Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/98 uku. 1
  • Watoto—Nyinyi Ni Shangwe Yetu!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watoto—Nyinyi Ni Shangwe Yetu!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Kujiwekea Miradi ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vijana—Miradi Yenu ya Kiroho Ni Ipi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Njia za Kupanua Huduma Yako
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Pata Shangwe Katika Mapendeleo Uliyo Nayo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 3/98 uku. 1

Watoto—Nyinyi Ni Shangwe Yetu!

1 Wavulana na wasichana wachanga, je, mwajua amri ya Yehova kwamba mwapaswa kutiwa ndani ya shughuli za kutaniko? (Kum. 31:12; Zab. 127:3) Ni shangwe kuwa nanyi kando yetu tumwabudupo Yehova pamoja! Mwachangamsha mioyo yetu mnapoketi kwa utulivu na kusikiliza kwa makini. Sisi huwa wenye furaha hasa mnapojaribu kutoa maelezo kwa maneno yenu wenyewe. Kutaniko zima lapendezwa mnapotoa sehemu zenu mlizogawiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, mnapojiunga kwa hamu pamoja nasi katika utumishi wa shambani, na tunaposikia kwamba mnatoa ushahidi kwa ujasiri kwa wanashule wenzenu na walimu.—Zab. 148:12, 13.

2 Twataka mjue kwamba twawaonea fahari tunapoona adabu zenu nzuri, sura yenu iliyo nadhifu, mwenendo wenu ulio safi, na staha yenu kwa watu wazima. Shangwe yetu huzidi hasa mnapoonyesha kwamba ‘mwamkumbuka Muumba wenu Mtukufu’ kwa kujiwekea miradi ya kitheokrasi wenyewe.—Mhu. 12:1; Zab. 110:3.

3 Tuambieni Miradi Yenu: Mvulana mmoja mwenye umri wa miaka minane alimwambia mwangalizi wa wilaya hivi: ‘Kwanza ningependa kubatizwa, kisha ningependa kusaidia katika kutaniko kwa kutumika katika mfumo wa sauti na kushughulika na maikrofoni, kuwa mkaribishaji, kusaidia kushughulikia fasihi, kusoma kwenye mafunzo ya kitabu na Mafunzo ya Mnara wa Mlinzi. Kisha ningependa niwe mtumishi wa huduma, kisha mzee. Pia ningependa kuwa painia na kwenda kwenye shule ya painia. Kisha ningependa kwenda Betheli, niwe mwangalizi wa mzunguko au mwangalizi wa wilaya.’ Alionyesha uthamini mzuri kama nini kwa pendeleo la kumtumikia Mungu!

4 Mnapofanya maendeleo ya kimwili na kiroho, twafurahia kuona mkifikia miradi yenu. (Linganisha Luka 2:52.) Kila mwaka, maelfu kati yenu huwa wahubiri wasiobatizwa kisha hustahili kubatizwa wakiwa watumishi wa Yehova waliojiweka wakfu. Shangwe yetu huongezeka kisha tunapowaona mkifikia kufanya upainia-msaidizi na hata kuingia utumishi wa wakati wote. Kweli, watoto, nyinyi ni shangwe yetu na chanzo kizuri ajabu cha kumsifu Baba yetu wa kimbingu. Yehova na awabariki nyinyi sana!—Mit. 23:24, 25.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki