Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 2/15 kur. 22-24
  • Vinaweza Kukusaidi Wewe Kuhubiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vinaweza Kukusaidi Wewe Kuhubiri
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kueneza Habari Njema Leo
  • Sehemu ya Magazeti Katika Kueneza Habari Njema
  • Kuhubiri Hadharani na Kutoka Nyumba Hadi Nyumba
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika Huduma
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • “Habari Njema Lazima Zihubiriwe Kwanza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Twapaswa Kuwa Walimu, Si Wahubiri Tu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 2/15 kur. 22-24

Vinaweza Kukusaidi Wewe Kuhubiri

YESU alipoambia wanafunzi wake waende kuhubiri, inaelekea kwamba wao hawakujua umaana kamili wa jambo alilokuwa akiwaelekeza wakafanye. (Mathayo 10:7) Kwa kutii, walifuata kielelezo chake wakaenda kutoka “jiji hadi jiji na kutoka kijiji hadi kijiji, wakihubiri na kutangaza habari njema za ufalme wa Mungu.” (Luka 8:1, NW) Huo ukawa ndio mwanzo mdogo wa jitihada ya kuhubiri ambayo imezileta habari njema za Ufalme kwenye fikira za watu duniani pote.

Katika siku za mapema za kundi la Kikristo, sana sana kuhubiri kulifanywa kwa neno la kinywa. Wanafunzi wa Kristo waliongea na yeyote ambaye angesikiliza. “Kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.”​—Matendo 5:42.

Utegemezo wa kimungu ulionekana wazi katika jambo la kwamba wao waliweza kufanya ishara. (Matendo 14:3) Watu wengi waliponywa kimwili kisha wakabakia pale ili kusikiliza maneno ya ponyo la kiroho. Tokeo ni kwamba, “walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana.”​—Matendo 5:14-16.

Kueneza Habari Njema Leo

Mitume walipokufa, zawadi za maponyo na ndimi zilikoma. Lakini je! hiyo ilibadili agizo ambalo Yesu alikuwa amewapa wanafunzi wake? Sivyo! Yeye alikuwa amewaambia ‘wafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ nao wakiwa wanafanya hivyo, yeye angekuwa pamoja nao “siku zote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.” (Mathayo 28:19, 20, NW) Leo, ithibati ya Kimaandiko iko wazi kwamba tunaishi kwenye umalizio wa mfumo wa mambo. Je! Yesu ametimiza ahadi yake kwamba angekuwa pamoja na wanafunzi wake katika kazi ya kufanya wanafunzi? Ithibati inasema ndiyo!

Kufikia mabilioni ya wakaaji wa dunia kwa neno la kinywa tu kungekuwa kazi isiyowezekana na mwanadamu. Kwa sababu hiyo, msaada umeandaliwa kwa namna ya fasihi za Biblia ambazo watu wanaweza kusoma katika maskani zao wenyewe. Kielelezo, katika 1879 wakati kikundi cha wanafunzi wa Biblia wenye moyo wa bidii kilipotaka kufikisha ujumbe wa Ufalme wa Mungu kwa wengine, wao walianza kutokeza fasihi, kama lile gazeti la Biblia linalojulikana kuwa Mnara wa Mlinzi, na pia trakti zinazoshughulika na habari za Biblia. Kwanza walitumia mashine-chapa za kibiashara kutokeza fasihi hizo. Kufikia 1920 walikuwa na matbaa yao wenyewe ya uchapaji katika jengo la kukodi, na kufikia 1927 wakawa wamejenga kiwanda chao wenyewe cha kuchapia Biblia, vitabu, vijitabu, magazeti, na trakti za kutumiwa na wowote waliotaka kusaidia kutimiza agizo ambalo Yesu aliwapa wanafunzi wake.

Bila kuogopeshwa na wapinzani waliosema kwamba jaribio hilo la uchapaji lingekosa mafanikio, Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi imekuja kuendesha viwanda vya uchapaji katika mabara ya kuzunguka duniani pote. Mwaka jana tu, walitokeza Biblia, vitabu, na vijitabu zaidi ya 63,000,000 na magazeti zaidi ya 582,000,000 katika lugha zaidi ya 200.

Fasihi ambazo wamechapisha zimekuwa za thamani kubwa sana katika kujaza mahitaji ya kiroho ya watu. Vimechapwa vitabu vilivyofanyizwa kwa kusudi la kufikia watu wenye maoni na itikadi fulani hususa. Mamilioni ya vijana wamethamini Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia na Kupata Faida Zote za Ujana Wako. Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha kimekuwa cha thamani kubwa katika kuimarisha vifungo vya jamaa na kufundisha waume na wake waonyeshane upendo mkubwa zaidi. Msaada kwa wapya wanaotaka kufanya ukweli uwe wao wenyewe umekuwa Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli. Watu wanaosoma kitabu hicho wamepata kwamba wanafanywa wafikiri na kusababu mambo kwa kina kirefu zaidi kuhusu uhusiano wao pamoja na Mungu.

Kile kitabu ambacho mara nyingi kilirejezewa kuwa “kombora la bluu,” Kweli Iongozayo kwenye Uzima wa Milele, kimekuwa na matokeo makubwa isivyo kawaida juu ya maisha za mamilioni ya watu. Bado inangojwa ionwe ni watu wangapi zaidi watatumikia Mungu kwa kujifunza kweli za Biblia kutokana na kitabu hicho.

Kwa sasa, wale wanaofanya kazi ya kuhubiri habari njema chini ya mwelekezo wa Yesu wanasaidiwa na kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Mafunzo ya Biblia yanaongozwa pamoja na mamilioni ya watu, wengi wao wakipatanisha maisha zao na viwango vya Biblia.

Mathalani, mwanamume mmoja wa miaka 68 katika Mkoa wa New York alifikishiwa habari na ndugu yake katika Colorado, aliyempelekea fasihi ya Mnara wa Mlinzi aisome. Mwanamume huyo alisoma haraka vitabu vyote vilivyopelekwa na akapendezwa kuanza funzo katika kitabu Kuishi Milele wakati Shahidi mmoja alipozuru kwenye maskani yake. Katika muda wa maisha yake, mwanamume huyo alikuwa amejiwekea mkusanyo wa kumbukumbu ya kihistoria wa silaha zenye thamani kubwa, lakini aliposoma kwamba wale wanaotumikia Yehova hawangejifunza tena vita, alifanya haraka kuuza silaha zake kwa hasara kubwa ya kifedha. (Isaya 2:4) Waaidha, baada ya kuwa amevuta sigareti kwa miaka 53, yeye aliacha mara tu aliposoma kwamba jambo hilo humchukiza Yehova. (2 Wakorintho 7:1) Alipojifunza kwamba anapaswa kushiriki habari njema na wengine, alijitayarisha kwa bidii nyingi sana kuzuru mwanaye na binti-mkwe wake ili akaongee nao na wajukuu wake. Alipoingia katika chumba cha kulala wageni, alipata upendezo mwingi kwa kuona kitabu Kuishi Milele juu ya meza fulani. Binti-mkwe wake alikuwa akijifunza kitabu hicho na alikuwa hajui ataanza-anzaje kumweleza habari hiyo. Wote wawili wamefanya maendeleo bora ya kiroho.

Katika Hispania, mahali pa kukutania Mashahidi wa Yehova palijengwa karibu na kanisa la Kikatoliki. Padri alikuwa na kiruu. Alisema kwamba kama angalijua Mashahidi wangejenga hapo mahali pa kukutania, angalinunua ardhi hiyo kuwazuia kuitumia. Hilo Jumba la Ufalme lina dirisha linaloonyesha kitabu Kuishi Milele. Kila siku mshiriki mmoja wa kundi aligeuza ukurasa mmoja. Wanamji wangesimama pale na kusoma ukurasa mpya. Tokeo ni kwamba, watu wengi walionyesha kupendezwa, na mafunzo ya Biblia yakaanzwa. Ndiyo, kitabu hicho kilithibitika kuwa ushuhuda mnyamavu lakini wenye matokeo.

Sehemu ya Magazeti Katika Kueneza Habari Njema

Wakati toleo la kwanza la Mnara wa Mlinzi lilipotangazwa kwa chapa katika Julai 1879, ni nakala 6,000 tu zilizochapwa. Hata hivyo, kikundi kidogo cha waliolisoma kiliambia wengine yaliyomo kwa hamu nyingi. Leo, Mashahidi wa Yehova zaidi ya 3,500,000 wanatumia zile nakala 13,000,000 zinazochapwa kwa kila toleo ili kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu kuwa ndilo tumaini pekee la aina ya binadamu.

Gazeti hilo limekuwa usaidizi mkubwa katika kueleza habari tofauti za Kimaandiko. Mfululizo mmoja unaoendelea sasa hivi katika Mnara wa Mlinzi umekazia maisha na huduma ya Yesu. Umesaidia mamilioni ya watu kuona katika fikira zao na kuelewa vizuri zaidi masimulizi ya maana katika zile Gospeli.

Mifululizo maalumu katika Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hufanyizwa kwa kusudi la kufikia mioyo ya vijana. Ule mfululizo “Neno la Mungu Li Hai” ulifundisha kanuni nyingi na kuelewesha wazi masuala mengi katika akili za watu. Mfululizo “Vijana Wanauliza . . ” umeshughulika na maswali ya maisha halisi, halafu ukatoa majibu yenye mafaa yakitegemezwa na maandiko ili kuongoza kufikiri na vitendo vya vijana katika hizi siku za taabu-taabu. Wakati Mashahidi wa Yehova wamekazia makala hizo katika kuyatoa magazeti, itikio limekuwa zuri sana.

Lakini zaidi ya makala zinazohusu habari maalumu, mnofu halisi wa Mnara wa Mlinzi umekuwa zile makala kuu, zinazoimarisha imani na usadikisho wa Wakristo wote wa kweli. Makala hizo zenye msingi wa Kimaandiko zinaandaa uthibitisho unaosadikisha juu ya ukaribio wa mwisho wa huu mfumo wa mambo, zinazungumzia utimizo wa manabii ya Biblia, na kutoa mashauri ya kupekua moyo juu ya jinsi Wakristo wanavyopaswa kuishi maisha zao kulingana na nyakati hizi. Kwa kujawa na maarifa hayo, Wakristo wanapiga moyo konde kuyatumia katika utendaji wa kuhubiri mambo wanayojifunza.

Kwa habari ya muda ambao kazi hii ya kuhubiri itazidi kuendelea kabla ya kuja mwisho wa huu mfumo wa mambo, sisi hatujui. Hata hivyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba vichapo vinavyochapwa na kugawanywa na Mashahidi wa Yehova vitaendelea kuwasaidia sana Wakristo wanapofuata utume wa Kiongozi wao, Yesu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki