-
Endelea Kutangaza Kazi za Ajabu za YehovaHuduma ya Ufalme—2004 | Februari
-
-
watu unaofahamu kazini au shuleni, wanafunzi wa Biblia wa sasa au wa zamani, na marudio yako yote. Waangalizi wa funzo la kitabu wanapaswa kutia katika orodha yao wahubiri wowote wasiotenda.
14 Tumia mialiko ya Ukumbusho iliyochapwa, na uandike vizuri saa na mahali pa Ukumbusho. Au unaweza kutumia mwaliko ulio kwenye ukurasa wa mwisho wa gazeti la Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 2004 au Amkeni! la Machi 22, 2004. Wakumbushe wote ulioalika kwa kuwatembelea au kuwapigia simu kadiri Aprili 4 inavyokaribia.
15 Kwenye Ukumbusho: Jaribu kufika mapema siku ya Ukumbusho. Wakaribishe wapya kwa kuwasalimu kwa uchangamfu. (Rom. 12:13) Una daraka la pekee kwa wale unaowaalika. Wasalimu kwa uchangamfu, na uwajulishe kwa wengine kutanikoni. Labda unaweza kuwasaidia wapate kiti karibu nawe. Na ikiwa kuna yeyote ambaye hana Biblia au kitabu cha wimbo, shiriki pamoja naye au upange mtu mwingine ashiriki pamoja naye. Baada ya mwadhimisho, uwe karibu ili kujibu maswali ambayo huenda wakawa nayo. Ikiwa wengine wamefika kwa mara ya kwanza, waulize kama wangependa kujifunza Neno la Mungu na makusudi yake. Jitolee kujifunza Biblia nyumbani pamoja nao.
16 Endelea Kuwasaidia Wale Watakaohudhuria: Majuma yanayofuata Ukumbusho, huenda wale waliohudhuria wakahitaji msaada. Wanatia ndani wale ambao hapo wakati mmoja walikuwa wakihudhuria mikutano kwa ukawaida lakini sasa hawashirikiani sana na kutaniko. Wazee watakuwa macho kuona kwamba watu hao hawapuuzwi, nao watajaribu kujua kwa nini waliacha kufanya maendeleo ya kiroho. Waonyeshe uharaka wa nyakati hizi. (1 Pet. 4:7) Wasaidie wote waone faida za kutii himizo la Kimaandiko la kukutana na watu wa Mungu kwa ukawaida.—Ebr. 10:24, 25.
17 Kazi za Yehova ni za ajabu sana kwetu hivi kwamba hatuwezi kuzielewa kikamili hata tukiishi milele. (Ayu. 42:2, 3; Mhu. 3:11) Kwa hiyo, hatutakosa kamwe mambo ya kumsifia. Katika majira haya ya Ukumbusho tunaweza kuonyesha uthamini kwa ajili ya kazi za ajabu za Yehova kwa kufanya jitihada ya pekee kupanua huduma yetu.
-
-
Pitio La Shule Ya Huduma Ya KitheokrasiHuduma ya Ufalme—2004 | Februari
-
-
Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Februari 23, 2004. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa kuanzia juma la Januari 5 hadi Februari 23, 2004. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Tunaweza kufanya nini ili kuhakikisha kwamba wasikilizaji wanaelewa waziwazi jinsi ya kutumia habari inayotolewa na kwamba inawafaidi kwelikweli? [be uku. 158 fu. la 1-3]
2. Kwa nini tunapaswa kuchagua maneno kwa uangalifu? [be uku. 160 fu. 1 na sanduku la pili]
3. Ni jambo gani kuu linalohusu usemi mzuri ambalo linakaziwa katika 1 Wakorintho 14:9, na tunawezaje kutumia kanuni hiyo tunapowafundisha wengine? [be uku. 161 fu. 1-4]
4. Andiko la Mathayo 5:3-12 na Marko 10:17-21 yanaonyesha jambo gani bora la pekee kuhusu ufundishaji wa Yesu ambalo tunaweza kuiga? [be uku. 162 fu. 4]
5. Katika utumishi wetu au tunapotoa maelezo mikutanoni, kwa nini tunapaswa kujitahidi kutumia maneno yanayoonyesha mkazo, hisia, na yanayovutia? (Mt. 23:37, 38) [be uku. 163 fu. 3–uku. 164 fu. 1]
HOTUBA NA. 1
6. Kichwa kikuu cha hotuba ni nini, nacho kinawezaje kutusaidia kuchagua na kupanga habari kwa ajili ya hotuba? [be uku. 39 fu. 6–uku. 40 fu. 1]
7. (a) Kuwa safi kiroho kunamaanisha nini, na kwa nini usafi wa kiroho ni muhimu kuliko usafi wa aina nyingine? (b) Wakristo wanawezaje kukataa mambo yasiyo safi kiadili ambayo ni ya kawaida sana ulimwenguni? [w02 2/1 uku. 5-6]
8. Ni kanuni zipi zilizo muhimu zaidi? [w02 2/15 uku. 5 fu.1, 4, 6]
9. Hisia-mwenzi ni nini, na Yesu alionyeshaje sifa hiyo? [w02 4/15 uku. 25 fu. 4-5]
10. Andiko la Methali 11:11 linahusuje makutaniko ya watu wa Yehova? [w02 5/15 uku. 27 fu. 1-3]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. “Mti wa uzima” unaotajwa katika Mwanzo 2:9 unawakilisha nini?
12. Kwa nini mke wa Loti alipoteza uhai wake? (Mwa. 19:26) [w90 4/15 uku. 18 fu. 10]
13. Katika tamasha ya kiunabii ya Mwanzo sura ya 24, ni nani anayefananishwa na (a) Abrahamu, (b) Isaka, (c) Eliezeri, mtumishi wa Abrahamu (d) ngamia kumi, na (e) Rebeka?
14. Je, Mungu aliamuru kimbele mambo ambayo yangewapata Yakobo na Esau? (Mwa. 25:23)
15. Kwa nini jitihada yenye bidii ya Raheli, iliyobarikiwa na Yehova, ni mfano mzuri? (Mwa. 30:1-8) [w02 8/1 uku. 29-30]
-