Litie Ndani ya Wengine Lile Tumaini la Uhai Udumuo Milele
1 Ijapokuwa mwanadamu ametafuta njia za kupunguza uzee na kuongeza muda wake wa maisha, kuzeeka na kifo bado ni visivyoepukika. Twashukuru kama nini kwamba Biblia hueleza sababu kwa nini wanadamu huzeeka na kufa, na vilevile jinsi ambavyo madhara ya uzee yatakavyoondolewa na kifo kufutwa kabisa. Kweli hizi zaelezwa kwa njia ya kusadikisha katika kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kitabu hicho chajibu waziwazi maswali yenye kutatanisha juu ya uhai na kifo, kikielekeza msomaji kwenye wakati ambapo Paradiso itarudishwa.
2 Katika Machi tutatoa kitabu Ujuzi tukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani. (Mt. 28:19, 20) Kisha tutafanya ziara za kurudia kwa wote ambao wanaonyesha kupendezwa na ujumbe wa Ufalme. Kwa njia hii twaweza kulitia ndani ya wengine lile tumaini la uhai udumuo milele. (Tito 1:2) Ili kutimiza hili, huenda ukaona madokezo yafuatayo kuwa yenye msaada.
3 Unapofanya ziara ya kwanza, waweza kuuliza swali hili:
◼ “Je, umepata kujiuliza ni kwa nini wanadamu hutamani sana maisha marefu zaidi? [Ruhusu itikio.] Wabudha, Wakristo, Wahindu, Waislamu, na wengine wote wana tumaini la uhai baada ya kifo.” Fungua kitabu Ujuzi kwenye sura ya 6, “Sababu Gani Tunazeeka na Kufa?,” na usome fungu la 3. Sababu juu ya maandiko yaliyotajwa. Ukirejezea maswali mawili yaliyo mwishoni mwa hilo fungu, mwulize mwenye nyumba ikiwa angetaka kujionea majibu yeye mwenyewe. Akitaka kufanya hivyo, endelea kuzungumzia mafungu machache yanayofuata. Funzo laanzishwa! Kama sivyo, mtolee kitabu asome, na ufanye mipango ya kurudi, hasa kati ya siku moja au mbili mzungumzie maswali hayo.
4 Unapofuatia angusho la kitabu “Ujuzi,” unaweza kusema hivi:
◼ “Nimerudi tuchunguze yale maswali mawili juu ya kifo tuliyoacha bila kujibiwa.” Mkumbushe mwenye nyumba hayo maswali. Kisha zungumzia habari iliyo katika sura ya 6 chini ya kichwa kidogo “Njama Yenye Uovu.” Ikitegemea hali, endelea na funzo au tumia swali la mwisho, mwishoni mwa fungu la 7 ili kuweka msingi wa kipindi kitakachofuata. Fanya mipango hususa ya kurudi. Mpe mwenye nyumba kikaratasi cha ukaribishaji ikiwa chapatikana, na ufafanue kifupi jinsi mikutano ya kutaniko inavyofanywa. Mkaribishe kwa uchangamfu ahudhurie.
5 Katika kutoa ushahidi wa mlango hadi mlango ama wa vivi hivi, waweza kuanzisha mazungumzo kwa kusema hivi:
◼ “Je, umepata kujiuliza wakati ujao wetu na wa dunia utakuwaje? [Ruhusu itikio.] Biblia hueleza wakati ujao kwa neno moja—Paradiso! Hiyo hueleza kwamba mwanzoni, Mungu alifanya sehemu ya dunia kuwa paradiso maridadi alimowaweka wanadamu wawili aliowaumba. Walipaswa waijaze dunia yote, wakiigeuza hatua kwa hatua iwe paradiso. Ona ufafanuzi huu wa jinsi lazima iwe ndivyo ilivyokuwa.” Fungua kitabu Ujuzi kwenye ukurasa wa 8, na usome fungu la 9, chini ya kichwa kidogo “Uhai Katika Paradiso.” Kisha zungumzia mambo yaliyo katika fungu la 10, na usome andiko lililotajwa, Isaya 55:10, 11. Jitolee kuendelea na mazungumzo ya jinsi uhai utakavyokuwa katika Paradiso iliyorudishwa na mmalizie pamoja fungu la 11-16. Au toa kitabu kwa mchango wa kawaida na umtie moyo huyo mtu akisome yeye mwenyewe, na upange mkutane tena mkizungumzie.
6 Ikiwa funzo halikuanzishwa mara ya kwanza, unaweza kujaribu kufanya hivyo kwenye ziara ya kurudia kwa kusema:
◼ “Kama tulivyozungumza katika mazungumzo yetu ya mwisho, ni kusudi la Mungu kwamba dunia nzima igeuzwe iwe paradiso. Hilo latokeza swali hili, Paradiso itakuwaje?” Fungua kitabu Ujuzi kwenye sura ya 1, na mjifunze fungu la 11-16, chini ya kichwa kidogo “Uhai Katika Paradiso Itakayorudishwa.” Baadaye onyesha picha iliyoko kwenye ukurasa wa 4-5, na umwulize huyo mtu ikiwa angependa kuishi katika mazingira mazuri kama hayo. Kisha soma sentensi ya kwanza ya fungu la 17 kwenye ukurasa wa 10. Ikitegemea hali, endelea na funzo au useme kwamba katika ziara yako ifuatayo utaeleza linalotakiwa ili mtu aishi katika Paradiso itakayorudishwa. Mwachie kikaratasi cha ukaribishaji ikiwa chapatikana, eleza ratiba ya mikutano, na umkaribishe kwa uchangamfu huyo mtu ahudhurie kwenye Jumba la Ufalme.
7 Kitabu Ujuzi ni chombo bora kabisa cha kutumia katika kufunulia wengine “uhai udumuo milele” ulioahidiwa na Mungu. Kuongoza kwako mafunzo ya Biblia na watu kwaweza kutia ndani yao tumaini hili tukufu lililopuliziwa na Mungu “asiyeweza kusema uwongo.”