Wimbo 54
Ni Lazima Tuwe Watakatifu
1. Ni lazima tuwe watakatifu,
Tumesafishwa kwa Kristo Yesu.
Watu wasafi, wanyenyekevu,
Machoni pa wote tuwe hivyo.
2. Tumewekwa kando kuwa wa Mungu,
“Taifa” na “kondoo wengine.”
Na kwa mwenendo wetu twakiri
Tunataka kushika sheria.
3. Inavutia tusongapo mbele
Tunasafishwa na Mungu wetu.
Awapa watu wake ukweli,
Na ‘tusiangalie ya nyuma.’
4. Na tuzitumie nafasi zote,
Tuzidi kuwa watakatifu.
Tusifu Mungu, tumupendeze,
Ndiye ’Takatifu, mwaminifu.