Wimbo Na. 103
“Nyumba kwa Nyumba”
Makala Iliyochapishwa
1. Kila mlango, kila nyumba,
Neno twaeneza.
Kwenye miji na mashamba,
Kondoo walishwa.
Ufalme unatawala,
Ni habari njema.
Wazee hata vijana,
Wanazitangaza.
2. Kila mlango, kila nyumba,
Wokovu twataja.
Wanaomwita Yehova,
Wataokolewa.
Wataitaje jina la
Wasiyemujua?
Kila mlango, kila nyumba,
Jina twatangaza.
3. Kila mlango, basi twende,
Habari tweneze.
Wakubali, wakatae,
Wajiamulie.
Angalau jina Lake,
Twatangaza kote.
Sikuzote na tuende,
Kondoo tupate.
(Ona pia Mdo. 2:21; Rom. 10:14.)