Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/99 uku. 1
  • Iga Sifa ya Yehova ya Kutobagua

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Iga Sifa ya Yehova ya Kutobagua
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unamwiga Mungu Wetu Asiyebagua?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Thamini Kikamili Sifa za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kuwafikia Wengi Hata Zaidi na Habari Njema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Onyesha Unawajali Watu Kikweli —Kwa Kuhubiri Bila Ubaguzi
    Huduma ya Ufalme—2006
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 12/99 uku. 1

Iga Sifa ya Yehova ya Kutobagua

1 Yehova hujali watu. Yeye hukubali bila kubagua, mtu yeyote anayefanya mapenzi yake. (Mdo. 10:34, 35) Yesu alipowahubiria watu, yeye vilevile hakuwa na ubaguzi. (Luka 20:21) Twahitaji kuiga vielelezo vyao, kama alivyofanya Paulo, aliyeandika: “Kuna Bwana yuleyule juu ya wote, aliye tajiri kwa wote wale wanaomwita.”—Rom. 10:12.

2 Kutangaza habari njema za Ufalme wa Mungu kwa wote tunaokutana nao huleta utukufu kwa Mungu. Lazima twendelee kuwaambia watu wote ujumbe huu mzuri ajabu, bila kujali jamii yao, hali yao ya kijamii, elimu, msimamo wa kifedha, au umashuhuri. (Rom. 10:11-13) Hilo lamaanisha kuwahubiria wote watakaosikiliza—wanaume, wanawake, vijana, na wazee. Twahitaji kwenda kila mlango tumpe kila mwenye nyumba fursa ya kusikia kweli.

3 Pendezwa na Kila Mtu: Mradi wetu ni kumfikia kila mtu tunayeweza. Wakikumbuka hilo, wahubiri fulani wamefanikiwa kutolea ushahidi watu walio katika ofisi za madaktari, hospitali, makao ya kutunzia wagonjwa, ofisi za vikundi vya maendeleo, na vituo vya urekebishaji wa tabia kwa waraibu wa dawa za kulevya na wa alkoholi. Kwa kuongezea, wahubiri wametolea ushahidi wale wenye kupanga mazishi, wasimamizi na washauri wa shule, na mahakimu. Unapowaendea maofisa mbalimbali, inafaa kuwaeleza unawathamini kwa sababu ya huduma zao zenye kusaidia wanazoipa jamii. Uwe mwenye staha, na uchague makala ya wakati ufaao yanayoshughulikia aina yao hasa ya kazi na matatizo wanayopata kutokana nayo.

4 Katika kisa kimoja dada aliweza kuongea na hakimu katika ofisi yake. Baada ya mazungumzo yenye kuchangamsha, hakimu huyo alitoa maelezo haya: “Wajua mimi hupendelea nini kuhusu Mashahidi wa Yehova? Wana kanuni zilizo imara ambazo huwa hawaziachi.” Mtu huyo mashuhuri alitolewa ushahidi mzuri.

5 Hatuwezi kusoma mioyo ya watu. Hata hivyo, kwa kuongea na kila mtu tumkutaye, twaonyesha imani katika uwezo wa Mungu wa kuongoza kazi yetu. Na zaidi, hiyo huwapa watu pendeleo la kusikia na kuitikia ujumbe wa tumaini. (1 Tim. 2:3, 4) Acheni tutumie wakati wetu kwa hekima na tujitahidi kuiga sifa ya Yehova ya kutobagua kwa kuhubiria watu wote tunaoweza habari njema.—Rom. 2:11; Efe. 5:1, 2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki