Wimbo Na. 73
Pendaneni Sana Kutoka Moyoni
Makala Iliyochapishwa
1. Upendo na tuonyeshe,
Unaotoka moyoni;
Tuwe na hisia-mwenzi,
Kwao ndugu zetu.
Na waone waziwazi,
Tuna nia njema kwao.
Tuonyeshe ukarimu,
Tumuige Mungu.
Kwa neno na matendo,
Na tuwasaidie wote.
Tuwaonyeshe wema,
Tunapopata fursa.
Tuwaonyeshe heshima;
Na fadhili nyingi pia.
Tusifunue makosa,
Ya ndugu wala dada.
Tudumishe umoja.
2. Upendo tukiwa nao,
Hatutakasirika la.
Tunawaamini sana,
Ndugu zetu wote.
Tutakuwa marafiki,
Wanaothaminiana,
Wanaoshirikiana,
Kutiana moyo.
Kila siku twakosa;
Na kuwaumiza wengine.
Tuwe waangalifu,
Tusikwaze yeyote.
Urafiki tudumishe,
Sikuzote tupendane.
Pendo litutambulishe,
Na kutukuza Mungu;
Tumuige Yehova.
(Ona pia 1 Pet. 2:17; 3:8; 4:8; 1 Yoh. 3:11.)