kirefu fadhili za upendo zote na wema ambao yeye ametuonyesha sisi. Kila kitu ambacho sisi tunacho kimetoka kwake. (Ufunuo 4:11) Tena, yeye ndiye Hakimu Mkuu Zaidi, yule Mwenye Nguvu Zote, mwenye uwezo wa kuua wale wanaokosa kumtii yeye. “Endeleeni kupangilia-pangilia wokovu wenu wenyewe kwa woga na mtetemeko,” anahimiza mtume Paulo. —Wafilipi 2:12; Hosea 3:5; Luka 12:4, 5, NW.

11. (a) Nimwelekeo gani unaopasa kuepukwa na Wakristo katika siku za mwisho hizi? (b) Ni roho ipi inayopasa kukuzwa?

11 Hapa hapana kionyesho cha kwamba sisi tunaweza kupata wokovu kwa kuchagua kufuata mwelekeo wa kizembe, kufanya kidogo iwezekanavyo na kutumainia kwamba kwa njia fulani mambo yatageuka yawe mazuri. Huo sio mwelekeo wa kuonyeshwa na Wakristo ambao katika siku za mwisho hizi wanajitahidi kudumisha uhusiano pamoja na yule Mmoja ambaye anaweza kuona moja kwa moja mpaka ndani ya mioyo yao na ambaye anajua fikira na makusudio yao ya ndani ndani kabisa. (Yeremia 17:10) Ni wale tu ambao wana utambuzi unaofaa wa Yehova watakaokubaliwa na yeye kuwa anawajua. Yeye anasema: “Kuelekea moja huyu, basi, mimi nitatazama, kuelekea yule mmoja anayesumbuka na mwenye majuto katika roho na mwenye kutetemekea neno langu.”—Isaya 66:2, NW.

Ni Lazima Sisi Tujifunze Kuogopa Yehova

12. (a) Ni katika njia gani mbalimbali taifa la Israeli lilipendelewa juu ya mataifa mengine? (b) Yehova alitazamia limrudishie nini?

12 Kufikiria shughuli za Yehova pamoja na Israeli kunaweza kukaza zaidi juu ya akili zetu uhitaji wa kumwogopa yeye. Hakuna taifa jingine lililopata utunzaji na fikira kama hizo kutoka kwa Mwenye Enzi Kuu wa ulimwengu wote mzima. (Kumbukumbu 4:7, 8, 32-36; 1 Samweli 12:24) Kwa macho yao wenyewe Waisraeli waliona mambo ambayo Yehova aliwatenda Wamisri, ambao, kwa kutokuwa na woga kwake yeye, walitumikisha na kuonea watu wake. Yeye alitazamia Waisraeli wamrudishie nini? “Kusanya wale watu, wale wanaume na wale wanawake na wale wadogo-wadogo na mkaaji wako wa kigeni ambaye yumo ndani ya malango yako, ili kwamba wao wapate kusikiliza na ili kwamba wao wapate kujifunza, kwamba wao lazima waogope Yehova Mungu wako na kujiangalia kutekeleza maneno yote ya sheria hii. Na wana wao ambao hawajapata kujua wanapaswa kusikiliza, na wao lazima wajifunze kuogopa Yehova Mungu wako sikuzote ambazo wewe unaishi juu ya udongo ambao wewe unauvuka Yordani kumiliki huo.”—Kumbukumbu 31:12, 13; 14:23, NW.

13. Ni nini linalopasa kuwa lenye hangaikio la msingi kwa wazazi kuhusu watoto wao?

13 Kama kwa habari ya Waisraeli, watumishi wa ki-siku-hizi wa Mungu “lazima wajifunze kuogopa Yehova.” Lo, ni daraka kama nini ambalo jambo hilo linaweka juu ya sisi sote —hasa wazazi! Wazazi, jiulizeni wenyewe: ‘Ni jinsi gani mimi naweza kusaidia watoto wangu wapate moyo ambao unaogopa Yehova?’ Siku moja wakati ambapo wao watakua wawe wakubwa na kuondoka nyumbani, ni jambo gani jingine linalozidi hilo ambalo litaandaa himaya nzuri zaidi kwa watoto wako, kiroho, kiakili, au kimwili? Yehova mwenyewe anaukazia umaana wa jambo hilo wakati anaposihi hivi: “Kama tu wao wangekuza moyo huu wao wa kuniogopa mimi na kushika amri zangu zote sikuzote, ili kwamba iweze kwenda vizuri kwao na wana wao kwa wakati usiojulikana!”—Kumbukumbu 5:29; 4:10, NW.

14. Taja jambo moja ambalo wazazi wanapasa kuzingatia katika akili katika kuzoeza watoto wao wawe waogopaji wa Yehova, na eleza jinsi jambo hilo linavyopasa kutumiwa.

14 Mkristo ye yote ambaye amelea jamaa atakubali kwa utayari kwamba hilo si jukumu rahisi. Hata hivyo, Neno la Mungu lililovuviwa linaleta mambo kadha ya muhimu kwenye fikira za wazazi. Moja ni kuanza wakati watoto ni wachanga. Uchanga gani? Wakati Waisraeli walipokutana kupokea maagizo kutoka kwa Yehova, “wadogo-wadogo” walitiwa ndani. (Kumbukumbu 29:10-13; 31:12, 13, NW) Kwa wazi, wanawake Waisraeli walikuja pamoja na watoto wachanga wao katika pindi hizo, kwa kuwa wote walitakwa wawe katika hudhurio. Kutoka pale pale penye “utoto mchanga,” wana na binti zao wangejifunza uhitaji wa kutulia na kusikiliza kwenye mikusanyiko hiyo. (2 Timotheo 3:15, NW) Kwa hiyo wewe uje pamoja na “wadogo-wadogo” wako kwenye mikutano. Pia, wahusishe wao katika utumishi wa shambani mara tu wao wanapoweza kuwa na ushiriki. Vijana wengi wamejifunza kutoa gazeti au trakti hata kabla wao hawajaanza kuhudhuria shule. Anza mapema kufundisha “wadogo-wadogo” wako, kwa njia ndogo-ndogo, kuogopa Yehova.

15. Ni nini jambo la pili, na ni jinsi gani wazazi wanavyoweza kulifanya?

15 Jambo jingine ni kufanya mambo kwa upatani-upatani. Jambo hilo linaweza kufanywa ikiwa sisi sikuzote tunashikamana na Neno la Mungu katika mazoezi, nidhamu, na maagizo ambayo sisi tunawapa watoto wetu. Hata wakati inapokuja kwenye starehe au tafrija, uwe mwenye upatani katika kuruhusu kanuni za Biblia ziamue ni mambo gani yatakayoruhusiwa katika pindi hizo. (Waefeso 6:4) Jambo hilo litataka jitihada, kama vile Neno la Mungu linavyoonyesha waziwazi sana wakati linaposema: “Na maneno haya ambayo mimi ninakuamuru wewe leo lazima yathibitike kuwa juu ya moyo wako; na lazima wewe ukaze hayo kikiki katika mwana wako na kusema juu yayo wakati wewe unapoketi katika nyumba yako na wakati wewe unapotembea barabarani na wakati wewe unapolala na wakati wewe unapoamka.” (Kumbukumbu 6:4-9; 4:9; 11:18-21, NW) Upatani huo kwa muda wa miaka kadha utasaidia sana watoto wako kukuza moyo ambao unaogopa Yehova.

16. (a) Ni nini jambo la tatu, na kwa sababu gani hilo ni la maana sana? (b) Ni maswali gani ambayo wazazi wangeweza kujiuliza wenyewe?

16 Wazazi lazima pia wajitahidi kukaza juu ya akili na mioyo ya watoto wao kwamba wao wenyewe, kama wazazi, ni “waogopaji wa Yehova.” (Zaburi 22:23, NW) Njia moja ambayo katika hiyo wao wanaweza kufanya hilo ni kwa kutumia mashauri ya kitheokrasi wanapozoeza na kutia nidhamu watoto wao. Hilo ndilo jambo la tatu litakalofikiriwa. Jiulize mwenyewe: ‘Je! mimi ninakuwa na funzo la Biblia kwa ukawaida pamoja na watoto wangu?’ ‘Je! mimi natumia kwa ukamili kwa ajili ya watoto wangu wenye umri mdogo zaidi misaada kama vile Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na Kumsikiliza Mwalimu Mkuu?’ ‘Wanapoendelea kuwa wenye umri mkubwa zaidi, je! mimi ninatumia kile kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako na zile makala “Vijana Wanauliza” katika Amkeni!?’ ‘Je! mimi napanga kuwe na tafrija na vitumbuizo vinavyofaa ambavyo havitakuwa na madhara juu ya watoto wangu?’ ‘Je! mimi nimekubali mambo ambayo yamesemwa na tengenezo la Yehova juu ya elimu ya juu zaidi?’ ‘Je! mimi ninaagiza watoto wangu kulingana na hayo?’ ‘Je! miradi ambayo mimi nimeweka kwa ajili ya watoto wangu ni ile ambayo itawasaidia wao kuwa na “woga wa kimungu”?’—Waebrania 5:7, NW.

