Wimbo 180
Kitabu cha Mungu Mwenyewe—Hazina
1. Kuna kitabu, kurasa ni nyingi,
Chaletea watu tumaini.
Mawazo yacho yana nguvu nyingi;
“Wafu” chafufua, hupa macho.
Na kitabu hicho ndicho Biblia.
Kiliandikwa na watu kale,
Waliomupenda Yehova sana,
Roho yake ikawachochea.
2. Waliandika mambo ya viumbe,
Ulimwengu ulivyotokea.
Ukamilifu wa mutu mwanzoni
Paradiso ilivyopotea.
Wanasema juu ya malaika
Ambaye kapinga enzi kuu.
Kukawa dhambi na huzuni nyingi,
Ushindi wa Yah waja upesi.
3. Leo twaishi muda wa furaha.
Ufalme wa Yesu kazaliwa.
Leo Yehova huwapa wokovu
Wote wenye umoja na yeye.
Kitabu kinazo habari njema;
Hakilinganishwi na dhahabu.
Hupa tumaini kubwa zaidi;
Ndiyo hadithi kubwa zaidi.