Je, Wewe Huthamini Subira ya Yehova?
1 Kama Yehova hangekuwa mwenye subira kwa miaka 10, 20, na zaidi iliyopita, akiruhusu ushahidi zaidi utolewe, je, ungekuwa umejifunza kweli? Tunashukuru kama nini kwamba ameruhusu watu wengi zaidi “wafikie toba.” Hata hivyo, siku ya Yehova iliyo kuu ya hukumu “itakuja kama mwizi.” (2 Pet. 3:9, 10) Kwa sababu hiyo, subira ya Mungu haipaswi kueleweka vibaya kuwa kuchelewa kumaliza mfumo huu wa mambo.—Hab. 2:3.
2 Wahurumie Watu: Uvumilivu wa Yehova umeshinda ufahamivu wetu. Hatupaswi kupuuza kusudi lake. (Yona 4:1-4, 11) Yehova huona hali ya kuhurumiwa ya wanadamu naye huwahurumia. Yesu huhisi vivyo hivyo. Akihurumia umati aliohubiria, alitaka kazi ya evanjeli ipanuke hivi kwamba wengi zaidi wapate fursa ya kupata uhai wa milele.—Mt. 9:35-38.
3 Maafa na misiba itokeapo, je, mioyo yetu haihurumii watu wasioijua kweli? Leo watu ni kama “kondoo wasio na mchungaji” wakijaribu kukabiliana na kuelewa msukosuko uliopo ulimwenguni. (Mr. 6:34) Kwa kuhubiri habari njema kwa bidii, twafariji wale walio na mioyo yenye mwelekeo unaofaa na kuonyesha uthamini kwa subira ya Yehova.—Mdo. 13:48.
4 Kazi Yetu Ni ya Uharaka: Mwaka jana watu 323,439 walibatizwa na zaidi ya 14,000,000 walihudhuria Ukumbusho. Huo ni uwezekano ulioje wa wengi zaidi kuepuka uharibifu wa mfumo huu mwovu! Hatujui “umati mkubwa” utafikia idadi gani. (Ufu. 7:9) Hatujui utume wetu wa kuhubiri utaendelea mpaka lini. Lakini Yehova anajua. Habari njema itahubiriwa mpaka atosheke, “na ndipo mwisho utakapokuja.”—Mt. 24:14.
5 Wakati ubakio ni mfupi, na siku ya Mungu inakaribia. (1 Kor. 7:29a; Ebr. 10:37) Pasipo shaka, “wokovu wetu uko karibu zaidi kuliko tulipopata kuwa waamini.” (Rom. 13:11) Na tusikose kuelewa kusudi la subira ya Mungu. Badala yake, na tuhubiri kwa uharaka ili wengi zaidi wanaotamani sana uadilifu wapate rehema kuu ya Yehova.