Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/97 uku. 8
  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Kupiga Mbiu ya ‘Maneno ya Unabii’
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Wasaidie Waelewe
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Saidia Wengine “Kuyashika Yaliyoandikwa”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Toa Mwaliko kwa Kila Mtu Aliye na Kiu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 2/97 uku. 8

Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka

1 Twaonyesha uthamini wetu wenye kina kirefu kwa ahadi za Ufalme wa Mungu tunaposhiriki kwa moyo wote katika huduma ya Kikristo. Twahitaji kushiriki katika kazi hii kwa hisi ya uharaka. Kwa nini? Kwa sababu wafanyakazi ni wachache, mwisho wa mfumo huu mbovu wa mambo unakaribia, na maisha za wale walio katika eneo letu zimo hatarini. (Eze. 3:19; Mt. 9:37, 38) Daraka hilo zito lahitaji jitihada yetu katika huduma. Twaweza kuonyeshaje hisi ya uharaka kuhusu utendaji wetu wa utumishi wa shambani? Kwa kutayarisha mapema utoaji mbalimbali ulio mzuri, kwa kuwa wenye bidii ya uendelevu katika kutafuta watu popote ambapo huenda wakapatikana, kwa kuweka maandishi mazuri ya wote wanaoonyesha kupendezwa, kwa kuwarudia bila kukawia ili kuendeleza kupendezwa huko, na kwa kukumbuka kwamba kwa kuwa uhai wahusika, twapaswa kuona huduma yetu kwa uzito. Madokezo yafuatayo huenda yakawa yenye msaada tunapojitayarisha kutoa habari njema kwa hisi ya uharaka wakati wa Februari. Toleo litakuwa kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!

2 Unaweza kuanza mazungumzo kwa kutaja kifupi baadhi ya matatizo yanayokabiliwa katika jumuiya, kisha uweze kusema:

◼ “Watu wengi huamini kwamba kuna Mungu, lakini wanajiuliza: ‘Ni wakati ujao wa aina gani anaotutakia?’ Ungejibuje hilo? [Ruhusu itikio.] Je, ulijua kwamba Biblia hueleza waziwazi mapenzi ya Mungu kwa wanadamu na hatua anazochukua kuyatimiza?” Fungua ukurasa wa 301 katika kitabu Upeo wa Ufunuo. Soma Ufunuo 21:1 katika fungu la 1, kisha usome maelezo yanayotolewa kulihusu katika nusu ya mwisho wa fungu la 2. Fungua picha kwenye ukurasa 302 uonyeshe kinachomaanishwa kwa wakati wetu ujao. Soma Ufunuo 21:4 katika fungu la 6. Ikiwa kuna itikio zuri, toa kitabu. Panga wakati unaofaa wa kurudi ili kuendeleza mazungumzo.

3 Unaweza kuendeleza mazungumzo ya wakati uliopita ya Ufunuo 21:1, 4 kwa utoaji huu mfupi:

◼ “Katika ziara yangu iliyopita, tuliongea kuhusu ahadi ya Mungu ya kutayarisha jamii mpya ya kidunia kwa ajili ya wanadamu. [Elekeza fikira tena kwenye picha iliyo kwenye ukurasa wa 302 katika kitabu Upeo wa Ufunuo.] Je, ungependa kuona familia yako ikifurahia hali kama hizo? [Ruhusu itikio.] Swali ni, Ahadi za Mungu ni zenye kutegemeka kadiri gani? Tafadhali ona yale ambayo yeye mwenyewe husema.” Soma Ufunuo 21:5, 6a katika fungu la 8 kwenye ukurasa wa 303. Uliza swali lililochapwa la fungu la 9 kwenye ukurasa wa 304, na usome jibu, kutia ndani sentensi ya mwisho ya fungu hilo. Taja toleo la funzo la Biblia bila malipo. Panga kulionyesha baadaye.

4 Kwa kuwa wengi wanahangaishwa na matatizo yenye kuongezeka yanayokabili wanadamu, unaweza kusema jambo kama hili katika ziara yako ya kwanza:

◼ “Karibu kila mtu ninayekutana naye anahangaishwa na matatizo tunayokabili katika jumuiya yetu. [Taja machache.] Kwa miongo kadhaa wanadamu wameahidi kuleta matatuzi ya daima, na wengine wamejaribu kufanya hivyo. Unafikiri ni nini ambacho husababisha hali ziendelee kuwa mbaya zaidi? [Ruhusu itikio.] Biblia hutoa elezo ambalo watu walio wengi hawajapata kamwe kulifikiria. Kitabu cha Ufunuo hufafanua vita iliyotokea mbinguni. Ona tokeo, kama inavyosemwa kwenye Ufunuo 12:9.” Soma mstari huo, kisha ufungue ukurasa wa 182 katika kitabu Upeo wa Ufunuo. Tumia picha ueleze kujihusisha kwa Shetani katika mambo ya duniani. Toa kitabu kwa mchango wa kawaida. Fanya mipango ya kurudi uzungumzie jinsi Mungu atakavyotatua matatizo ya wanadamu.

5 Ikiwa uliahidi kurudi ueleze utatuzi wa Mungu wa matatizo ya leo, unaweza kujaribu mfikio huu:

◼ “Nilifanya jitihada ya pekee kurudi ili tuweze kuendeleza mazungumzo yetu juu ya utatuzi halisi wa matatizo yanayokabili wanadamu. Katika ziara yangu iliyopita, tuliona kwamba Biblia humtambulisha Shetani Ibilisi kuwa anayeongoza vibaya dunia nzima inayokaliwa na watu. Kwa kuwa yeye ni kiumbe-roho mwenye uwezo kupita ule wa binadamu, unafikiri kuna njia ya kuondoa uvutano wake? [Ruhusu itikio.] Tafadhali ona vile Biblia husema.” Soma na ueleze Ufunuo 20:1-3. Kwa kutumia picha iliyo kwenye kurasa 4-5 za kitabu Ujuzi, onyesha hali zitakavyokuwa bila uvutano wa Shetani. Mtolee funzo la Biblia na ujitahidi kulianzisha mara hiyo.

6 Kukiwa na watu wengi wenye kupendezwa na mazingira, unaweza kusema jambo kama hili ili kuanzisha mazungumzo:

◼ “Tumeona kwamba karibu kila mtu anahangaikia uchafuzi wa hewa, maji, na chakula. Katika nchi kadhaa hali ya mazingira tayari inatishia uhai. Kwa kuwa Mungu ndiye Muumba wa dunia, unafikiri atafanya nini kuhusu hilo? [Ruhusu itikio.] Biblia husema kwamba Mungu atatoza hesabu kuhusu jinsi tunavyoitumia dunia. [Soma Ufunuo 11:18b.] Wazia kuishi kwenye dunia ambayo haina uchafuzi!” Eleza juu ya ahadi ya Mungu ya paradiso, kama inavyoonyeshwa kwenye Ufunuo 21:3, 4. Onyesha picha iliyo kwenye ukurasa wa 302 katika kitabu Upeo wa Ufunuo. Ikiwa kuna kupendezwa, toa kitabu na upange kurudi.

7 Unaporudia mtu aliyeonyesha kupendezwa katika dunia ya Paradiso, unaweza kusema hivi:

◼ “Katika ziara yangu iliyopita, tulikubaliana kwamba ili kutatua matatizo ya dunia iliyochafuliwa, itambidi Mungu aingilie mambo ya mwanadamu. Lakini swali ni, Lazima tufanye nini ili kuokoka kuingia katika ulimwengu mpya wenye uadilifu uliofanyizwa na Mungu?” Soma Yohana 17:3. Alika mwenye nyumba atwae manufaa ya mtaala wetu wa funzo la Biblia bila malipo ili apate ujuzi huu wa pekee.

8 Ni pendeleo lililoje kutumiwa tuwe wafanyakazi wa mavuno wa siku ya kisasa na kufanya kazi ya kuhubiri ya kuokoa uhai! Sisi sote na tuendelee kuwa wenye shughuli katika kutoa habari njema kwa hisi ya uharaka, ‘tukijua kwamba kazi yetu ya jasho si bure kuhusiana na Bwana.’—1 Kor. 15:58.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki