Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Machi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Machi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Machi 2
  • Juma Linaloanza Machi 9
  • Juma Linaloanza Machi 16
  • Juma Linaloanza Machi 23
  • Juma Linaloanza Machi 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 3/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Machi

Juma Linaloanza Machi 2

Wimbo 3

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 15: “Fulizeni Kufanya Hili Katika Ukumbuko Wangu.” Hotuba itolewe na mzee. Eleza kifupi juu ya kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 80-81, ukikazia umaana wa kuhudhuria Ukumbusho.

Dak. 22: “Litie Ndani ya Wengine Lile Tumaini la Uhai Udumuo Milele.” Mazungumzo ya makala na wasikilizaji. Eleza kifupi jinsi maswali yanavyoweza kutumiwa kwa matokeo kuendeleza mazungumzo. Toa vielelezo kadhaa vya maswali yenye kuonyesha majibu unayotaka na ya maoni ambayo huenda yakatumiwa katika utoaji. (Ona kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 51-52, fungu la 10-12.) Panga mhubiri mwenye kuweza atoe wonyesho wa mojawapo wa madokezo ya utoaji mbalimbali wa kuanzia pamoja na ziara ya kurudia, akionyesha funzo la Biblia likianzishwa.

Wimbo 88 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 9

Wimbo 60

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Mambo Makuu ya Broshua Mpya, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji kuhusu sababu zinazoifanya Biblia istahili kuchunguzwa nasi. Broshua hii ilitayarishwa ili kusaidia watu ambao huenda wakawa wameelimishwa vizuri lakini hawajui mengi kuhusu Biblia. Badala ya kujaribu kuwasadikisha kwamba Biblia imepuliziwa na Mungu, broshua hiyo yaacha mambo ya hakika yajisemee yenyewe. Twapaswa kuisoma na kuwagawia wengine, kutia na wale tunaojifunza nao.

Dak. 22: “Je, Tutaufanya Tena?” (Fungu la 1-11) Maswali na majibu. Simulia mambo makuu ya kampeni ya mwaka jana ya upainia-msaidizi ya miezi ya Machi, Aprili, na Mei, kama ilivyoripotiwa katika 1998 Yearbook. Taja idadi ya watu waliofanya upainia-msaidizi kwenu wakati huo. Zungumzia manufaa za kibinafsi tunazopata moja kwa moja kutokana na kupainia, na uonyeshe jinsi ambavyo jitihada ya ziada huchangia maendeleo ya kutaniko. Eleza mipango ya utumishi inayopangwa kwenu katika Aprili na Mei kusaidia wengi zaidi wapainie. Wahubiri wanaweza kupata fomu za ombi baada ya mkutano.

Wimbo 195 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 16

Wimbo 43

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Karibisha watu wote wenye kupendezwa wahudhurie hotuba ya pekee Machi 29. Hotuba yenyewe ina kichwa “Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia.”

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 22: “Je, Tutaufanya Tena?” (Fungu la 12-19) Maswali na majibu. Pitia sifa za ustahili zinazoonyeshwa katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 113-114. Eleza jinsi upainia-msaidizi humtayarisha mtu kwa ajili ya utumishi wa painia wa kawaida. Karibisha wengine waliofanya upainia-msaidizi miezi ya mwaka uliopita ya Machi, Aprili au Mei waeleze jinsi ambavyo wamepanga ratiba yao watimize takwa la saa 60. Ni mfano upi wa ratiba kwenye ukurasa wa mwisho wa nyongeza ambao uliwafaa zaidi? Wakati uruhusupo, simulia mambo yaliyoonwa katika 1987 Yearbook, ukurasa wa 48-49, 245-246. Tia moyo wahubiri wapate fomu za ombi baada ya mkutano.

Wimbo 224 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 23

Wimbo 94

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia moyo wote waanze kukaribisha watu wenye kupendezwa kwenye Ukumbusho, Aprili 11. Onyesha nakala ya mwaliko, na usihi wote wazipate na kuanza kuzigawanya juma hili. Tangaza majina ya wote watakaofanya upainia-msaidizi Aprili. Eleza kwamba si kuchelewa mno kuleta fomu ya ombi. Eleza ratiba nzima ya mikutano ya utumishi wa shambani kama ilivyopangiwa Aprili.

Dak. 20: Tayarisha Wapya kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji. Wale wanaoongoza funzo katika kitabu Ujuzi wapaswa kufikiria kumtayarisha mwanafunzi wao ashiriki katika utumishi wa shambani. Onyesha yanayosemwa katika kitabu Ujuzi, kwenye ukurasa wa 105-106, fungu la 14, na ukurasa wa 179, fungu la 20. Pitia utaratibu uliopo katika Mnara wa Mlinzi, Novemba 15, 1988, ukurasa wa 16-17, fungu la 7-10, kwa wapya kutambuliwa kuwa wahubiri wasiobatizwa. Fikiria madokezo yaliyo katika nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996, fungu la 19, kusaidia wahubiri wapya wasiobatizwa waanze utumishi.

Dak. 15: Sanduku la Swali. Maswali na majibu. Mzee apitia habari iliyo katika kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 131, fungu la 1 na la 2.

Wimbo 47 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Machi 30

Wimbo 29

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wote walete ripoti zao za utumishi wa shambani za Machi. Onyesha matoleo ya wakati uliopo ya magazeti, dokeza ni makala zipi unazoweza kukazia unapoyatoa, na utaje mambo fulani mahususi ya kuzungumzia. Pitia “Vikumbusha vya Ukumbusho,” na ueleze mipango ya kwenu ya Ukumbusho. Wote wapaswa kufanya mipango ya kumalizia ya kusaidia wanafunzi wa Biblia na wengine wenye kupendezwa wahudhurie. Kumbusha wote wahakikishe kufuata usomaji wa Biblia wa Ukumbusho ulioratibiwa kwa ajili ya Aprili 6-11, kama ionyeshwavyo katika Kuyachunguza Maandiko Kila Siku.

Dak. 13: “Watoto—Nyinyi Ni Shangwe Yetu!” Maswali na majibu. Simulia jambo lililoonwa kutoka Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 1987, ukurasa wa 25.

Dak. 20: Njia Fulani za Kupigana na Uchovu wa Kiroho. Wazee wawili wazungumzia sanduku lililo katika Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1986, ukurasa wa 19. Katika kila ya “Dalili za Uchovu,” eleza Kimaandiko jinsi ambavyo mtu anaweza kunufaika na “Misaada ya Kuvumilia.” Kisha hoji wahubiri wawili waeleze jinsi matumizi ya mambo hayo yalivyowasaidia wadumishe nguvu yao ya kiroho.

Wimbo 140 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki