Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rs uku. 257-uku. 260
  • Sala

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sala
  • Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mtu Akisema—
  • Kuhusu Sala Ambazo Mungu Anasikiliza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Namna ya Kupata Msaada kwa Sala
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Jinsi ya Kusali na Kusikiwa na Mungu
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
rs uku. 257-uku. 260

Sala

Maana: Maneno ya kuabudu, yanayoweza kusemwa kwa sauti kubwa au kimya-kimya katika mawazo ya mtu, yanayoelekezwa kwa Mungu wa kweli au kwa miungu ya uwongo.

Je, wewe unaona, kama wengine, kwamba sala zako hazijibiwi?

Mungu anapenda kusikiliza sala za nani?

Zab. 65:2; Mdo. 10:34, 35: “Ee msikiaji wa sala, kwako wewe watu wote wenye mwili watakuja.” “Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.” (Taifa, rangi ya ngozi, wala hali za kiuchumi za mtu si muhimu kuhusiana na jambo hili. Lakini jambo muhimu ni kile kinachouchochea moyo wa mtu na njia yake ya maisha.)

Luka 11:2: “Wakati wowote mnaposali, semeni, ‘Baba, jina lako na litakaswe.’” (Je, unatoa sala zako kwa Baba, ambaye Biblia inasema jina lake ni Yehova? Au, badala yake unatoa sala zako kwa “watakatifu”?)

Yoh. 14:6, 14: “Yesu akamwambia: ‘Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna anayekuja kwa Baba ila kupitia kwangu. Mkiomba jambo lolote katika jina langu, nitalifanya.’” (Je, wewe husali katika jina la Yesu Kristo, ukitambua kwamba ukiwa mwanadamu mwenye dhambi unahitaji kutetewa?)

1 Yoh. 5:14: “Na huu ndio uhakika ambao tunao kwake, kwamba, hata tukiomba nini kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.” (Hata hivyo, ili kuwa na uhakika huo, ni lazima kwanza ujue mapenzi ya Mungu. Kisha uhakikishe kwamba maombi yako yanapatana na mapenzi hayo.)

1 Pet. 3:12: “Macho ya Yehova yako juu ya waadilifu, na masikio yake yanaielekea dua yao; bali uso wa Yehova uko dhidi ya wale wanaotenda mambo mabaya.” (Je, umetenga wakati wa kujifunza yale ambayo Yehova anasema kupitia Neno lake kuhusu mambo ya uadilifu na mambo mabaya?)

1 Yoh. 3:22: “Chochote kile tunachoomba tunapokea kutoka kwake, kwa sababu tunazishika amri zake na tunafanya mambo yanayopendeza machoni pake.” (Je, kweli unatamani kumpendeza Mungu, na je, unajitahidi kutii amri zake ambazo tayari unazijua?)

Isa. 55:6, 7: “Mtafuteni Yehova, wakati anapoweza kupatikana. Mwiteni akiwa bado yupo karibu. Mtu mwovu aiache njia yake, na mtu mwenye madhara ayaache mawazo yake; naye arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema, na kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.” (Kwa rehema, Yehova anawaalika hata watu ambao wametenda mambo mabaya wamwombe katika sala. Lakini, ili wapate kibali cha Mungu, ni lazima watubu kwa unyoofu njia zao na mawazo yao mabaya na kubadili mwenendo wao.)

Ni nini kinachoweza kumfanya Mungu asikubali sala za mtu?

Mt. 6:5: “Wakati mnaposali, msiwe kama wanafiki; kwa sababu wanapenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kwenye pembe za njia pana ili waonekane na watu. Kwa kweli ninawaambia ninyi, Wanapata thawabu yao kwa ukamili.” (Pia Luka 18:9-14)

Mt. 6:7: “Mnaposali, msiseme mambo yaleyale tena na tena, kama vile watu wa mataifa wanavyofanya, kwa maana wao huwaza watasikiwa kwa kutumia maneno mengi.”

Met. 28:9: “Anayegeuzia mbali sikio lake asiisikie sheria [ya Mungu]—hata sala yake ni chukizo.”

Mika 3:4: “Wakati huo watamwomba Yehova msaada, lakini hatawajibu. Naye atauficha uso wake kutoka kwao wakati huo, kulingana na walivyotenda ubaya kwa matendo yao.”

Yak. 4:3: “Mnaomba, na bado hampokei, kwa sababu mnaomba kwa kusudi baya, ili mvitumie kwa tamaa zenu za mwili.”

Isa. 42:8, ZSB; Mt. 4:10, UV: “Mimi ni BWANA [“Yehova,” NW], ndilo jina langu; na utukufu wangu sitamupa mwingine, wala sanamu ya kuchonga sifa zangu.” “Msujudie Bwana Mungu [“Yehova Mungu,” NW] wako, umwabudu yeye peke yake.” (Pia Zaburi 113:4-8 [115:4-8], VB) (Sala ni namna ya ibada. Ukisali mbele ya vitu vya kuchongwa, au sanamu, je, hilo litampendeza Mungu?)

Isa. 8:19: “Nao wakiwaambia ninyi: ‘Toeni maombi kwa wenye kuwasiliana na pepo au kwa wale wenye roho ya kubashiri wanaonong’oneza na kusema maneno kwa sauti za chini,’ je, kundi lolote la watu halipaswi kutoa maombi kwa Mungu wake? Je, maombi yatolewe kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?”

Yak. 1:6, 7: “Na aendelee kuomba kwa imani, bila kutia shaka hata kidogo, kwa maana yeye anayetia shaka ni kama wimbi la bahari linaloendeshwa na upepo na kupeperushwa huku na huku. Kwa kweli, mtu huyo asidhani kwamba atapokea kitu chochote kutoka kwa Yehova.”

Ni mambo gani yanayofaa kutolewa sala?

Mt. 6:9-13: “Basi, ninyi msali hivi: ‘[1] Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. [2] Ufalme wako na uje. [3] Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. [4] Utupe leo mkate wetu kwa ajili ya siku hii; na [5] utusamehe madeni yetu, kama vile ambavyo sisi pia tumewasamehe wadeni wetu. Na [6] usituingize katika jaribu, bali utukomboe kutokana na yule mwovu.’” (Ona kwamba jina la Mungu na kusudi lake vinapaswa kutangulizwa.)

Zab. 25:4, 5: “Nijulishe njia zako, Ee Yehova; nifundishe mapito yako mwenyewe. Nitembeze katika kweli yako na kunifundisha, kwa maana wewe ni Mungu wangu wa wokovu.”

Luka 11:13: “Ikiwa ninyi, mjapokuwa waovu, mnajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi zilizo njema, je, Baba aliye mbinguni hatawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomwomba!”

1 The. 5:17, 18: “Salini bila kuacha. Kuhusiana na kila jambo toeni shukrani.”

Mt. 14:19, 20: “[Yesu] akachukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akatoa baraka na, baada ya kuimega ile mikate, akawagawia wanafunzi, nao wanafunzi wakaugawia ule umati. Kwa hiyo wote wakala wakashiba.”

Yak. 5:16: “[M]sali kwa ajili ya mtu na mwenzake.”

Mt. 26:41: “Endeleeni kukesha na kusali sikuzote, ili msiingie katika jaribu.”

Flp. 4:6: “Msihangaike juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.”

Mtu Akisema—

‘Tuombe kwanza, kisha unipe ujumbe wako’

Unaweza kujibu hivi: ‘Ninafurahi kujua kwamba wewe unafahamu umuhimu wa sala. Mashahidi wa Yehova pia husali kwa ukawaida. Lakini kuna jambo ambalo Yesu alisema kuhusu wakati na jinsi ya kusali ambalo huenda likawa jipya kwako. Je, unajua kwamba aliwaambia wanafunzi wake wasisali hadharani ili wengine waone kwamba wao ni watu wa dini, watu wenye kusali? . . . (Mt. 6:5)’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Ona yale ambayo alisema tunapaswa kuyahangaikia zaidi na ambayo tunapaswa kutanguliza katika sala zetu. Hayo ndiyo mambo ambayo nimekuja kukueleza. (Mt. 6:9, 10)’

Au unaweza kusema: ‘Ninajua kwamba washiriki wa vikundi fulani vya kidini hufanya hivyo. Lakini Mashahidi wa Yehova hawafanyi hivyo, kwa sababu Yesu aliwaagiza wanafunzi wake wafanye kazi yao ya kuhubiri kwa njia tofauti. Badala ya kusema, “mnapoingia ndani ya nyumba, salini kwanza,” ona aliyosema, kama yalivyoandikwa katika Mathayo 10:12, 13. . . . Na ona hapa katika mstari wa 7 jambo walilopaswa kuzungumzia. . . . Ufalme huo unaweza kuwasaidiaje watu kama mimi na wewe? (Ufu. 21:4)’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki