Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 7/15 kur. 21-24
  • Unaweza Kupita Vizuizi Hivi!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kupita Vizuizi Hivi!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Umechoshwa na Hali?
  • Kuvunjwa Moyo na Kielelezo Kibaya?
  • Je, Kuwa Shahidi Kwaonekana Kuwa Kugumu Sana?
  • Dumisha Mwendo wa Kuendelea
  • Jinsi Yehova Anavyotuongoza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Vijana Wenye Furaha Katika Utumishi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Je, Mungu Hutangulizwa Katika Familia Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kwa Nini Tukutanike Pamoja?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 7/15 kur. 21-24

Unaweza Kupita Vizuizi Hivi!

NDEGE kubwa yaweza kubeba mamia ya wasafiri na tani za mizigo. Ndege nzito kama hiyo yawezaje kupaa juu? Kwa njia ya lifti pekee.

Ndege ikimbiapo uwanjani, hewa hupita kwa kasi juu na chini ya mbawa zilizopindika. Tendo hili hutokeza mwinuko wa kuelekea juu uitwao lifti. Lifti ya kutosha inapochochewa, ndege yaweza kupaa juu na kuruka. Bila shaka, ndege inayobeba mizigo kupita kiasi haiwezi kuchochea lifti ya kutosha ili iwe na hewa ya kutosha.

Sisi pia twaweza kulemewa. Karne nyingi zilizopita, Mfalme Daudi alisema kwamba ‘dhambi zake zilimlemea mno.’ (Zaburi 38:4) Vilevile, Yesu Kristo alionya dhidi ya kulemewa na masumbufu ya maisha. (Luka 21:34) Mawazo na hisia zisizofaa zaweza kutulemea kiasi cha kwamba huenda ikawa vigumu kupata “hewa ya kutosha.” Je, wewe umelemewa hivyo? Au je, umewahi kuona kizuizi cha kuendelea kwako zaidi kiroho? Ikiwa ndivyo, ni nini chaweza kusaidia?

Je, Umechoshwa na Hali?

Kuchoshwa na hali—tatizo la kawaida leo—kwaweza kuwa kizuizi cha akilini, hata kwa baadhi ya watu wa Yehova. Wachanga hasa wana mwelekeo wa kuacha utendaji fulani wanaouona kuwa wenye kuchosha. Je, wakati mwingine wewe huhisi hivyo kuhusu mikutano ya Kikristo? Ikiwa ndivyo, unaweza kufanya nini ili ufanye kuhudhuria kwako mikutano kuwe kwenye kusisimua?

Kuhusika mikutanoni ni jambo la msingi. Paulo aliandikia kijana Timotheo hivi: “Ujizoeze kupata utauwa. Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.” (1 Timotheo 4:7, 8) Kitabu cha mazoezi ya mwili chaweza kuwa kisichopendeza na chenye thamani ndogo ikiwa hatukufuata mazoezi yote yanayopendekezwa. Mikutano ya Kikristo imekusudiwa kuzoeza akili zetu na itafanya hivyo ikiwa tunatayarisha na kushiriki. Kuhusika huku kutafanya mikutano iwe yenye kuthawabisha na kupendeza zaidi.

Kuhusiana na hilo, mwanamke mchanga Mkristo aitwaye Mara alisema hivi: “Nisipotayarisha mikutano, siifurahii. Walakini, ninapokuwa nimetayarisha kimbele, akili na moyo wangu huwa tayari zaidi kusikiliza. Mikutano huwa yenye maana zaidi, nami hutazamia kutoa maelezo.”

Kujifunza kusikiliza kutasaidia pia. Kusikiliza muziki mtamu ni rahisi na huleta raha mara moja. Lakini si uradhi wote ulio wa mara moja. Tunapata uradhi kutokana na programu ya mikutano tusikilizapo tu kwa makini yale yanayosemwa. Mkristo aitwaye Rachel alionelea hivi: “Msemaji asiposema kwa kuvutia, inanibidi kusikiliza kwa makini sana. Kanuni yangu ni, ‘Hotuba isipovutia sana, ndivyo ninavyohitaji kusikiliza kwa makini zaidi.’ . . . Mimi hupa maandiko uangalifu wa kipekee, nikijaribu kupata mengi iwezekanavyo kutoka kwayo.” Tunahitaji kujitia nidhamu, kama vile Rachel, ili tusikilize. Kitabu cha Mithali husema: “Mwanangu, sikiliza hekima yangu; tega sikio lako, mzisikie akili zangu.”—Mithali 5:1.

Habari fulani inayotolewa mikutanoni huenda ikawa yenye kurudiwarudiwa. Jambo hili ni la lazima! Watumishi wote wa Mungu wahitaji vikumbusha. Mwili usiokamilika, pamoja na mielekeo yawo mipotovu na kumbukumbu lenye kasoro, unahitaji msaada wowote uwezao kupata. Mtume Petro ‘alikuwa tayari kuwakumbusha waamini wenzake mambo fulani, ijapokuwa waliyajua na kuthibitika katika kweli waliyokuwa nayo.’ (2 Petro 1:12) Yesu pia alieleza kwamba “kila mwandishi . . . amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.” (Mathayo 13:52) Hivyo, ingawa mikutano yetu huwa na mawazo tujuayo ya Kimaandiko, au ‘hazina za kale,’ sikuzote kuna ‘hazina mpya’ za kutupendeza.

Kuazimia kupata faida zote mikutanoni kunaweza kuleta kitia moyo halisi cha kiroho. “Wenye furaha ni wale wenye kutambua uhitaji wao wa kiroho [wale walio maskini wa roho],” Yesu akasema. (Mathayo 5:3, NW, kielezi chini) Mtazamo kama huo kuelekea chakula chenye kujenga cha kiroho kiandaliwacho mikutanoni utaondolea mbali kuchoshwa na hali.—Mathayo 24:45-47.

Kuvunjwa Moyo na Kielelezo Kibaya?

Je, umewahi kuudhiwa na tabia ya mtu fulani katika kutaniko lenu? Labda ulishangaa, ‘Ndugu awezaje kutenda namna hii na bado awe na msimamo mzuri?’ Mawazo kama hayo yaweza kutumika kuwa kizuizi cha akilini, yakituzuia tusitambue thamani ya uhusiano wenye kupendeza tuwezao kupata pamoja na watu wa Mungu.—Zaburi 133:1.

Labda washiriki fulani wa kutaniko katika Kolosai walikuwa na tatizo kama hilo. Paulo aliwasihi hivi: “Mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake.” (Wakolosai 3:13) Paulo alitambua kwamba Wakristo fulani Wakolosai huenda walijiendesha kwa njia mbaya na hivyo huenda waliwapa wengine sababu ya kweli ya kulalamika. Hivyo hatupaswi kushangaa kupita kiasi ikiwa mmoja wa ndugu au dada zetu kwa kipindi fulani anakosa sifa fulani ya Kikristo. Yesu alitoa shauri lenye kutumika la kushughulikia tofauti nzito. (Mathayo 5:23, 24; 18:15-17) Lakini wakati mwingi, tunaweza kuchukuliana na mapungukio ya waamini wenzetu na kuwasamehe. (1 Petro 4:8) Kwa kweli, kuona mambo kwa jinsi hiyo kunaweza kuwa kwa faida yetu na ya wengine. Kwa nini ndivyo ilivyo?

“Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; nayo ni fahari yake kusamehe makosa,” yasema Mithali 19:11. Ni jambo bora kama nini kusamehe badala ya kuchochea hasira na ghadhabu! Salvador, mzee ajulikanaye kwa roho yake ya upendo, alisema hivi: “Ndugu anitendeapo vibaya au asemapo neno lisilo la fadhili, mimi hujiuliza: ‘Nawezaje kumsaidia ndugu yangu? Nawezaje kuzuia kupoteza uhusiano wangu wenye thamani pamoja naye?’ Sikuzote mimi hujua jinsi ilivyo rahisi kusema jambo lisilofaa. Mtu asemapo bila kufikiri, suluhisho la kweli lingekuwa afutilie mbali alilosema na kuanza tena. Lakini hilo haliwezekani, hivyo mimi nachukua mwendo unaofaa na kuachana na lililosemwa. Mimi hulihusisha na mwili usiokamilika badala ya utu halisi wa ndugu yangu.”

