Wimbo 45
Sala ya Shukrani
1. Yehova mwema, sifa ni zako,
Ni wewe tunayekuitia,
Twaja kwako, Musikia sala,
Twajiweka kwako ututunze.
Sisi watenda dhambi dhaifu;
Tunakuomba utusamehe.
Asante! kwa damu ya Mwanao.
Tunatamani utufundishe.
2. Wa furaha unaoalika
Nyuani za mafunzo na nuru.
Neno lako linatuongoza.
Tutaridhika na wema wako.
Nguvu zako za haki zatisha,
Hukumu yako inyoshe mambo.
Mungu wa wokovu ’Falme wako,
Tuuhubiri, hautashindwa.
3. Ulinzi wako ufurahishe;
Na ibada yako iwe kote.
Ufalme wako wa wema waja,
Magonjwa, kifo, huzuni kwisha.
Yesu ataharibu uovu.
Viumbe walie kwa furaha.
Kwa shangwe ya ushindi tuimbe:
“Sifa ni za Yehova Mufalme!”