Wimbo 122
Tukijiongoza Wenyewe Kama “Aliye Mdogo Zaidi”
1. Wamependelewa wale
Wanaotii Mungu.
Wategemeao Mungu
Wanapata baraka.
Na kwa kuwa tumerithi
Kutokukamilika,
Twapaswa kunyenyekea
Na kutii Yehova.
2. ‘Na muwe kama wadogo,’
Yesu akashauri.
Na matokeo bora ni
Amani na umoja.
Aliuweka mufano.
Aliofurahia
Kutii Yehova Mungu
Na kumutumikia.
3. Basi tuwe na hekima
Kwa kuheshimiana
Naye Yesu alifia
Na ndugu yetu pia.
Ndugu ni mali ya Mungu;
Akawapa talanta.
Na tuwe kama wadogo
Nasi tusawazike.
4. Na kanuni ya ukichwa
Inatusaidia
Sisi tujiweke nyuma
Tukazie upendo.
Roho yake Mungu ipo
Kutufanya imara.
Uhusiano na Mungu
Utatunyenyekeza.