Wimbo Na. 21
Wenye Furaha Ni Walio na Rehema!
Makala Iliyochapishwa
1. Wenye furaha ya kweli!
Ni walio na rehema.
Hujulisha watu wote,
Mungu apenda rehema.
Alionyesha rehema,
Kwa kumutoa Mwanaye.
Huwarehemu wapole,
Anajua tu dhaifu.
2. Wenye rehema hupata,
Baraka zake Yehova.
Wanaonyeshwa rehema.
Kristo anawatetea.
Wanarehemu wengine,
Kwa kulihubiri Neno,
Na kuwajulisha watu:
“Ufalme unatawala.”
3. Wapole watauona
Upendo wake Yehova.
Wataonyeshwa rehema,
Kwa kuwa wanamuiga.
Na tuwe wenye rehema
Kama Yehova na Kristo.
Na tuonyeshe rehema
Daima siku kwa siku.
(Ona pia Luka 6:36; Rom. 12:8; Yak. 2:13.)