Wimbo Na. 114
Kitabu cha Mungu Ni Hazina
Makala Iliyochapishwa
1. Kuna kitabu kinacholetea,
Watu amani na tumaini.
Mawazo yake yana nguvu nyingi;
Kinafumbua macho ya watu.
Ni Biblia takatifu ya Mungu.
Iliandikwa kale na watu.
Waliomupenda Yehova sana,
Walichochewa na roho yake.
2. Waliandika kuhusu ’umbaji,
Ulimwengu ulivyotokea.
Ukamilifu wa mutu mwanzoni,
Paradiso ilivyopotea.
Pia kuhusu malaika ’moja
Ambaye kapinga enzi kuu.
Kisha dhambi, huzuni katokea,
Ushindi wa Yah waja upesi.
3. Leo twaishi pindi ya pekee.
Ufalme wa Mungu watawala.
Leo Yehova huwapa wokovu
Wote wanaomwendea Yeye.
Biblia inazo habari njema;
Ni chakula tele cha kiroho.
Huwapa watu wote tumaini;
Hiyo ni hazina kwelikweli.
(Ona pia 2 Tim. 3:16; 2 Pet. 1:21.)