Wimbo 67
Wekeni Hazina Mbinguni
1. Na tumupende Yehova,
Baba wa nuru juu!
Zawadi kamili zote,
Zatoka kwake yeye.
Hupa nguo hata nyumba,
Mbegu, jua na mvua.
Tumushukuru Mukimu
Atupaye uzima.
2. Ni jambo la upumbavu
Tukijikaza, mali,
Za muda tu kurundika,
Hazitupi uzima!
Lakini na tutosheke
Na tunayohitaji,
Na kwa mema na tushike
Uzima wa hakika.
3. Tutumie mali, nguvu
Tulishe “masikini”,
’Wa njaa, habari njema
Watumai Ufalme.
Hapo ndipo Mungu, Kristo,
Watakuwa rafiki;
Tuweke hivyo hazina
Mbinguni kwa ’milele.