17. Ni nani wanaonufaika wakati watoto wanapojifunza kuogopa Yehova? Toa mfano.

17 Manufaa na furaha zitakuja si kwa watoto wako tu bali kwako wewe pia kwa kufanya yote uwezayo ili kuwaagiza katika “kuogopa Yehova.” Kwa mfano, Shahidi mmoja wa kike ambaye mwishoni mwa siku kama yeye anavyosema, wakati anapokuwa akihisi ni kama amepata makovu ya pambano kali yeye anaona mambo yote yanafaa anaposikia binti yake wa miaka saba akimpelekea Yehova sala. Machozi yanamlenga-lenga machoni na anameza kitonge cha mate anaposikiliza sala ya binti yake: “Yehova mwenye upendo, asante kwako wewe kwa mema yote ambayo wewe umenifanyia mimi leo. Na asante kwako wewe kwa chakula changu. Saidia ndugu wote katika gereza na kambi za mateso wapate chakula, Yehova, na ndugu na dada wote ambao wamekonda katika nchi nyinginezo. Wasaidia wao pia wapate chakula cha kutosha, Yehova. Na wale ambao ni wagonjwa, wasaidie wapate nafuu ili wao waweze kwenda kwenye mikutano. Acha malaika tafadhali wanitunze mimi wakati ninapolala usiku, Yehova, na mama yangu na baba, na ndugu yangu, na nyanya yangu na babu, na ndugu na dada wote katika ukweli. Kupitia Yesu Mwana wako, Amen.”

18. Ni jinsi gani sisi tunavyoathiriana mtu na mwenzake katika jambo hili la kuogopa Yehova?

18 Katika jambo hili la kuogopa Yehova, ni lazima sisi tukumbuke kwamba sisi tunaathiriana mtu na mwenzake kwa mfano tunaoweka. Wazazi wanaathiri watoto wao. Wazee na watumishi wa huduma wanaathiri makundi yao. Waangalizi wanaosafiri wanaathiri wale ambao wao wanatumikia. Kwa wazi, hiyo ndiyo sababu wafalme katika Israeli waliagizwa kusoma Sheria ya Mungu sikuzote za maisha yao ili kwamba wao ‘wapate kujifunza kuogopa Yehova.’ (Kumbukumbu 17:18-20, NW) Mfano ambao mfalme angeweka katika kuogopa Yehova ungeweza kuathiri taifa nzima.

19. Historia inatolea nini ushuhuda kwa mintarafu ya Waisraeli?

19 Historia inatoa ushuhuda kwa uhakika wa kwamba Israeli, wakiwa taifa, walipoteza woga wao kwa Yehova. Wao walifikiri kwamba kuwa na hekalu katika Yerusalemu kulitumika kama himaya kwao, kama namna fulani ya hirizi ya “bahati,” bila kujali kama wao walitii au hawakutii sheria zake. (Yeremia 7:1-4; Mika 3:11, 12) Lakini wao walikosea. Yerusalemu na hekalu lake liliharibiwa. Baadaye, wakati wao waliposimamishwa tena wakiwa taifa, wao walishindwa tena kuonyesha woga unaofaa kwa Yehova. (Malaki 1:6) Kuna mengi ambayo sisi tunaweza kujifunza kutokana na jambo hilo lililowapata, nayo yatazungumzwa katika makala inayofuata.

20. Ni jinsi gani sisi tungeweza kujumlisha kwa muhtasari sababu inayofanya sisi tupaswe kuogopa Yehova?

20 Kumbuka, basi, kwamba kuogopa Yehova hakudhoofishi upendo wetu kwake; badala ya hivyo, kunautia nguvu na kuukaza zaidi. Si kwamba utii kwa amri zake zote utathibitisha sisi tunaogopa tu Yehova bali kwamba sisi tunampenda pia. Yote hayo mawili ni ya muhimu. Haiwezekani kuwa na moja kati ya mambo hayo bila kuwa na lile jingine. Ni jambo la maana kama nini wazazi kukaza kikiki ndani ya watoto wao hali hiyo ya kuogopa Yehova na upendo kwa ajili yake! na jambo hilo linaletea wenye umri mkubwa na mdogo kadhalika furaha kubwa kama nini! Basi, sisi na tuhisi jinsi ile ile kama mtunga zaburi wakati yeye aliposema: “Unganisha kwa umoja moyo wangu ili kuogopa jina lako wewe.”—Zaburi 86:11, NW.

Mambo ya Kufikiria Sana

◻ Ni jinsi gani sisi tunavyoweza kupenda na pia kuogopa Yehova?

◻ Ni nini baadhi ya manufaa za kuogopa Yehova?

◻ Ni mambo gani matatu ambayo yanaweza kusaidia wazazi wawape watoto wao msaada wa kukuza moyo ambao unaogopa Yehova?

◻ Ni jinsi gani sisi tunaathiriana mtu na mwenzake katika jambo hili la kuogopa Yehova?

[Picha katika ukurasa wa 12]

Kuogopa Yehova kutasaidia vijana wakatae vishawishi vya kufanya yaliyo mabaya

[Picha katika ukurasa wa 14]

Wazazi wanapaswa wasaidie watoto wao kukuza hali inayofaa ya kuogopa Yehova

[Picha katika ukurasa wa 15]

“Itageuka kuwa vizuri kwa wale ambao wanaogopa yule Mungu wa kweli.”—Mhubiri 8:12, NW.

[Credit Line]

By courtesy of Hartebeespoort Snake and Animal Park

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki