Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/13 uku. 1
  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Amosi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo—Amosi
  • Huduma ya Ufalme—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Sema Neno la Mungu kwa Ujasiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Kitabu Cha Biblia Namba 30—Amosi
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kifo cha Taifa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Hukumu ya Yehova Itakuja Juu ya Waovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2013
km 9/13 uku. 1

Wachukueni Manabii Kuwa Kielelezo​—Amosi

1. Kwa nini mfano wa Amosi unaweza kututia moyo?

1 Je, umewahi kuhisi hustahili kuhubiri kwa sababu una elimu ndogo na hali ya chini ya maisha? Ikiwa ndivyo, unaweza kupata ujasiri kupitia mfano wa Amosi. Ingawa alikuwa mchungaji wa kondoo na kibarua tu, Yehova alimpa nguvu za kuhubiri ujumbe muhimu. (Amo. 1:1; 7:14, 15) Vivyo hivyo leo, Yehova huwatumia watu wanyenyekevu. (1 Kor. 1:27-29) Ni mambo gani mengine tunayoweza kujifunza kutoka kwa nabii Amosi yatakayotusaidia katika kazi yetu ya kuhubiri?

2. Licha ya upinzani, kwa nini tunaweza kubaki imara tunapohubiri?

2 Simama Imara Licha ya Upinzani: Amazia, kuhani aliyeabudu ndama katika ufalme wa makabila kumi ya taifa la Israeli alipomsikia Amosi akitoa unabii, ni kana kwamba alimwambia ‘Nenda nyumbani! Achana na sisi! Tuna dini yetu!’ (Amo. 7:12, 13) Alipokuwa akizungumza na Mfalme Yeroboamu, Amazia aliyapotosha maneno ya Amosi ili Mfalme huyo aipige marufuku kazi ya Amosi. (Amo. 7:7-11) Lakini Amosi hakuogopa. Leo, makasisi fulani hutafuta msaada wa wanasiasa ili wawatese watu wa Yehova. Hata hivyo, Yehova anatuhakikishia kwamba hakuna silaha yoyote itakayofanywa dhidi yetu itakayofaulu.​—Isa. 54:17.

3. Ujumbe tunaohubiri unatimiza mambo gani mawili?

3 Tangaza Hukumu ya Mungu na Baraka Zitakazokuja: Ingawa Amosi alitabiri ujumbe wa hukumu dhidi ya ufalme wa makabila kumi ya taifa la Israeli, alikamilisha kuandika kitabu kinachoitwa kwa jina lake kwa kutaja baraka nyingi ambazo Yehova ataleta. (Amo. 9:13-15) Sisi pia tunahubiri kuhusu “siku ya hukumu” ya Mungu inayokuja, hata hivyo hiyo ni sehemu tu ya “habari njema ya ufalme” ambayo ni lazima tuhubiri. (2 Pet. 3:7; Mt. 24:14) Yehova atawaharibu waovu katika vita vya Har–Magedoni na kisha dunia itageuzwa kuwa paradiso.​—Zab. 37:34.

4. Tuna uhakika gani kwamba tunaweza kutimiza mapenzi ya Yehova?

4 Tunaonyesha kwamba tumejitoa kwa Yehova na tumeazimia kabisa kufanya mapenzi yake, tunapojitahidi kuhubiri kuhusu Ufalme wake katika ulimwengu huu uliojaa wapinzani. (Yoh. 15:19) Hata hivyo, tuna uhakika kwamba Yehova ataendelea kuandaa yote tunayohitaji ili tufanye mapenzi yake kama Amosi.​—2 Kor. 3:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki