Endelea Kuhubiri Ule Ufalme
“Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia nzima yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo uie mwisho utakuja.”—MATHAYO 24:14, NW.
1, 2. (a) Ni nini iliyo kazi ya maana zaidi ya karne hii, na ni kwa kadiri gani hiyo Inaendelea kufanywa? (b) Kuna ithibati gani ya baraka ya Yehova juu ya kazi hii?
KUHUBIRI zile habari njema za Ufalme wa Mungu ndiyo kazi iliyo ya maana zaidi ya karne hii. Hilo ndilo jambo ambalo yule Mungu Mweza Yote anataka lifanywe sasa, nalo linaendelea kufanywa kwa utimizo wa Neno lake la kiunabii. Itikio lako kwa kazi hiyo litaathiri mwisho wako wa milele.—1 Wakorintho 9:16, 23.
2 Inasisimua kuona kwamba hesabu ya wanaoshiriki katika kazi hii ya kuhubiri inaendelea kuongezeka, sasa wakiwako watu zaidi ya milioni tatu wenye kufanya sehemu yao. Hesabu za watu walio wengi zaidi ya wakati mwinginewo wote wanaingia ile huduma ya wakati wote. Na watu wengi zaidi wenye kupendezwa wanakubali funzo la Biblia na kutia jitihada ya kujifunza kufanya mapenzi ya Mungu.
3. Huenda watu fulani wakasema nini juu ya ule uhitaji wa kuendelea na kuhubiri zile habari njema?
3 Hata hivyo, nyakati nyingine huenda watu fulani ‘wakaachilia kufanya yaliyo bora’ na ‘kuchoka’ kwa ka diri ambavyo ile kazi ya kuhubiri inahusika. (Wagalati 6:9; Waebrania 12:3, NW) Huenda wao wakasema kwa mba zile habari njema tayari zimekwisha kuhubiriwi kwa mweneo mkubwa katika eneo lao na kwamba wati wamechukua msimamo wao na sasa wanaudhika wakat sisi tunapotembelea makao yao. Wale wanaofanya ile kazi ya kuhubiri huko wanapata matokeo machache sam au hawapati yo yote. Kwa hiyo, wao wanahisi, labdasehemu iliyo ya maana zaidi ya ile kazi imekwisha kufanywa, na hakuna uhitaji wa kuendelea. Njia hii ya kufikiri ina kosa gani?
Kwa Sababu Gani Tuendelee Tu?
4. Ni jambo gani ambalo linapasa kutusukuma sisi twendelee kuhubiri hata katika eneo ambamo itikio ni la hali ya chini?
4 Kwanza, kuvumilia kwetu kwa uaminifu katika ile kazi ya kuhubiri hakupasi kutegemee kama watu wanatusikiliza au hawatusikilizi. Yeremia alihubiri kwa miaka 40 katika Yerusalemu hata ingawa ni wachache sana ambao walisikiliza na wengi walimpinga yeye kwa jeuri. Kwa sababu gani yeye aliendelea tu? Kwa sababu yeye alikuwa akifanya kazi ambayo Yehova alikuwa ameamuru na kwa sababu ya maarifa yake ya kiunabii juu ya mambo ambayo yangepata Yerusalemu yalimlazimisha aendelee kusema. (Yeremia 1:17-19) Yeye alisema: “Moyoni mwangu kumekuwamo kama moto uwakao, uliofungwa ndani ya mifupa yangu, nami nimechoka kwa kustahimili, wala siwezi kujizuia.” (Yeremia 20:7-10) Hali yetu inafanana na hiyo. Ni Yehova, kupitia Yesu Kristo, ambaye aliamuru kwamba “zile habari njema” zinapasa kuhubiriwa katika dunia yote inayokaliwa. (Mathayo 24:14) Wakati watu wanapokataa kusikiliza, hiyo inatupa sisi nafasi ya kuonyesha kina cha upendo wetu na bidii ya kujitolea Yehova kwa kuendelea tu kufanya jambo ambalo linafaa. (1 Yohana 5:3) Zaidi ya hilo, wakati sisi tunapotafakari juu ya mambo ambayo yanangoja aina ya wanadamu katika wakati ujao ulio karibu, ni jinsi gani sisi tunavyoweza kujizuia tusijaribu kuonya jirani zetu?—2 Timotheo 4:2.
5. (a) Ni kwa sababu gani nyingine inatupasa sisi tuvumilie katika ile kazi ya kuhubiri? (b) Ni jinsi gani ile kazi ya kuhubiri ni msingi wa hukumu?