Huenda ukahisi kwamba kusema jambo hili ni rahisi kuliko kulitenda. Lakini mengi yanahusika na jinsi tunavyoongoza kufikiri kwetu. “Mambo yo yote yaliyo ya kweli, . . . yatafakarini hayo,” Paulo akashauri. (Wafilipi 4:8) “Kupendeza” kwa halisi humaanisha “kutokeza shauku.” Yehova anataka tufikirie yaliyo mema katika watu, tufikirie hayo yanayotokeza shauku badala ya ghadhabu. Yeye mwenyewe hutupa kielelezo cha hali ya juu kuliko zote katika jambo hili. Mtunga-zaburi alitukumbusha juu ya hilo, akisema: “Kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?”—Zaburi 103:12; 130:3.

Kweli, wakati mwingine tabia ya ndugu yaweza kuwa yenye kukatisha tamaa, lakini waabudu wenzetu walio wengi ni mifano bora ya maisha ya Kikristo. Tukikumbuka jambo hili, kama Daudi tutakuwa wenye furaha ‘kumshukuru BWANA na kumsifu katikati ya makutano.’—Zaburi 109:30.

Je, Kuwa Shahidi Kwaonekana Kuwa Kugumu Sana?

Kwa kusikitisha, kwa sababu ya kizuizi kingine cha akilini, wengine hawajaanza kumsifu Yehova. Wanaume wengi ambao si Mashahidi wa Yehova wanachukua daraka la kutunza familia zao na hata kutegemeza wake zao katika huduma ya Kikristo. Wao ni wenye urafiki na huenda wakapendezwa na kutaniko, lakini wanaepuka kuwa watumishi wa Mungu waliojiweka wakfu. Ni nini kinachowazuia?

Tatizo moja huenda likawa kwamba waume hawa wanaona utendaji wa kitheokrasi wenye shughuli nyingi wa wake zao na kuhisi kwamba kuwa Shahidi ni kwenye kudai mno. Au labda wanaogopa kwamba hawawezi kamwe kushiriki katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Kwa maoni yao, madaraka hayo yanaonekana mengi kuliko baraka. Kwa nini kizuizi hicho cha akilini? Wanafunzi wengi wa Biblia hujifunza na kutumia kweli polepole. Lakini waume wasioamini mara nyingi wanajua sana madaraka yote ya Kikristo kabla hawajajenga msukumo wa kuyakubali.

Manuel, aliyekuwa katika hali hii, aeleza: “Karibu miaka kumi, niliandamana na mke wangu kwenye makusanyiko na kwenye mikutano. Kusema kweli, nilipendelea ushirika wa Mashahidi kuliko ule wa watu wa ulimwengu, nami nilifurahi kuwasaidia nilipoweza kufanya hivyo. Nilivutiwa na upendo ulioenea miongoni mwao. Lakini wazo la kwenda nyumba kwa nyumba lilikuwa kizuizi kikubwa kwangu, nami niliogopa kwamba wafanyakazi wenzangu wangenidhihaki.

“Mke wangu alikuwa mwenye subira sana nami na hakujaribu kamwe kunilazimisha kujifunza Biblia. Yeye na watoto vilevile ‘walihubiri’ hasa kwa kielelezo chao kizuri. José, mzee katika kutaniko, alionyesha upendezi wa pekee kwangu. Nafikiri ni kitia moyo chake kilichonifanya mwishowe nianze kujifunza kwa bidii. Baada ya kubatizwa, nilitambua kwamba vizuizi vya akilini ndivyo vilivyonizuia. Mara nilipoamua kumtumikia Yehova, nilihisi msaada wake katika kushinda woga wangu.”

Wake na wazee Wakristo wawezaje kusaidia waume kama vile Manuel kushinda kizuizi chao cha akilini? Funzo la Biblia laweza kujenga uthamini na tamaa ya kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa kweli, maarifa yaliyosawazika ya Maandiko ndiyo msingi wa kudhihirisha imani na kuwa na uhakika katika tumaini lililoko mbele.—Warumi 15:13.

Ni nini kitasaidia waume kama hao kukubali funzo la Biblia? Mara nyingi, urafiki pamoja na ndugu mwenye utambuzi kutanikoni waweza kuwa kisababishi cha kumfanya aamue. Pengine mzee au ndugu mwingine mwenye maarifa angeweza kupata kumjua mume huyo. Mara uhusiano mwema unapoanzishwa, yote ambayo huenda akahitaji ni mtu wa kumtolea funzo. (1 Wakorintho 9:19-23) Wakati uleule, mke Mkristo mwenye busara anaweza kushiriki mambo madogo-madogo ya kiroho pamoja na mume wake asiyeamini, akitambua kwamba huenda asitake kulazimishwa.—Mithali 19:14.

Kama vile Manuel alivyojifunza kwa mambo aliyoona, mara mtu apatapo uwezo wa kiroho, vizuizi vilivyo kama mlima huwa vidogo. Yehova hutia nguvu wale watamanio kumtumikia. (Isaya 40:29-31) Kwa uwezo wa Mungu pamoja na kuungwa mkono na Mashahidi wakomavu, vizuizi huenda vikaondolewa. Hivyo kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba inaweza kuwa isiyoogopesha sana, na wafanyakazi wenzi wasiwe wenye kutisha sana, huku utumishi wa nafsi yote ukiwa wenye kuvutia zaidi.—Isaya 51:12; Warumi 10:10.

Dumisha Mwendo wa Kuendelea

Inawezekana kupita vizuizi kama vile vitatu tulivyofikiria. Wakati ndege ianzapo mwendo, kiasi kikubwa cha nguvu kutoka kwenye injini kwa kawaida huhitajiwa na vilevile uangalifu usiogawanyika wa kundi la wafanyakazi wayo. Wakati wa kuanza mwendo, injini hutumia petroli kiasi kikubwa kuliko wakati mwingine wowote wa kusafiri hewani. Sawa na hilo, kuachana na mawazo na hisia zisizofaa huhitaji jitihada kiasi kikubwa na kukaza fikira. Kuanza huenda kukawa sehemu iliyo ngumu zaidi, kisha maendeleo huwa rahisi mara mwendo wa kuendelea upatikanapo.—Linganisha 2 Petro 1:10.

Maendeleo hudumishwa kwa kutii kwa uharaka kitia moyo cha Kimaandiko. (Zaburi 119:60) Tunaweza kuwa na hakika kwamba kutaniko litataka kusaidia. (Wagalatia 6:2) Hata hivyo, la maana zaidi ya yote, ni utegemezo wa Yehova Mungu. Kama Daudi alivyosema, “Na ahimidiwe Bwana, siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu.” (Zaburi 68:19) Tujiondoleapo mzigo kwa sala, mzigo wetu huwa mwepesi.

Mara nyingine, ndege huondoka wakati halihewa ni yenye unyevu na mawingu, hupita mawingu, na kuruka hadi kwenye mbingu zilizojaa mwangaza wa jua. Sisi pia twaweza kuacha nyuma mawazo yasiyofaa. Kwa msaada wa kimungu, tunaweza kupita mawingu, kwa usemi wa mfano, na kuingia katika mwangaza, mazingira yenye furaha ya familia ya ulimwenguni pote ya waabudu wa Yehova.

[Picha katika ukurasa wa23]

Kwa msaada wa Yehova, twaweza kupita vizuizi vya akilini

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki