Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/05 uku. 6
  • Kujifunza Broshua Endeleeni Kukesha!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujifunza Broshua Endeleeni Kukesha!
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Mei 23
  • Juma Linaloanza Mei 30
  • Juma Linaloanza Juni 6
  • Juma Linaloanza Juni 13
  • Juma Linaloanza Juni 20
Huduma ya Ufalme—2005
km 4/05 uku. 6

Kujifunza Broshua Endeleeni Kukesha!

Kuanzia juma linaloanza Mei 23 hadi Juni 20, 2005, makutaniko ulimwenguni pote yatajifunza broshua Endeleeni Kukesha! katika Funzo la Kitabu. Tafadhali tumia maswali yafuatayo kutayarisha na kuongoza mkutano huo. Wakati wa funzo, mafungu yanapaswa kusomwa na maandiko yaliyoonyeshwa yasomwe kadiri wakati unavyoruhusu.

Juma Linaloanza Mei 23

◼ Ukurasa wa 3-4: Ni tukio lipi kati ya yale yaliyoorodheshwa hapa ambalo limekuathiri wewe binafsi? Ni nini kinachoonyesha kwamba matukio hayo si matukio yasiyohusiana yanayotukia katika maeneo fulani tu?

◼ Ukurasa wa 5: Kwa nini unasadiki kwamba Mungu anajali? Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunamjali Mungu na kwamba tunathamini yale anayofanya?

◼ Ukurasa wa 6-8: Mathayo 24:1-8, 14 linasema nini kuhusu maana ya mambo yanayotukia ulimwenguni leo? Kulingana na 2 Timotheo 3:1-5, tunaishi katika kipindi gani cha wakati? Hizi ni siku za mwisho za nini? Ni nini kinachokusadikisha kwamba kwa kweli Biblia ni Neno la Mungu? Ni nini ule Ufalme tunaohubiri kuuhusu?

◼ Ukurasa wa 9-10: Kwa nini tunapaswa kufikiria kwa makini maamuzi tunayofanya kila siku na mambo tunayotanguliza maishani? (Rom. 2:6; Gal. 6:7) Unapopitia maswali yaliyo kwenye ukurasa wa 10, wewe hukumbuka maandiko gani unayopaswa kuzingatia unapofanya maamuzi?

Juma Linaloanza Mei 30

◼ Ukurasa wa 11: Kwa nini sisi binafsi tunapaswa kuzingatia maswali yaliyo katika ukurasa huu? (1 Kor. 10:12; Efe. 6:10-18) Majibu yetu kwa maswali hayo huonyesha nini kuhusu jinsi tunavyozingatia shauri la Yesu kwenye Mathayo 24:44?

◼ Ukurasa wa 12-14: Ni nini ile “saa ya hukumu” inayotajwa katika Ufunuo 14:6, 7? ‘Kumwogopa Mungu na kumpa utukufu’ kunamaanisha nini? Babiloni Mkubwa ni nini, nao utapatwa na nini? Tunapaswa kuchukua hatua gani sasa kuhusiana na Babiloni Mkubwa? Saa ya hukumu iliyotabiriwa huhusisha matukio gani mengine? Kutojua “ile siku wala saa” ya kutekelezwa kwa hukumu ya Mungu kunatunufaishaje? (Mt. 25:13)

◼ Ukurasa wa 15: Ni nini lile suala la enzi kuu, na kila mmoja wetu anahusikaje katika suala hilo?

◼ Ukurasa wa 16-19: “Mbingu mpya” na “dunia mpya” ni nini? (2 Pet. 3:13) Ni nani anayetoa ahadi kuhusu mbingu mpya na dunia mpya? Ni mabadiliko gani yatakayoletwa na mbingu mpya na dunia mpya? Je, zitatufaidi sisi binafsi?

Juma Linaloanza Juni 6

◼ Ukurasa wa 20-21: Yesu aliwapa wanafunzi wake wa karne ya kwanza onyo gani kuhusu kukimbia kutoka katika eneo la hatari? (Luka 21:20, 21) Wangeweza kukimbia lini? Kwa nini ilikuwa muhimu kukimbia bila kukawia? (Mt. 24:16-18, 21) Kwa nini watu wengi hupuuza maonyo? Maelfu ya watu huko China na Ufilipino, walinufaikaje kwa kutii maonyo yanayotegemeka? Kwa nini ni muhimu sana kutii maonyo ya Biblia kuhusu mwisho wa mfumo huu wa mambo? Kwa kuwa wakati unaobaki ni mfupi sana, sisi tuna wajibu gani? (Met. 24:11, 12)

◼ Ukurasa wa 22-23: Kwa nini watu wengi huko Australia katika mwaka wa 1974, na Kolombia katika mwaka wa 1985, walipuuza maonyo kuhusu msiba, na walipatwa na ni nini? Unafikiri wewe ungeitikiaje maonyo hayo, na kwa nini? Ni nini kinachoweza kuonyesha jinsi ambavyo tungaliitikia onyo lililotolewa katika siku za Noa? Kwa nini watu walitamani kuishi ndani au karibu na jiji la kale la Sodoma? Tunaweza kunufaikaje kwa kufikiria kwa uzito kile kilichotukia Sodoma?

Juma Linaloanza Juni 13

◼ Ukurasa wa 24-27: Tumia “Maswali ya Funzo” kwenye ukurasa wa 27.

Juma Linaloanza Juni 20

◼ Ukurasa wa 28-31: Tumia “Maswali ya Funzo” kwenye ukurasa wa 31.

Kujifunza broshua hiyo kutatusaidia ‘kuendelea kukesha’ na kuwa tayari. Kazi yetu ya kuhubiri na ionyeshe umuhimu wa ujumbe huu wa malaika: “Mwogopeni Mungu na kumpa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imefika.”—Mt. 24:42, 44; Ufu. 14:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki