Wimbo 12
“Mungu Hupenda Mtoaji Mwenye Furaha”
1. Tutumikie Baba na pia kukumbuka
Yeye ni wa furaha na mukarimu.
Asiye na kifani alitoa Mwanaye,
Aponye aina zote za wanadamu.
2. Kutoa kwake kwema mufano tufuate.
Kutoa kwa furaha, ni nia njema.
Wakati, mali zetu vyote ni vya Yehova.
Tukimupa hivyo vyote hatupunguki.
3. Kutoa kwa furaha, kwapendeza Yehova.
Kwapamba mafundisho, pia upendo.
Thamani yake bora kutokapo moyoni;
Tuwe na furaha kuu atuokoe.
4. Kwa Mungu na kwa Yesu asante kwa furaha,
Nguvu tunatoa kwa ibada safi.
Moyo utuongoze tutoe kwa furaha
Tumupendeze Yehova tungali hai.