5 Tena, kuhubiri kwa Yeremia kulikuwa kazi ya hukumu kweli kweli. Katika 607 K.W.K., hakuna wo wote wa wale ambao walipatwa na kifo au wakatiwa utumwani wakati Yerusalemu ulipoanguka wangeweza kudai kwamba wao hawakujua ni kwa sababu gani jambo hilo lilikuwa likiwapata wao. Kwa miaka 40 kabla ya hapo, Yeremia alikuwa amekuwa akiwaonya juu ya matokeo yayo hayo kama wao wangeendelea kuwa waasi dhidi ya Yehova. (Linganisha Ezekieli 2:5.) Vilevile leo, kule kuhubiriwa kwa zile habari njema kama “ushuhuda kwa mataifa yote” ni msingi wa hukumu. Mtume Paulo anaonyesha jambo hilo wazi wakati yeye anaposema kwamba Kristo Yesu ataleta mlipizo wa kisasi juu ya “wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.” (2 Wathesalonike 1:8, 9, NW) Watu watahukumiwa kulingana na itikio kwa zile habari njema. Kwa sababu ya hiyo, ile kazi ya kuhubiri lazima iendelee kufanywa kwa kupaaza sauti yenye kusikika waziwazi moja kwa moja mpaka ule mwisho. (Ufunuo 14:6, 7) Hakuna kitu cho chote kinachopasa kuzuia ujumbe muhimu huo usiletwe kwa wale watu mara nyingi iwezekanavyo. Jambo hilo linaweka daraka kubwa juu ya watumishi wote wa Yehova walio wakfu.
6. Ingawa ujumbe wetu huenda ukawa unajulikana mahali pengi, kwa sababu gani sisi tunahitaji kuendelea kuhubiri?
6 Ni kweli, huenda sisi tukawa tayari tumekwisha kuhubiri zile habari njema kwa mweneo mkubwa katika eneo letu. Lakini kuna mambo mengi sana yanayotukia katika ulimwengu ambayo hata ingawa watu wengi wamesikia ujumbe wetu, wao wangeusahau karibuni kama sisi tungekoma kuhubiri. Fikira juu ya yale mapinduzi makubwa, vitendo vya wavamizi harama, migomo, zile kashifa mbaya sana, na matukio mengine ambayo yanatangazwa kwa mweneo mkubwa. Halafu kuna zile namna nyingi za vitumbuizo vinavyopendwa na wengi sana na viondoshafikira vingine. Ni lazima sisi tuendelee kuhubiri ili tuzidi kuweka ujumbe wetu mbele ya wale watu kujapokuwa na mambo mengine yote hayo yanayovuta fikira zao.
7. Ni jinsi gani itikio la wengi leo linafanana na lile la Waisraeli kwa utoaji unabii wa Isaya, lakini kwa sababu gani jambo hilo halipasi kutuzuia kuhubiri?
7 Wakati wengi wanapojaribu kutupuuza sisi, inatupasa sisi tukumbuke ni watu wa aina gani ambao nabii Isaya alilazimika kuhubiria. Yehova alimwambia hivi: “Kwa maana wao ni jamii ya watu waasi, wana wasio wa kujawa na ukweli, wana ambao wamekuwa hawana nia ya kusikia ile sheria ya Yehova; ambao wamesema kwa wale wanaoona, ‘Ni lazima ninyi msione,’ na kwa wale wenye kuwa na njozi, ‘Ni lazima ninyi msione njozi za mambo manyofu yo yote kwa ajili yetu. Semeni kwetu mambo laini; oneni njozi za mambo madaganyifu. Geukieni kando kutoka ile njia; kengeukeni kutoka kile kijia. Sababisheni yule Mmoja Mtakatifu wa Israeli akome kwa sababu yetu tu.’” Hata hivyo, kwa uaminifu Isaya aliambia wale watu: “Yehova ni Mungu wa hukumu. Wenye furaha ni wale wanaoendelea kumtarajia yeye.” (Isaya 30:9-11, 18, NW) Inatupasa sisi tufanye ivyo hivyo. Maadamu sisi tunaendelea tu, ujumbe wetu utapenya ndani kwa kadiri fulani. Watu fulani watasikiliza na wengine hawatasikiliza. Lakini wote watakuwa na ile nafasi ya kusikia.
Ni Jinsi Gani Wao Watasikia?’
8. Ingawa huenda watu wakaonekana kuwa wamekwisha kuchukua msimamo wao dhidi ya ule ukweli, ni mambo gani ambayo yangeweza kubadili akili zao?
8 Labda sisi tunahisi kwamba watu katika eneo fulani wamechukua msimamo ulio dhahiri na wamepiga moyo konde kukataa ujumbe wetu au hata kuupinga. Lakini kumbuka, hali katika maisha za watu inabadilika sikuzote. Huenda wao wakaelekeana na matatizo au hali mpya-mpya kesho, juma linalokuja, au mwezi unaokuja ambazo zitafanya wao waupokee ukweli. Huenda wao wakasikia juu ya matukio yenye kusumbua akili katika ulimwengu au labda wapatwe na mabadiliko makubwa ya kiuchumi, ugonjwa, au kifo katika jamaa. Mambo kama hayo huenda yakasababisha wao waamke na kutaka kujua sababu ya taabu kubwa yao. Ikiwa sisi tunaendelea kuhubiri, ,vao watajua mahali pa kugeukia.
9. Ni jinsi gani kazi yetu ya kuhubiri ingeweza kulinganishwa na ile ya wafanya kazi wenye kuponyosha uhai wa watu katika eneo la msiba?
9 Hali yetu ingeweza kulinganishwa na ile ya wafanya kazi wa kuponyosha uhai wa watu katika eneo lenye msiba, kama vile baada ya tetemeko la dunia. Huenda watu fulani wakawa wanafanya kazi katika eneo ambamo ni waokokaji wachache zaidi walipatikana lakini uhakika wa kwamba wafanya kazi wenzao wanakuta waokokaji wengi zaidi katika eneo jingine haungesababisha wao wajilegeze na kuacha. Badala ya hivyo, wafanya kazi wote wa kuokoa uhai wanazidi tu kuvumilia bila kuchoka hata wakati wao wanapohisi huenda kusiwe tena na waokokaji katika kisehemu chao walichogawiwa. Na, ndipo, nyakati fulani-fulani, inapokuwa kwamba wao wanapata bado kuna mwokokaji mwingine. Ule utafutaji unaachishwa tu inapokuwa kwamba wakati ambao umepita unafunua kwamba hakuna tumaini zaidi. Basi, utafutaji wetu haujaachishwa bado, na sisi bado tunapata maelfu juu ya maelfu ambao wanataka kuponyoshwa kutoka ulimwengu wa kale huu na kuokoka “dhiki kubwa.” (Ufunuo 7:9, 14, NW) Hata katika maeneo ambayo yamefanywa kwa ukamili na ambamo watu walio wengi hawaitikii, bado mna matokeo fulani. Na kuna sababu zaidi za kuendelea kuhubiri.
10. Ni jinsi gani tu watu watajua mahali pa kugeukia ikiwa wao wanataka kutstfuta ule ukweli, kulingana na Warumi 10:13, 14?
10 Watu wanahitaji kuendelea kukumbushwa kwamba “kila mtu ambaye huita juu ya jina la Yehova ataokolewa.” Hata hivyo, kama vile Paulo anavyoendelea kusema katika barua yake kwa Waroma, “ni jinsi gani wao wataita juu ya huyo ambaye katika yeye wao hawajatia imani? Ni jinsi gani, tena, wao watatia imani katika huyo ambaye wao hawajasikia juu yake? Ni jinsi gani, tena, wao watasikia bila mtu fulani wa kuhubiri?” (Warumi 10:13, 14, NW) Maneno hayo yanapasa kukaza juu ya kila mmoja wetu ule uhitaji wa kuendelea tu katika kuhubiri zile habari njema za Ufalme wa Mungu.
11. Ni kizazi kipya gani ambacho kinatokea, na ni daraka gani ambalo sisi tunalo kuelekea wachanga hao wanaokua kufikia utu mzima?
11 Ule wakati wa mwisho unapokuwa unaendelea, watoto wamezaliwa na wakakua kufikia utu mzima au kufikia umri wa kujichukulia madaraka yao wenyewe. Mara nyingi vijana hawa wanakuwa hawajaelekeza fikira zo zote kwenye ule ukweli. Huenda ikawa wazazi wao walikataa ule ujumbe na hata wakanena dhidi ya huo. Lakini sasa vijana hawa wana umri wa kutosha kutumia fikira zao wenyewe kufikiria kwa uzito juu ya hali za ulimwengu, juu ya wakati ujao, na juu ya kusudi lao katika maisha. Wao pia wanahitaji kuita juu ya jina la Yehova ikiwa wao wataokolewa. Lakini “ni jinsi gani . . . wao watatia imani katika huyo ambaye wao hawajasikia juu yake” (Warumi 10:14, NW) Katika visa vingi vijana-matineja na watu wazima hawa walio vijana-vijana wanaitikia ule ukweli, kwa hiyo sisi tunahitaji kuwatafuta-tafuta na kuwahubiria.
12. Ni jinsi gani kuendelea kwetu na ile kazi ya kuhubiri kunafanyiza wonyesho wa rehema ya Yehova?
12 Uhakika wa kwamba ile njia ingali imefunguliwa ili kuhubiri kufanywe ni wonyesho wa rehema ya Yehova. Mtume Petro anaandika: “Yehova si wa polepole kwa habari ya ahadi yake, kama watu fulani hufikiri ni upolepole, bali yeye husubiri na ninyi kwa sababu yeye hatamani watu wo wote waharibiwe bali hutamani wote wafike kwenye toba. Zaidi ya hayo, ifikirieni saburi ya Bwana yetu kuwa wokovu.” (2 Petro 3:9, 15, NW) Tamaa ya Yehova kwamba namna zote za wanadamu ziokolewe inaonyeshwa si kwa kuwa kwake mwenye subira tu katika kuruhusu wakati kabla yeye hajafikiliza hukumu bali pia kwa kuendelea kwake kuvutia wanadamu wamgeukie yeye na kupata kuokolewa. (1 Timotheo 2:4, NW) Wakati sisi tunapoendelea kuhubiri zile habari njema, sisi tunakazia rehema ya Mungu, na katika njia hii sisi tunamsifu yeye.
Kuepuka Hatia ya Damu
13, 14. (a) Ni jinsi gani kazi yetu ya kuhubiri inavyoweza kulinganishwa na ile kazi ya mlinzi, kama ilivyotajwa katika unabii wa Ezekieli? (b) Kwa sababu gani Paulo angeweza kusema kwamba yeye ‘hakuwa na hatia kwa damu ya mtu awaye yote’ na ni jinsi gani tu Mashahidi wa Yehova wanaweza kusema hivyo leo?
13 Lile daraka la Mashahidi walio wakfu wa Yehova kuonya watu juu ya hukumu ya Mungu inayokuja linaweza kulinganishwa na lile la Ezekieli katika wakati wake. Yeye alichaguliwa akatajwa wazi kuwa mlinzi kwa ile nyumba ya Israeli. Mgawo wake ulikuwa kuonya Waisraeli kwamba wangeuawa ikiwa wao hawangegeukia mbali kutoka njia zao mbaya. Ikiwa yeye akiwa mlinzi angekosa kusikizisha onyo hilo, bado watu waovu wale wangeuawa, lakini damu yao ingekuwa juu ya kichwa cha yule mlinzi mwenye kupuuza wajibu. Katika jambo hilo Yehova anaonyesha mwelekeo wake kuhusu ufikilizaji hukumu: “Sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?”—Ezekieli 33:1-11.
14 Mtume Paulo alikiri daraka lake la kuwa mlinzi, akiambia hivi wale wazee kutoka Efeso: “Kwa hiyo nawashuhudia wote siku hii ya leo, ya kuwa mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote.” Kwa sababu gani yeye angeweza kusema hivyo? Yeye aliendelea: “Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.” (Matendo 20:26, 27) Ndivyo ilivyo kwa ile jamii ya mlinzi leo, yale mabaki ya wafuasi wapakwa-mafuta wa Yesu Kristo. Wote hao, pamoja na milioni zaidi ya tatu za waandamani wao ambao wana tumaini la kuokoka ule mwisho wa huu mfumo wa mambo na kupokea uzima wa milele duniani, lazima wasipunguze kamwe mwendo wa kuhubiri zile habari njema za Ufalme wa Mungu na kuonya juu ya mfikilizo unaokuja wa hukumu yake. Katika njia hii wao wanaepuka hatia ya damu.
15. Kulingana na Ezekieli sura ya 9, ni nani waliotiws alama, na ni nani ambaye aliitia alama?
15 Ile kazi ya leo ya kuhubiri inaelezwa kiunabii katika Ezekieli sura 9. Hapa, adhabu ya Yehova iliamuliwa kupata ule mji wa Yerusalemu. Kabla ya mfikilizo wa hukumu hiyo, mwanamume mmoja aliyevikwa kitani na mwenye kidau cha wino cha mwandishi kwenye viuno vyake anaambiwa aende kupitia ule mji na kutia alama juu ya vipaji vya nyuso za wote wale ambao wanapiga kite juu ya makuruhi yanayofanywa humo. Wakati kazi hii ya kutia alama ingekamilishwa, wote katika ule mji isipokuwa wale waliotiwa alama ya kuokolewa wangeuawa. Kwenye ukamilisho wa kazi yake ya kutia alama, mwanamume yule aliripoti: “Nimefanya kama ulivyoniamuru.” (Ezekieli 9:11) Yeye alitekeleza kwa uaminifu mgawo wake mpaka mwisho.
16. (a) Yule mwanamume aliyevikwa kitani anafananisha nani leo? (b) Ni jinsi gani lile swala la kuondolewa malawama juu ya enzi kuu ya Yehova linavyotushurutisha kuendelea kuhubiri?
16 Yule mwanamume aliyevikwa kitani anafananisha yale mabaki ya wapakwa mafuta walio wafuasi wa Kristo, na wao wanaungwa na ule “umati mkubwa” wa “kondoo wengine.” Lile swala kubwa leo, kama lilivyokuwa katika wakati wa Ezekieli, ni kuondolewa malawama juu ya enzi kuu ya Yehova. Kwa habari ya ule mwisho wa mfumo mbovu uliopo wa mambo kwenye ile vita ya siku ile kuu ya Mungu Mweza Yote, Yehova anasema: “Na yale mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” (Ufunuo 7:9; Yohana 10:16; Ezekieli 39:7, NW) Ili mataifa yajue hivyo, ni lazima watumishi wa Yehova duniani waendelee kuhubiri jina na kusudi lake kuwa ushuhuda kwa mataifa yote.
17, 18. (a) Ni jinsi gani kuendelea kwetu kuhubiri kunavyotusaidia sisi kuendelea kuwa katika lile lindo? (b) Ni ripoti gani ambayo sisi sote tunataka kufanyia Yehova wakati yeye aletapo ile kazi ya kuhubiri kwenye umalizio wayo, na ni jinsi gani tu sisi tunavyoweza iufanya hivyo?
17 Kwa kuzidi kuhubiri zile habari njema za Ufalme, sisi tunadumisha kukesha kwetu wenyewe. Sisi tunazidi kuung’amua ule umaana wa jina na kusudi la Yehova. Tukipunguza mwendo, tumaini letu la Ufalme linaweza kudhoofika tunaweza na kuvutwa fikira na “mawasiwasi na mali na anasa za maisha haya . . . na kutoleta cho chote kwenye ukamilifu.” (Luka 8:14, NW) Kwa kuvumilia kwa juhudi katika kutangaza “habari njema,” sisi tunafuata kwa uaminifu zile amri za Bwana-mkubwa wetu, Yesu Kristo: “Endeleeni kutazama, endeleeni kuamka, kwa maana ninyi hamjui ni lini ulio ule wakati uliowekwa rasmi. Lakini yale ambayo mimi nasema kwa ninyi mimi nasema kwa wote, Endeleeni kuwa katika lile lindo.”—Marko 13:33, 37, NW.
18 Basi, acheni sisi sote tuvumilie katika kutafuta-tafuta ‘wale ambao wanapiga kite’ maadamu Yehova anaruhusu ule wakati wa kufanya hivyo. Sisi sote, kama tu wa yale mabaki ya wapakwa-mafuta au tu wa “kondoo wengine,” na tuwe waaminifu katika kutekeleza mgawo wetu kuhubiri zile habari njema za ule Ufalme katika dunia yote inayokaliwa, kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote. (Mathayo 24:14, NW) Wakati Yehova mwenyewe atakapoleta kazi hii kwenye mwisho wayo kwa kuanzisha “dhiki kubwa,” kila mmoja wetu na aweze kusema kwa Yehova, ‘Sisi tumefanya kama vile ambavyo wewe umeamuru.’
Je! Wewe Unakumbuka?
◻ Matokeo yanaonyesha nini kwa habari ya kuhubiri kwetu?
◻ Ni sababu gani nyingine zinazofanya itupase sisi kuendelea kuhubiri?
◻ Ni jinsi gani kuhubiri kwetu ni wonyesho wa rehema ya Yehova?
◻ Ni jinsi gani sisi tunavyoweza kuendelea kuwa safi bila hatia ya damu ya watu wote?
◻ Ni jinsi gani kuhubiri kwetu kunavyotusaidia sisi kuendelea kuwa katika lile lindo?
[Chati katika ukurasa wa 28]
MATOKEO YA KUHUBIRI KWA MUDA WA MIAKA SABA
Hesabu va Waliobatizwa Hudhuriola Ukumbusho Hesabu va Mafunzo va Biblia
1981 119,836 5,987,893 1,475,177
1982 138,540 6,252,787 1,586,293
1983 161,896 6,767,707 1,797,112
1984 179,421 7,416,974 2,047,113
1985 189,800 7,792,109 2,379,146
1986 225,868 8,160,597 2,726,252
1987 230,843 8,965,221 3,005,048